Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/02 uku. 8
  • Ongeza Furaha Yako katika Mahubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ongeza Furaha Yako katika Mahubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Tumikieni Yehova kwa Furaha’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Shangwe—Sifa Yenye Tunapata Kutoka kwa Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
  • Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 3/02 uku. 8

Ongeza Furaha Yako katika Mahubiri

1 Furaha ya kushiriki habari njema​—je, unaipata katika huduma yako? Ikiwa sisi si waangalifu, ulimwengu mwovu unaotuzunguka unaweza kutufanya tukose ujasiri wa kuhubiri, jambo litakalotufanya tupoteze furaha yetu. Kutumika katika eneo ambamo watu hawaitikii kunaweza pia kutuvunja moyo. Ni hatua gani zenye kufaa ambazo tunaweza kuchukua ili kuongeza furaha yetu katika mahubiri?

2 Uwe Mwenye Kutazamia Mema: Kuendeleza mtazamo wenye kufaa kunasaidia kwelikweli. Njia moja ya kufanya hivyo ni kwa kutafakari juu ya pendeleo la pekee tulilo nalo la kuwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu.” (1 Kor. 3:9) Yesu pia yuko pamoja nasi katika kutimiza kazi hii. (Mt. 28:​20) Na anatumia jeshi la malaika ili kututegemeza. (Mt. 13:​41, 49) Hivyo, tunaweza kuwa hakika kwamba jitihada zetu zinaongozwa na Mungu. (Ufu. 14:​6, 7) Kwa hiyo, ijapokuwa jinsi watu fulani wanavyoweza kuitikia kazi yetu, itikio la kimbingu ni la furaha kubwa!

3 Jitayarishe Vizuri: Matayarisho mazuri pia huongeza furaha yetu. Kujitayarisha kwa ajili ya huduma hakuhitaji kazi nyingi. Inachukua tu dakika chache ili kuchunguza jambo la kuzungumzia kutoka katika magazeti ya sasa au toleo la vichapo la mwezi. Chagua utoaji mmoja kutoka makala “Tuseme Nini Kuhusu Magazeti,” katika Huduma Yetu ya Ufalme. Chunguza nyongeza ya Januari 2002, “Utoaji Uliopendekezwa kwa Ajili ya Utumishi wa Shambani,” au tafuta utangulizi wenye matokeo katika kitabu Kutoa Sababu. Ikiwa unazuiwa na kipingamizi ambacho wenye nyumba hutokeza kwa kawaida, tayarisha jibu kulingana na maneno yao na kuongoza uangalifu kwenye habari inayoamsha kupendezwa. Kitabu Kutoa Sababu ni chenye kusaidia sana katika kufanya hivyo. Kutumia misaada hiyo kutatupatia uhakika tunaouhitaji ili kuhubiri kwa furaha.

4 Sali kwa Bidii: Sala ni ya maana sana ili kuwa na furaha yenye kudumu. Kwa kuwa tunafanya kazi ya Yehova, tunahitaji kumwomba sana roho yake, ambayo tunda lake moja ni shangwe. (Gal. 5:​22) Yehova atatupatia nguvu ili kuendelea kuhubiri. (Flp. 4:​13) Kusali kuhusu huduma yetu kunaweza kutusaidia tuendelee kuwa na maoni yenye kufaa wakati tunapopatwa na mambo yasiyofaa. (Mdo. 13:​52; 1 Pet. 4:​13, 14) Ikiwa tunajisikia wenye kuogopeshwa, sala inaweza kutusaidia tuendelee kwa ujasiri na kwa furaha.​—Mdo. 4:​31.

5 Tokeza Nafasi za Kutoa Ushahidi: Bila shaka, huduma yetu ni yenye furaha zaidi wakati tunapoweza kupata watu na kuwatolea ushahidi. Kubadili programu yako ili kutembelea watu nyumba kwa nyumba pa saa tofauti-tofauti, labda jioni, kunaweza kutokeza mafanikio zaidi. Unakutana na watu kila wakati unapotembea barabarani, unapofanya ununuzi dukani, unaposafiri katika basi, au unapotembea katika bustani. Sababu gani usitayarishe utangulizi mfupi wa kuanzisha mazungumzo na kuchukua hatua ya kukaribia wale ambao wanaonekana kuwa wenye urafiki? Au labda unafanya kazi ya kimwili au kwenda kwenye shule ya watu wote, ambako unazungumza na watu wengine kila siku. Huenda ukapata nafasi ya kutoa ushahidi kwa kutokeza tu habari ya Kimaandiko inayoamsha kupendezwa fulani. Mapendekezo mazuri yanapatikana kwenye ukurasa wa kwanza wa nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002. Zozote za jitihada hizo zinaweza kufanya mengi ili kuongeza furaha ya mtu katika mahubiri.

6 Kwa kuwa furaha hutusaidia kuvumilia, ni jambo la maana sana kama nini kuiendeleza! Kwa kufanya hivyo, tutavuna thawabu kubwa wakati kazi hii ambayo haitarudiliwa kamwe itafikia umalizio wake. Tazamio hilo lenyewe linaweza kuongeza furaha yetu katika mahubiri.​—Mt. 25:21.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine