Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/02 uku. 2
  • Kisanduku Cha Maulizo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kisanduku Cha Maulizo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Majibu Kwa Maulizo Yenu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Kisanduku Cha Maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Juu ya Nini Tunapaswa Kufikiria Namna Yetu ya Kuvala na Kujipamba?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Matendo ya Muzuri Yenye Haiwezi Kusahauliwa
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2019
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 6/02 uku. 2

Kisanduku Cha Maulizo

◼ Ni kiwango gani tunachopaswa kufuata kuhusu mavazi na kujipamba tunapotembelea makao ya Betheli na majengo ya ofisi za tawi?

Tunapotembelea Betheli, iwe kwamba ni kwa kusudi la kuona jinsi jengo hilo lilivyo au kuongea na washiriki wa familia ya Betheli, “mavazi yetu, kujipamba kwetu na mwenendo wetu umepasa uwe namna ileile tunayotazamiwa kuwa tunapohudhuria mikutano ya ibada kwenye Jumba la Ufalme.” (om-SW 131) Hata hivyo, imeonekana kwamba wanapotembelea ofisi za tawi, ndugu na dada fulani wanaelekea kupita kiasi kwa kuvaa kwa namna isiyojali. Hilo si jambo lenye kufaa tunapotembelea majengo hayo. Sura yetu inapaswa kuwa yenye kutengenezwa vizuri na yenye kiasi, ikionyesha adabu na heshima inayostahili watumishi wa Yehova Mungu.​—1 Tim. 2:​9, 10.

Hilo ni jambo la maana hasa tunapotembelea makao ya Betheli na majengo ya ofisi za tawi, kwa sababu yanavuta uangalifu wa watazamaji wengi wasio Mashahidi. Huenda watazamaji hao wakawa na maoni mbalimbali kuhusu watu wa Mungu na tengenezo lake kwa msingi wa yale wanayoona. Ni jambo lenye kufaa kuzungumza na wanafunzi wa Biblia na wengine wanaoweza kutembelea makao hayo ili kuwakumbusha umaana wa kuwa waangalifu kuhusu mavazi na kujipamba kunakofaa. Familia ya Betheli itashukuru mkifanya hivyo.

Tukiwa wahudumu Wakristo, tunapaswa kuwa waangalifu ili sura yetu isitoe sababu yoyote ya kukwaza. (2 Kor. 6:​3, 4) Badala ya hivyo, kupitia utaratibu wetu wenye kufaa, acheni sikuzote ‘turembe fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote’.​—Tito 2:​10.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine