Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/97 uku. 3
  • Wazazi—Muwazoeze Watoto Wenu Katika Mahubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Wazazi—Muwazoeze Watoto Wenu Katika Mahubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Fundisha Watoto Wako Kumsifu Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Muwazoeze Watoto Wenu Wawe Wahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Wazazi—Zoezeni Watoto Wenu Tangu Utoto
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Wazazi, Mufundishe Watoto Wenu Wamupende Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 7/97 uku. 3

Wazazi​—Muwazoeze Watoto Wenu Katika Mahubiri

1 Makutaniko yetu yanayo furaha kuhesabu kati ya washiriki wayo watoto wengi walio na tamaa nyofu ya kumtumikia Mungu. (Muh. 12:1) Wao ni kati ya wale wanaopokea mwaliko wa kumsifu Yehova. (Zab. 148:12-14) Pia mazoezi ambayo wazazi wanatoa kila siku kwa watoto wao yangepaswa, kati ya mambo mengine, kuwatayarisha kueleza imani yao kwa wengine katika mahubiri.—Kumb. 6:6, 7.

2 Tuwazoeze Watoto Wetu Hatua kwa Hatua: Watoto wanastahili kupewa mazoezi tangu utoto wao ili kuwashindikiza wazazi wao katika huduma. Kabla ya kushiriki katika utumishi, tutayarishe watoto wetu kuushiriki kwa bidii. Tuanze kwa kuwaambia waziwazi yale tunayotaka kwao mlango kwa mlango. Watoto wenye umri mdogo sana wanaweza kutoa trakti au karatasi za mwaliko na kuomba watu waje kwenye Jumba la Ufalme. Inawezekana kuomba kwa watoto wadogo wanaosoma vizuri kufanya usomaji wa Maandiko. Wanaweza kutolea magazeti kwa kuyaonyesha tu. Kwa kadiri wanavyojipatia ujuzi, tuwafundishe kutumia Biblia katika utoaji wao mbalimbali. Vijana wengi wahubiri wanaacha kikawaida magazeti kwa watu na wanafanya ziara za kurudia. Ni vizuri kwamba mtoto afuatane na mtu mzima badala ya kijana mwingine Mkristo. Mtu mzima anaweza kumfasiria msikilizaji kwamba mtoto yuko katika mazoezi kwa ajili ya huduma.

3 Binti mmoja mdogo aliomba wazee msaada ili kutimiza matakwa yanayoombwa ya mhubiri wa Ufalme. Alikuwa tu na miaka mitano wakati huo na alikuwa asiyejua kusoma, lakini alikuwa hata hivyo na uwezo wa kutoa kwa matokeo ujumbe wa Ufalme kwenye milango. Alirudilia-rudilia akilini mistari ya Maandiko, alikuwa akifungua Biblia pa nafasi hizo, alikuwa akimuomba msikilizaji kusoma na alikuwa akitoa mafasirio.

4 Kwa kielelezo chao, wazazi wangepaswa kufundisha watoto wao umaana wa kupanga mambo yao vizuri ili kushiriki kikawaida katika huduma. Ni jambo la muhimu kwamba wapange programu nzuri kila siku kwa ajili ya utumishi na kwamba waiheshimu, ili kwamba watoto wajue ni nyakati gani za juma ambazo zinalindwa tu kwa ajili ya mahubiri.

5 Ikiwa watoto wanajifunza tangu umri wao mdogo zaidi kupenda huduma na kuishiriki, watachochewa kufanya maendeleo ili kupata, katika wakati ujao, mapendeleo makubwa zaidi na, labda, kuanzisha utumishi wa painia. (1 Kor. 15:58) Tungepaswa sote kuwatia moyo watoto tunaoshirikiana nao kufanya maendeleo mazuri kwa sifa ya Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine