Video: Biblia—Simulizi la Kihistoria la Kweli, Unabii Wenye Kutegemeka
(La Bible : un récit historique exact, des prophéties dignes de foi)
Ni mambo gani yanayohakikisha kwamba Biblia inapatana na historia? Ni unabii gani mbalimbali ambao tayari umetimizwa unaotuhakikishia kwamba unabii kuhusu wakati ujao utatimizwa pia? Maulizo hayo yatajibiwa katika video La Bible : un récit historique exact, des prophéties dignes de foi, video ya tatu katika DVD La Bible : un livre historique et prophétique. Baada ya kutazama video hii, je, unaweza kujibu maulizo yafuatayo?
(1) Ni nani aliye Chanzo cha habari yenye kutegemeka ya Biblia? (Dan. 2:28) (2) Namna gani Biblia inatoa maelezo sahihi kuhusu Misri ya kale, na unabii unaoandikwa katika andiko la Isaya 19:3, 4 ulitimia namna gani? (3) Namna gani Akiolojia imehakikisha maelezo ya Biblia kuhusu Waashuru, wafalme wao, na uharibifu wa Ashuru? (Nah. 3:1, 7, 13) (4) Ni unabii gani mbalimbali kuhusu Babiloni ulioonekana kuwa wenye kutegemeka? (Yer. 20:4; 50:38; 51:30) (5) Ni unabii gani uliotimia kuhusu Umedi na Uajemi? (Isa. 44:28) (6) Maandiko ya Danieli 7:6 na 8:5, 8 yalitimizwa namna gani kuhusu Ugiriki? (7) Andiko la Danieli 7:7 lilitimia namna gani Roma ilipokuwa serikali kuu ya ulimwengu? (8) Ni Makaisari gani wanaozungumziwa katika Biblia? (9) Wakati wa utawala wa Nero, Wakristo walipatwa na nini? (10) Unabii unaopatikana katika andiko la Ufunuo 13:11 na 17:10 ulitimia namna gani? (11) Mfalme wa nane anafananisha nani? (12) Ni mambo gani yaliyoonyeshwa katika video yanayohakikisha ukweli wa Mhubiri 8:9? (13) Ni unabii gani mbalimbali kuhusu wakati ujao ambao wewe unangojea kwa hamu uone utimizo wake? (14) Namna gani unaweza kutumia video hii ili kusadikisha wengine kwamba Biblia iliongozwa na roho ya Mungu?