Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/02 uku. 1
  • Saidia Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Lako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Saidia Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Lako
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Waangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Wanavyoonyesha Kupendezwa Kibinafsi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Funzo la Kitabu la Kutaniko—Kwa Nini Tunalihitaji
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Namna ya Kufaidika na Kikundi Chenu cha Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Waangalizi wa Kuchunga Kundi
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 11/02 uku. 1

Saidia Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko Lako

1 Kila mmoja wetu anapata faida nyingi zinazotokana na Funzo la Kitabu la Kutaniko. Mwezi uliopita tulizungumzia jinsi Mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko anavyotimiza fungu lake. Lakini ni jambo gani tunaloweza kufanya ili kumsaidia na hivyo kufaidika sisi wenyewe na pia wengine?

2 Hudhuria Kila Juma: Kwa kuwa vikundi vya funzo la kitabu vinafanywa kuwa vidogo, kuwapo kwako ni jambo la lazima. Fanya iwe mradi wako kuhudhuria kila juma. Unaweza pia kusaidia kwa kufika pa wakati, kwani hilo linasaidia mwangalizi kuanza mkutano katika hali yenye utaratibu.—1 Kor. 14:40.

3 Maelezo Yenye Kujenga: Njia nyingine katika hiyo unaweza kusaidia ni kwa kujitayarisha vizuri na kutoa majibu yenye kujenga. Maelezo yanayokazia jambo moja kwa kawaida ndiyo maelezo bora, na hilo linatia moyo wengine kutoa maelezo. Epuka kujaribu kutoa maelezo kuhusu kila jambo katika fungu. Ikiwa jambo moja katika habari linagusa moyo wako, tajirisha mazungumzo kwa kushiriki wazo lako na wengine katika maelezo yako.—1 Pet. 4:10.

4 Ikiwa una pendeleo la kusoma mafungu kwa faida ya kikundi, uwe mwenye juhudi katika kutimiza mgawo huo. Usomaji mzuri unachangia kufanya funzo liwe la hali ya juu na lenye kupendeza.—1 Tim. 4:13.

5 Kutoa Ushahidi Katika Kikundi: Mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani inafanywa katika mahali pengi pa funzo la kitabu, na msaada wako kwa mipango hiyo utasaidia mwangalizi anapochukua uongozi katika kazi ya kueneza evanjeli. Ona mipango hiyo kuwa nafasi ya kukaribia ndugu na kuwatia moyo.

6 Ripoti za Utumishi wa Shambani: Kutoa ripoti yako ya utumishi wa shambani bila kukawia mwisho wa kila mwezi ni njia nyingine ya kusaidia mwangalizi. Unaweza kumpatia ripoti yako moja kwa moja au kuiweka katika kisanduku kilichotayarishwa kwa ajili ya ripoti kwenye Jumba la Ufalme. Mwandishi anaweza kutumia kisanduku ili kukusanya ripoti za utumishi zilizokusanywa na waangalizi wa funzo la kitabu.

7 Ushirikiano wako na mwangalizi wako wa Funzo la Kitabu la Kutaniko utathaminiwa. Zaidi ya yote, unaweza kuwa hakika kwamba Yehova atakuwa ‘pamoja na roho ambayo waonyesha.’—Flp. 4:23.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine