Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/03 uku. 8
  • ‘Tumikieni Yehova kwa Furaha’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Tumikieni Yehova kwa Furaha’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Ongeza Furaha Yako katika Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Shangwe—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 10/03 uku. 8

‘Tumikieni Yehova kwa Furaha’

1 Mtume Paulo alisema hivi: “Sikuzote shangilieni katika Bwana. Mara moja tena hakika nitasema, Shangilieni!” (Flp. 4:4) Pendeleo la kushiriki habari njema na kusaidia watu wenye mfano wa kondoo ili wamwabudu Yehova ni chanzo cha furaha kubwa. (Luka 10:17; Mdo. 15:3; 1 The. 2:19) Hata hivyo, tukiona kwamba wakati mwingine furaha inakosekana katika huduma yetu, tunaweza kufanya nini?

2 Kazi Iliyoamuriwa na Mungu: Kumbuka kwamba utume wetu wa kuhubiri unatoka kwa Yehova. Ndiyo, sisi ni wenye kupendelewa kama nini kuwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu” katika kutangaza ujumbe wa Ufalme na kufanya wanafunzi! (1 Kor. 3:9) Kristo Yesu yuko pamoja nasi katika kazi hiyo ambayo haitarudiliwa kamwe. (Mt. 28:18-20) Malaika pia wanahusika sana na wanatumika pamoja nasi katika mavuno makubwa ya kiroho yanayofanywa wakati huu. (Mdo. 8:26; Ufu. 14:6) Maandiko, pamoja na mambo waliyojionea watu wa Mungu, yanatoa uhakikisho ulio wazi kwamba Yehova anategemeza kazi hii. Kwa hiyo, tunapohubiri, tunaenda “tukiwa waliotumwa kutoka kwa Mungu, mbele ya Mungu, kwa ushirika na Kristo.” (2 Kor. 2:17) Hiyo ni sababu yenye nguvu kama nini ya kuwa na furaha!

3 Sala ni ya maana sana ili kudumisha furaha yetu katika utumishi wa Mungu. (Gal. 5:22) Kwa kuwa hatuwezi kufanya kazi ya Mungu bila kupewa nguvu kutoka kwake, tunapaswa kuomba roho yake, anayoitoa kwa ukarimu kwa wale wanaomwomba. (Luka 11:13; 2 Kor. 4:1, 7; Efe. 6:18-20) Kusali kuhusu huduma yetu kutatusaidia tudumishe maoni yanayofaa tunapokutana na watu wanaoitikia isivyofaa. Kutatuwezesha tuendelee kuhubiri kwa ujasiri na kwa furaha.—Mdo. 4:29-31; 5:40-42; 13:50-52.

4 Jitayarishe Vizuri: Njia moja inayofaa ya kuongeza furaha yetu tunaposhiriki katika huduma ni kujitayarisha vizuri. (1 Pet. 3:15) Kujitayarisha huko hakupaswi kuchukua wakati mwingi. Inaomba dakika chache tu ili kurudilia utoaji mbalimbali uliopendekezwa kuhusu magazeti ya sasa au utoaji unaofaa kichapo unachopanga kutolea watu. Ili kupata utangulizi unaofaa, unaweza kuchunguza kitabu Kutoa Sababu au matoleo ya zamani ya Huduma Yetu ya Ufalme. Wahubiri fulani wa Ufalme wanaona kuandika utoaji mfupi kwenye karatasi ndogo kuwa jambo lenye kuwasaidia. Pindi kwa pindi, wanatupia jicho kwenye karatasi hiyo ili kuchemsha akili yao. Hilo linawasaidia kushinda wasiwasi na linawapa uhakika ili wahubiri kwa ujasiri.

5 Furaha inaleta faida nyingi. Mtazamo wenye furaha unafanya ujumbe wetu uwe wenye kuvutia zaidi. Furaha inatutia nguvu ili tuvumilie. (Neh. 8:10; Ebr. 12:2) Zaidi ya yote, utumishi wetu wenye furaha unamtukuza Yehova. Kwa hiyo, ‘tutumikie Yehova kwa furaha.’—Zab. 100:2.

[Study Questions]

1. Ni nini kinachoweza kuwa chanzo cha furaha kubwa kwa watumishi wa Yehova?

2. Kukumbuka chanzo cha utume wetu kunachangiaje furaha yetu?

3. Sala inasaidiaje kudumisha furaha yetu katika utumishi wa Mungu?

4. Kujitayarisha vizuri kunatusaidiaje kuongeza furaha yetu katika mahubiri, na ni nini njia fulani zenye kufaa ambazo katika hizo tunaweza kujitayarisha?

5. Furaha inatuletea sisi na wengine faida gani?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine