Video: Mashahidi wa Yehova—Tengenezo Linalohubiri Habari Njema
Mashahidi wa Yehova wamekuwa wakihubiri habari njema kwa zaidi ya miaka 100. Katika kampanye hii ya kuhubiri iliyo kubwa zaidi ambayo haijawahi kufanyika ulimwenguni, tunahubiri katika luga nyingi na pia katika inchi zaidi ya 230. (Mt. 24:14) Lakini, kwa nini kazi hii ni ya maana? Na namna gani inatimizwa ulimwenguni pote? Video Mashahidi wa Yehova—Tengenezo Linalohubiri Habari Njema (Les Témoins de Jéhovah : organisés pour proclamer la bonne nouvelle) inajibu maulizo hayo kwa kufasiria kwa kirefu sehemu mbalimbali za kazi tunayofanya ulimwenguni pote. Kisha kutazama video hiyo, fikiria maulizo haya:
Namna gani video hii imekusaidia upendezwe sana na (1) namna tengenezo la Yehova linavyojikaza ili kufanya habari njema ihubiriwe? (2 Tim. 4:2) (2) kazi inayofanywa na familia za Betheli ulimwenguni pote? (3) mazoezi ambayo waangalizi na wamisionari wanapewa? (2 Tim. 2:2) (4) faida ya kuanza siku kwa kuchunguza andiko la Biblia na kujitayarisha kila juma kwa ajili ya mikutano? (Mdo. 17:11) (5) faida za kuhuzuria mikutano yetu ya Kikristo? (Ebr. 10:24, 25) (6) baraka utakazopokea wakati Paradiso itarudishwa duniani? (Isa. 11:9) (7) pendeleo ulilo nalo la kushiriki katika kazi ya mavuno inayoendelea?—Yoh. 4:35.
Video imeonekana kuwa kifaa kizuri sana ili kusaidia watu wanaopendezwa wajuwe vizuri kazi inayofanywa na Mashahidi wa Yehova ulimwenguni pote. (8) Ni wakati gani itakuwa vizuri kuonyesha video hii kwa watu tunaojifunza nao Biblia, watu wa jamaa, na wengine? (9) Je, watu wanafurahi wanapoitazama video hii?
Tunapofikiri sana juu ya mambo ambayo Yehova anatimiza, tunachochewa kusema kama mtunga-zaburi: “Wewe mwenyewe umefanya mambo mengi, Ee Yehova Mungu wangu, naam, kazi zako za ajabu na mawazo yako kutuelekea; hakuna wa kulinganishwa nawe.” (Zab. 40:5) Na tutumie vizuri video hii ili kusaidia wengine wapendezwe na Yehova na tengenezo lake!