Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/02 uku. 3
  • Kwa Nini Tupende Ushirika Wetu Mzima wa Ndugu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kwa Nini Tupende Ushirika Wetu Mzima wa Ndugu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Tupende Ushirika Muzima wa Akina Ndugu’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2013
  • Familia ya Ndugu na Dada Yenye Umoja
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Video: Mashahidi wa Yehova—Tengenezo Linalohubiri Habari Njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Habari Njema Iko Nahubiriwa Namna Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 6/02 uku. 3

Kwa Nini Tupende Ushirika Wetu Mzima wa Ndugu

Katika ulimwengu wa leo usio na upendo, tunawezaje kuendelea kuonyesha upendo mwingi sana kwa ndugu zetu? (1 Pet. 2:​17) Tunawezaje kuonyesha wengine kwamba undugu wetu wa kweli na wa ulimwenguni pote upo kweli? (Mt. 23:8) Kwa kutumia vidio Toute la communauté de nos frères (Ushirika Wetu Mzima wa Ndungu). Inaonyesha kwa nini sisi tunapendana. Angalia ikiwa unaweza kujibu maulizo haya:

(1) Ni utendaji gani tatu tunaoshiriki pamoja na ndugu zetu ulimwenguni pote? (2) Ndugu zetu wanaonyeshaje azimio lao la kuhubiri (a) katika jangwa la Alaska, (b) katika bandari kubwa za Ulaya, na (c) katika misitu mikubwa ya Peru? (3) Ni nini chombo chenye matokeo ya pekee katika kutoa ushahidi? (4) Kwa nini hatupaswi kamwe kufikiri kwamba kuhubiri ni kazi ya kawaida tu? (5) Toa mifano ya jinsi ambavyo Mashahidi wa Yehova wamefarijiana na kutegemezana wakati wa taabu​—matetemeko ya dunia, upepo mkali, na vita vya wananchi wenyewe kwa wenyewe. (Ona maelezo ya Takao kwenye ukurasa wa 23 katika Amkeni! ya Agosti 22, 1995, na ya Kotoyo kwenye ukurasa wa 20 katika Amkeni! ya Oktoba 22, 1996) (6) Ni katika njia gani zenye kutenda sisi sote tunaweza kuonyesha ile alama kubwa yenye kutambulisha undugu wetu wa Kikristo? (Yn. 13:​35) (7) Ni kwa kiasi gani tunapaswa kuonyesha kwamba tunathamini mikutano yetu ya kutaniko? (8) Namna gani kuwa na Jumba la Ufalme kwa ajili ya mikutano kuna uvutano juu ya wale ambao hawakuwa nalo hapo mbele? (9) Ndugu zetu katika Ulaya ya Mashariki na Urusi waliokokaje kiroho walipopigwa marufuku? (10) Hata sasa, ni jitihada gani isiyo ya kawaida wanayofanya Mashahidi wengi ili kuhudhuria makusanyiko, na kwa nini? Jambo hilo limegusaje moyo wako? (11) Kwa nini mnaazimia kuabudu pamoja katika umoja, kuwasaidia wengine wakati wa uhitaji, na kuhubiri kwa uaminifu wakati wowote na kwa namna yoyote mwezavyo? (12) Kwa nini ni vema kuwa na nakala yako binafsi ya vidio hii na kuionyesha watu wanaopendezwa wengi zaidi iwezekanavyo?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine