Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/11 uku. 7
  • Muwazoeze Watoto Wenu Wawe Wahubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Muwazoeze Watoto Wenu Wawe Wahubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wazazi—Zoezeni Watoto Wenu Tangu Utoto
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Fundisha Watoto Wako Kumsifu Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Wazazi, Musaidie Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2011
km 1/11 uku. 7

Muwazoeze Watoto Wenu Wawe Wahubiri

1. Zaburi 148:12, 13 inachochea wazazi Wakristo kufanya nini?

1 Yehova anawaalika vijana wamsifu. (Zab. 148:12, 13) Kwa hiyo, wazazi Wakristo wanafanya mengi zaidi ya kuwafundisha watoto wao kweli za Biblia na sheria za Mungu kuhusu mwenendo. Wanawazoeza pia kuwa wahubiri wa habari njema. Namna gani wanaweza kufanya hivyo hatua kwa hatua?

2. Namna gani mfano mzuri wa mzazi unaweza kuwasaidia watoto wake?

2 Muwaonyeshe Mfano Mzuri: Mwamuzi Gideoni aliwaambia wanaume wake 300: “Jifunzeni kwa kunitazama.” (Amu. 7:17) Kwa kawaida watoto wanawatazama na kuwaiga wazazi wao. Baba mmoja anatumika usiku, lakini kuliko kulala anaporudi nyumbani Siku ya Posho asubuhi, anaenda katika mahubiri na watoto wake hata ikiwa yeye ni mwenye kuchoka sana. Bila kusema jambo lolote, anawafundisha watoto wake kwamba kazi ya kuhubiri ndilo jambo la maana maishani. (Mt. 6:33) Je, watoto wako wanaona kwamba unashiriki kwa furaha katika sehemu mbalimbali za ibada, kama vile kusali, kusoma Biblia, kutoa maelezo kwenye mikutano, na kuhubiri? Ni kweli kwamba hauwezi kuwaonyesha mfano mkamilifu. Hata hivyo, watoto wako wanapoona kwamba una bidii katika kumtumikia Yehova, huenda watakubali yale unayowafundisha ili kumtumikia Yehova.​—Kum. 6:6, 7; Rom. 2:21, 22.

3. Ni miradi gani ya kiroho ambayo wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao wajiwekee na kufikia hatua kwa hatua?

3 Muwawekee Miradi Hatua kwa Hatua: Bila kuchoka, wazazi wanawazoeza watoto wao kutembea, kusema, kuvaa nguo, na mambo mengine. Watoto wanapofikia hatua fulani, wazazi wanaweza kuwawekea miradi mingine. Ikiwa wazazi ni Wakristo, wanawasaidia pia watoto wao wajiwekee na kufikia miradi ya kiroho kulingana na miaka na uwezo wao. (1 Kor. 9:26) Je, unawafundisha watoto wako jinsi ya kutoa maelezo kwa maneno yao kwenye mikutano, na kutayarisha wao wenyewe migawo yao kwenye Shule ya Huduma ya Kitheokrasi? (Zab. 35:18) Je, unawazoeza kushiriki katika sehemu mbalimbali za mahubiri? Je, unawachochea wajiwekee mradi wa kubatizwa na kufanya utumishi wa wakati wote? Je, unawasaidia wafanye urafiki na wahubiri wenye furaha na wenye bidii ambao wanaweza kuwatia moyo?​—Met. 13:20.

4. Namna gani watoto wanafaidika ikiwa wazazi wanaanza kuwazoeza kuwa wahubiri tangu utoto?

4 Mtunga-zaburi alisema hivi: “Ee Mungu, umenifundisha tangu ujana wangu, na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako za ajabu.” (Zab. 71:17) Tangu utoto, anza kuwazoeza watoto wako ili wawe wahubiri wa habari njema. Mazoezi ya kiroho unayowatolea wakati wangali watoto wadogo yatawasaidia hakika wanapokuwa watu wazima!​—Met. 22:6.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine