Kujifunza kutokana na Vidio la Bible: un récit historique exact, des prophéties dignes de foi
Baada ya kutazama vidio hii, je, unaweza kujibu maulizo yafuatayo? (1) Ni nani aliye Chanzo cha habari yenye kutegemeka ya Biblia? (Dan. 2:28) (2) Biblia inatoaje maelezo sahihi kuhusu Misri ya kale, na unabii unaoandikwa kwenye Isaya 19:3, 4 ulikuja kuwa wa kweli namna gani? (3) Akiolojia imehakikishaje wazo ambalo Biblia inatoa kuhusu Wasiria, wafalme wao, na mwisho wa Siria? (Nah. 3:1, 7, 13) (4) Ni unabii gani mbalimbali kuhusu Babiloni ulionekana kuwa wenye kutegemeka? (5) Umedi na Uajemi ulikuwa na uvutano gani juu ya watu wa Mungu? (6) Andiko la Danieli 8:5, 8 lilitimizwaje, na hilo lilitabiriwa kimbele sana kadiri gani? (7) Yesu alionekanaje kuwa ndiye Masiya wa kweli? (8) Ni tawala gani za kisiasa za sasa zinazotimiza unabii unaopatikana kwenye Ufunuo 13:11 na 17:11? (9) Katika vidio, ni picha gani zinazohakikisha ukweli wa Mhubiri 8:9? (10) Utoaji huu umetiaje nguvu imani yako katika ahadi za Biblia kuhusu wakati ujao? (11) Unawezaje kutumia chombo hiki ili kusadikisha wengine kwamba Biblia ilitoka kwa Mungu?