Fundisha Watoto Wako Kumsifu Yehova
1 Andiko la Zaburi 148:12, 13 linatia moyo vijana wanaume na wanawake “walisifu jina la Yehova.” Maandiko yanaonyesha mifano mingi ya watoto wadogo waliofanya hivyo. Kwa mfano, ‘Samweli alikuwa akitumika mbele za Yehova akiwa kijana.’ (1 Sam. 2:18) Ni ‘binti mdogo’ aliyemwambia muke wa Naamani kwamba nabii wa Yehova katika Israeli angemponyesha Naamani ukoma wake. (2 Fal. 5:1-3) Yesu alipoingia katika hekalu na kufanya matendo yenye nguvu, ni ‘vijana’ ndio waliopaza sauti na kusema: “Mwokoe Mwana wa Daudi, tunaomba!” (Mt. 21:15) Namna gani wazazi wanaweza kufundisha watoto wao kumsifu Yehova?
2 Kuwafundisha Kupitia Mfano: Kabla ya kukazia kweli ndani ya mioyo ya watoto wao, baba Waisraeli waliagizwa wampende Yehova kwanza na kutia sheria zake ndani ya mioyo yao wenyewe. (Kum. 6:5-9) Ikiwa mnazungumzia kazi ya kuhubiri kwa njia yenye kutia moyo na kuitia katika programu yenu ya kila juma, watoto wenu wataona kazi ya kuhubiri kuwa ya maana na yenye kuleta furaha.
3 Dada mmoja anakumbuka kwa furaha hivi: “Nilipokuwa nikikomaa, familia yetu ilikuwa ikishiriki kwa ukawaida katika kazi ya kuhubiri kila Siku ya Posho na Siku ya Yenga. Niliona kwamba wazazi wangu walifurahia kabisa kazi ya kuhubiri. Tulikomaa tukiona kazi ya kuhubiri kuwa jambo lenye kupendeza.” Dada huyo alipata kuwa mhubiri asiyebatizwa akiwa bado na miaka saba na sasa ana zaidi ya miaka 32 katika utumishi wa wakati wote.
4 Kuwazoeza Polepole: Mhubiri pamoja na watoto wenu. Labda wanaweza kupiga hodi kwenye mlango, kumtolea msikilizaji trakti au kusoma andiko. Hilo litawafurahisha na kuwasaidia wawe hakika na uwezo wao wa kutangazia wengine habari ya Ufalme. Wanapokomaa, watashiriki zaidi katika kazi ya kuhubiri. Kwa hiyo, muwasaidie kufanya maendeleo na kufikiria miradi ya kiroho.
5 Muzungumze na wazee munapoona kwamba watoto wenu wanastahili kuwa wahubiri wasiobatizwa na wanapoonyesha nia hiyo. Kuwa mhubiri kutakazia akilini mwao daraka lao la kumsifu Yehova. Kumbuka kwamba, ili astahili kubatizwa, si lazima mtoto ajue mambo mengi zaidi sawa na watu wazima wenye kubatizwa. Je, mtoto wako anaelewa mafundisho ya mwanzo mwanzo ya Biblia? Je, anashika kanuni za Biblia za mwenendo mzuri? Je, ana nia ya kushiriki katika kazi ya kuhubiri na kujulikana kuwa Shahidi wa Yehova? Ikiwa jibu ni ndiyo, basi wazee wataamua kwamba anastahili kuwa mhubiri asiyebatizwa.—Ona kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, uku. 79-82.
6 Inaomba kufanya nguvu ili kuwafundisha watoto wamsifu Yehova kutoka moyoni. Hata hivyo, jambo linalofurahisha sana wazazi kuliko mambo mengine ni kuona watoto wao wakifanya maendeleo ya kiroho. Jambo la maana zaidi, Yehova ni mwenye furaha sana watoto wanapozungumzia wengine kuhusu kazi zake za ajabu.
[Maulizo ya Funzo]
1. Je, watoto wanaweza kumsifu Yehova?
2. Kwa nini ni jambo la maana wazazi waonyeshe watoto wao mfano mzuri?
3. Namna gani dada mmoja alifaidika kupitia mfano wa wazazi wake?
4. Namna gani tunaweza kuzoeza watoto polepole?
5. Ni mambo gani yanayoombwa ili mtoto astahili kuwa mhubiri asiyebatizwa?
6. Kwa nini ni jambo lenye kufaa wazazi wafundishe watoto wao?