Kisanduku Cha Maulizo
◼ Ni wakati gani inapofaa kuunda kikundi cha lugha ya kigeni?
Eneo la kutaniko linapotia ndani kiasi cha kutosha cha watu wenye kusema lugha ya kigeni, wazee wanapaswa kufanya yale wawezayo ili kupanga kazi ya kuhubiri katika lugha hiyo. (km-ZS 7/02 uku. 1; km-SW 3/98 uku. 3-4) Huenda ikawa kwamba watu wanaosema lugha ya kigeni wanatawanyika sana katika maeneo yote ya makutaniko jirani mawili au zaidi. Katika hali hiyo, waangalizi wa mzunguko watatoa uongozi unaohitajiwa, wakisaidia hivyo makutaniko yanayohusika yashirikiane katika kazi ya kuhubiri. Pindi kwa pindi, hotuba ya watu wote au Funzo la Mnara wa Mlinzi linaweza kupangwa ili kuona ni watu wangapi watakaohudhuria mikutano katika lugha ya kigeni.
Kikundi cha lugha ya kigeni kinaweza kuundwa ikiwa matakwa yafuatayo yanatimizwa: (1) Kuna wahubiri au watu wanaopendezwa ambao wanasikia vizuri zaidi habari njema katika lugha ya kigeni. (2) Kuna mzee mmoja au mtumishi wa huduma mwenye kustahili atakayechukua uongozi na kuendesha hata mkutano moja wa kila juma. (3) Baraza moja la wazee lina nia ya kusaidia kikundi hicho. Matakwa hayo yanapotimizwa, wazee wanapaswa kujulisha ofisi ya tawi ili kikundi kiweze kujulikana rasmi, na ili maagizo zaidi yatolewe.
Vikundi vilivyo vingi huanza kwa kufanya Funzo la Kitabu la Kutaniko kila juma. Baadaye, huenda wazee wakakubali kuongeza mikutano mingine, kama vile Mkutano wa Watu Wote na Funzo la Mnara wa Mlinzi. Migawo Na. 2, 3, na 4 ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi inaweza kutolewa katika darasa lenye kutenganishwa ikiwa mzee au mtumishi wa huduma mwenye kustahili na anayesema lugha hiyo anaweza kutumikia kuwa mshauri. Lakini, kikundi kitaungana na kutaniko kwa ajili ya hotuba ya maagizo, mambo makuu kutoka usomaji wa Biblia, na Mkutano wa Utumishi. Mikutano kwa ajili ya utumishi wa shambani inaweza pia kupangwa kwa ajili ya kikundi.
Wote katika kikundi wanatumika kwa ukaribu chini ya usimamizi wa baraza la wazee. Wazee wanapaswa kutoa uongozi wenye kusawazika na kuonyesha kwamba wanapendezwa na kikundi kwa kuhangaikia mahitaji yacho. Wakati mwangalizi wa mzunguko anapotembelea kutaniko linalotoa msaada, atapanga pia kufanya kazi na kikundi katika utumishi wa shambani ili kukijenga kiroho. Kwa baraka ya Yehova, kikundi cha lugha ya kigeni kinaweza kuwa kutaniko kwa wakati wake.