Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/02 uku. 8
  • Wazazi—Zoezeni Watoto Wenu Tangu Utoto

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wazazi—Zoezeni Watoto Wenu Tangu Utoto
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Muwazoeze Watoto Wenu Wawe Wahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 1/02 uku. 8

Wazazi​—Zoezeni Watoto Wenu Tangu Utoto

1 “Fundisha [zoeza, NW] mutoto katika njia inayomupasa kwenda, na hata wakati atakapokuwa muzee hataiacha.” (Mez. 22:6) Wazazi, ikiwa hampendi watoto wenu ‘waache’ njia ya ile kweli, mazoezi hayo yanapaswa kuanza wakati gani? Mapema katika maisha!

2 Mtume Paulo aliposema kwamba elimu ya kiroho ya Timotheo ilikuwa “tangu utoto sana,” kwa wazi alimaanisha tangu alipokuwa mtoto mchanga. (2 Tim. 3:​14, 15) Kama tokeo, Timotheo alikomaa akawa mtu bora wa kiroho. (Flp. 2:​19-​22) Wazazi, nyinyi pia mnapaswa kuanza “tangu utoto sana” kuwapa watoto wenu mazoezi wanayohitaji ili ‘kukomaa mbele ya Yehova.’​—1 Sam. 2:​21.

3 Wapeni Maji Wanayohitaji ili Kukomaa: Kama vile tu miti michanga inavyohitaji kiasi cha maji kilicho cha kawaida ili kukomaa kuwa miti mikubwa, watoto wa umri zote wanahitaji kupewa kwa wingi maji ya ile kweli ya Biblia ili wafikie kuwa watumishi wakomavu wa Mungu. Njia ya msingi ya kufundisha watoto kweli na kuwasaidia wapate uhusiano wa kirafiki pamoja na Yehova ni kupitia funzo la Biblia la kawaida katika familia. Lakini wazazi, fikirieni uwezo wa kukaza akili wa kila mtoto. Kwa watoto wadogo, yaelekea vipindi vingi vya funzo vyenye kufupishwa vitakuwa vyenye matokeo zaidi kuliko vipindi vichache virefu.​—Kum. 11:​18, 19.

4 Msipuuze kamwe uwezo wa kujifunza wa watoto wenu. Waelezeeni hadithi kuhusu watu wa kibiblia. Waombeni wachape picha za matukio ya Biblia au kucheza matukio hayo. Fanyeni matumizi mazuri ya vidio na kaseti zetu za kusikiliza, kutia ndani drama za kibiblia. Rekebisheni funzo la familia ili kulipatanisha na umri na uwezo wa kujifunza wa watoto wenu. Mazoezi ya kwanza yatakuwa ya kimsingi, yakitolewa kwa kiasi kidogo; lakini mtoto anapokomaa, mazoezi yake yanapaswa kuwa yenye kupanuka zaidi na yenye kuendelea. Fanyeni mafundisho ya Biblia yawe na habari tofauti-tofauti na yawe yenye uchangamfu. Mnataka watoto wenu “wafanyize hamu sana” ya lile Neno; kwa hiyo, fanyeni funzo liwe lenye kupendeza zaidi mwezavyo.​—1 Pet. 2:2.

5 Wahusisheni Katika Kutaniko: Wekeeni watoto wenu miradi yenye kuendelea kusudi wapate kuhusika kikamili katika kutaniko. Ni nini unaoweza kuwa mradi wao wa kwanza? Wazazi wa watoto wawili wachanga walisema: “Wote wawili walianza kupokea mazoezi ya kukaa kimya katika Jumba la Ufalme.” Baadaye, saidieni watoto watoe maelezo katika maneno yao wenyewe kwenye mikutano, na mwasaidie wajiwekee mradi wa kujiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. Katika utumishi wa shambani, miradi mizuri ya kufikia inaweza kuwa kutoa trakti kwenye mlango, kusoma andiko, kufanya utoaji wa gazeti, na kuhusisha wenye nyumba katika mazungumzo yenye maana.

6 Iweni Mifano Yenye Shauku: Je, watoto wenu wanawasikia nyinyi mkisema kila siku kuhusu Yehova na kumwomba katika sala? Je, wanawaona mkijifunza Neno lake, mkihudhuria mikutano, mkishiriki katika huduma ya shambani, na mkipata furaha katika kufanya mapenzi ya Mungu? (Zab. 40:8) Ni jambo la maana sana kwao kuwaona mkifanya hivyo na kufanya mambo hayo pamoja nao. Binti mmoja aliyekomaa alisema hivi kuhusu mama yake, ambaye alilea watoto sita mpaka wakawa Mashahidi waaminifu: “Jambo lililotuchochea zaidi ni mfano wa Mama mwenyewe​—ulitoa ujumbe wenye nguvu zaidi kuliko maneno.” Mzazi mmoja wa watoto wanne alisema: “ ‘Yehova ndiye tunayetanguliza’ hayakuwa maneno ya kawaida tu lakini njia ambayo katika hiyo tuliishi maisha yetu.”

7 Wazazi, anzeni mapema kuzoeza watoto wenu, mkiwafundisha kweli kutoka katika Neno la Mungu, mkiwawekea miradi yenye kuendelea, na mkiwa mifano bora zaidi iwezekanavyo. Mtakuwa wenye furaha kwa kufanya hivyo!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine