Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/01 uku. 1
  • “Kwa Mungu mambo yote yawezekana”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Kwa Mungu mambo yote yawezekana”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unawaza “Haiwezekane?”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • ‘Hii Habari Njema Itahubiriwa’!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Umuige Yesu, Ukuwe na Bidii kwa Ajili ya Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • ‘Muende Mufanye Wanafunzi Kutoka kwa Watu wa Mataifa Yote’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 4/01 uku. 1

“Kwa Mungu mambo yote yawezekana”

1 Kazi ya msingi ya kutaniko la Kikristo ni kuhubiri ujumbe wa Ufalme ulimwenguni pote. (Mt. 24:14) Hilo ni daraka kubwa sana. Kwa watazamaji wengi, kazi hiyo inaonekana kuwa yenye kuomba mali nyingi zaidi kuliko ile tuliyo nayo. Kwa wengine, kutimiza mgawo huo ni jambo ambalo kwa kweli haliwezekani kwa kuwa sisi tunadhihakiwa, tunapingwa, na tunateswa. (Mt. 24:9; 2 Tim. 3:12) Watu wenye mashaka-mashaka wanasadiki kwamba kazi hii ni jambo lisilowezekana kutimiza. Hata hivyo, Yesu alisema: “Kwa Mungu mambo yote yawezekana.”—Mt. 19:26.

2 Mifano yenye kufaa ya kuiga: Yesu alianza huduma yake akiwa mtu mmoja dhidi ya mfumo mzima wa mambo. Ili kujaribu kumzuia asifanikiwe, wapinzani walimshushia heshima kwa njia zote zinazoweza kuwazika; baadaye wakamfanya apatwe na kifo chenye maumivu makali. Hata hivyo, mwishoni, Yesu alisema kwa uhakika: “Nimeushinda ulimwengu.” (Yn. 16:33) Timizo lisiloweza kuaminika kwelikweli!

3 Wanafunzi wa Yesu walionyesha roho hiyohiyo ya uhodari na ya bidii katika huduma ya Kikristo. Wengi walipigwa fimbo, walitupwa gerezani, na hata kuuawa. Hata hivyo, walikuwa “wakishangilia kwa sababu walikuwa wamehesabiwa wenye kustahili kuvunjiwa heshima kwa ajili ya jina lake.” (Mdo. 5:41) Ingawa mambo ambayo yangeweza kuwapata, walitimiza ile kazi iliyoonekana kuwa isiyowezekana ya kuhubiri habari njema “hadi sehemu ya mbali zaidi sana ya dunia.”—Mdo. 1:8; Kol. 1:23.

4 Jinsi ya kufanikiwa katika siku yetu: Sisi pia tumechukua kazi ya kuhubiri Ufalme ingawa matukio yaliyoonekana kuwa yasiyowezekana. Ingawa marufuku, mateso, kufungwa gerezani, na majaribio mengine yenye jeuri ya kutusimamisha, sisi ni wenye kufanikiwa. Hilo linawezekanaje? “Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, lakini kwa Roho yangu, BWANA anasema.” (Zek. 4:6) Kwa kuwa tuna utegemezo wa Yehova, hakuna kitu kinachoweza kusimamisha kazi yetu!—Rom. 8:31.

5 Wakati tunapohubiri, hatuna sababu yoyote ya kuona haya wala kuogopa wala kujisikia kuwa wasiostahili. (2 Kor. 2:16, 17) Tunazo sababu zenye kuzidi za kusonga mbele katika kueneza habari njema ya Ufalme. Kwa msaada wa Yehova, tutatimiza “mambo yasiyowezekana”!—Luka 18:27.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine