Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 15/2 uku. 15-18
  • Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • UWASAIDIE WAHUBIRI WAPYA
  • UZUNGUMUZE NA MUHUBIRI MWENZAKO
  • UENDELEE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU KWA UKAWAIDA
  • UKUWE TAYARI KUTUMIKISHA MAPENDEKEZO
  • UJIWEKEE MIRADI YENYE UNAWEZA KUFIKIA
  • Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Jinsi ya Kuwazoeza Wapya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Endelea Kuwa na Mawazo ya Muzuri juu ya Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Umuige Yesu, Ukuwe na Bidii kwa Ajili ya Mahubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 15/2 uku. 15-18
Muhubiri anakutana na hali hizi katika mahubiri: 1. Hakuna mutu nyumbani; 2. Mwenye nyumba hapendezwe; 3. Mwenye nyumba ni mukali

Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri

KUHUBIRI habari njema ndio kazi ya maana zaidi yenye kufanyika hapa duniani leo. Kwa sababu wewe ni mutumishi wa Yehova, bila shaka unaona kwamba ni pendeleo kubwa kufanya wanafunzi. Hata hivyo, kuna wakati mapainia na wahubiri wengine wanapambana na hali ngumu zenye zinawafanya wasiendelee kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri.

Muhubiri wa Ufalme anagonga kwenye mulango; anafanya hivyo kwa furaha

Ni nini inaweza kukusaidia uendelee kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri?

Ni vigumu kwa wahubiri fulani kupata watu wa kuzungumuza nao katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba. Kwa mufano, watu wa eneo wanaweza kukosa kuwa nyumbani. Hata wakati wanakuta watu katika eneo, watu hao wanaweza kukosa kupendezwa ao wanaweza kuwa wakali. Wahubiri wengine wanahubiri katika eneo kubwa na lenye kuzaa matunda, na wanaogopa kwamba hawataweza kuhubiria kila mutu wa eneo. Wengine katika kutaniko wamehubiri kwa miaka mingi, kisha wamevunjika moyo kwa sababu wameona kwamba mwisho haufike mbio.

Watumishi wote wa Yehova wanapambana na magumu yenye inaweza kufanya wapunguze bidii yao katika kazi ya kuhubiri, na hilo haliwezi kutushangaza. Hatuwezi kutazamia kwamba itakuwa mwepesi kuhubiri habari njema katika ulimwengu huu wenye kutawaliwa na “yule mwovu,” Shetani Ibilisi.​—1 Yoh. 5:19.

Hata kama unapambana na magumu ya namna gani katika kazi ya kutangaza habari njema, ukuwe hakika kwamba Yehova atakusaidia kuyavumilia. Lakini, unaweza kufanya nini ili kuongeza bidii yako katika kazi ya kuhubiri? Acha tuone mapendekezo fulani.

UWASAIDIE WAHUBIRI WAPYA

Muhubiri wa Ufalme mwenye anamuzoeza muhubiri mupya katika mahubiri

Kila mwaka, maelfu ya watu wanabatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova. Ikiwa umebatizwa hivi karibuni, bila shaka unaweza kufaidika na uzoefu wa wale wenye wamefanya kazi ya kuhubiri kwa miaka mingi. Ao ikiwa wewe ni muhubiri wa Ufalme tangu miaka mingi, hauone kwamba ni jambo lenye kufaa na lenye kufurahisha kuwazoeza wahubiri wapya?

Yesu alijua kwamba wanafunzi wake walikuwa na lazima ya muongozo ili wapate matokeo mazuri katika kazi ya kutangaza habari njema, na alionyesha namna kazi hiyo inapaswa kufanyika. (Lu. 8:1) Leo pia, wahubiri wako na lazima ya kuzoezwa ili wapate matokeo mazuri katika kazi ya kuhubiri.

Hatupaswe kufikiri kwamba muhubiri mupya atakuwa na ufundi wa kufundisha kwa sababu tu anaenda katika mahubiri. Iko na lazima ya kuzoezwa na muhubiri mwengine mwenye upendo. Muhubiri huyo mwenye upendo atamuonyesha namna ya (1) kujitayarisha na kufanya mazoezi mbele ya kuenda katika mahubiri, (2) kuzungumuza na mutu kwenye nyumba ao katika njia, (3) kutolea watu vichapo, (4) kurudilia watu wenye kupendezwa, na (5) kuanzisha funzo la Biblia. Kwa kweli, matokeo itakuwa muzuri ikiwa ule muhubiri mupya anafuata na kuiga ufundi wa muhubiri mwenye kumuzoeza. (Lu. 6:40) Bila shaka, muhubiri mupya atafurahia kuwa na mutu mwenye anaweza kumusikiliza na kumusaidia, wakati iko na lazima ya musaada. Tena, muhubiri mupya atafaidika sana ikiwa anapongezwa na kupewa mapendekezo mazuri.​—Mhu. 4:9, 10.

UZUNGUMUZE NA MUHUBIRI MWENZAKO

Muhubiri wa Ufalme anafanya funzo la pekee

Hata kama unajikaza kuanzisha mazungumuzo na watu wa eneo, unaweza kuwa na mazungumuzo mazuri zaidi pamoja na ndugu ao dada mwenye unahubiri pamoja naye. Kumbuka kwamba Yesu alituma wanafunzi “wawili-wawili” katika mahubiri. (Lu. 10:1) Wakati walihubiri pamoja, walikuwa na nafasi ya kuchocheana na kutiana moyo. Leo pia, Wakristo wanapata nafasi ya kuwa na “ubadilishanaji wa kitia-moyo” wakati wanahubiri pamoja.​—Rom. 1:12.

Munaweza kuzungumuzia mambo gani? Kuna jambo fulani mumoja kati yenu alikutana nalo hivi karibuni lenye linaweza kutia moyo? Umejifunza jambo fulani lenye kufurahisha wakati wa ibada ya familia ao wakati wa funzo lako la pekee? Kuna jambo fulani ulisikia kwenye mikutano lenye lilikutia moyo? Wakati fulani, haitawezekana uhubiri kila mara na muhubiri uleule. Unajua namna alifikia kuwa Shahidi wa Yehova? Ni nini ilimuhakikishia kwamba tuko kabisa katika tengenezo la Yehova? Ni mapendeleo gani amepata, na amekutana na mambo gani? Pengine utamuelezea mambo yenye ulikutana nayo. Wakati Wakristo wawili wanahubiri pamoja, wanakuwa na nafasi nzuri za ‘kuendelea . . . kujengana,’ hata kama katika mahubiri wanakutana na hali gani.​—1 Tes. 5:11.

UENDELEE KUJIFUNZA NENO LA MUNGU KWA UKAWAIDA

Wahubiri wawili wa Ufalme wanafanya onyesho kwa ajili ya mahubiri

Ili uendelee kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri, ni lazima uendelee kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida. ‘Mutumwa mwaminifu na mwenye busara’ anachapisha habari mbalimbali katika vichapo vyetu. (Mt. 24:45) Kwa hiyo, unaweza kujifunza mambo mbalimbali ili upate chakula cha kiroho. Tuchukue kwa mufano habari moja yenye unaweza kuchunguza katika funzo lako la pekee: Sababu gani kazi ya kuhubiri Ufalme ni ya maana sana? Kisanduku chenye kupatikana kwenye ukurasa wa 16, kinatoa sababu fulani.

Ukichunguza sababu zenye kupatikana katika kisanduku hicho, utachochewa kuendelea kuhubiri kwa bidii. Katika funzo lako la pekee, unaweza kuchukua mupango wa kutafuta sababu zingine zenye zinaweza kukuchochea uendelee kuhubiri kwa bidii. Kisha, ufikiri sana juu ya sababu hizo, na juu ya maandiko yenye kuzitegemeza. Ukifanya hivyo, bila shaka bidii yako katika kazi ya kuhubiri itaongezeka.

UKUWE TAYARI KUTUMIKISHA MAPENDEKEZO

Wahubiri wawili wa Ufalme wanafanya onyesho kwa ajili ya mahubiri

Tengenezo la Yehova linatutolea kwa ukawaida mapendekezo yenye inatusaidia ili tuhubiri muzuri zaidi. Kwa kawaida tunahubiri nyumba kwa nyumba. Lakini tunatiwa pia moyo kuhubiri kupitia barua, kupitia telefone, kuhubiri mahali pa watu wengi kama vile kwenye barabara, kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo, ao kuhubiria watu katika maeneo ya biashara. Tunaweza pia kuchukua mipango ili kutoa ushahidi katika eneo lenye halihubiriwe kwa ukawaida.

Uko tayari kutumikisha mapendekezo hayo? Umekwisha kutumikisha mapendekezo fulani? Wakristo wengi wenye walifanya hivyo wamepata matokeo mazuri na hilo limewaletea furaha nyingi. Tuone mifano tatu.

Mufano wa kwanza unaonyesha matokeo yenye dada mumoja mwenye kuitwa April alipata wakati alitumia mapendekezo yenye ilitolewa katika Huduma Yetu ya Ufalme kuhusu namna ya kuanzisha mafunzo ya Biblia. Mapendekezo hayo ilimuchochea kuanzisha mafunzo ya Biblia pamoja na wanawake watatu wenye alikuwa anatumika nao. Alishangaa sana na kufurahi wakati wote watatu walikubali kujifunza na walianza kukusanyika.

Mufano wa pili ni juu ya kutolea watu magazeti. Tumetiwa moyo kutafuta watu wenye wanaweza kupendezwa na habari fulani zenye kupatikana katika magazeti yetu. Katika États-Unis, mwangalizi mumoja wa muzunguko alisema kwamba alihubiria watu wenye kusimamia maduka ya kuuzisha magurudumu (pneus) ya motokari, na akawatolea gazeti Amuka! lenye lilikuwa na habari juu ya magurudumu. Pia, yeye na bibi yake walitolea waganga gazeti Amuka! lenye kichwa “Kuwaelewa Madaktari” kwenye biro zaidi ya 100. Anasema hivi: “Kuenda kuona watu hao kumetuwezesha kujitambulisha na kuwatolea vichapo. Kisha kuanzisha urafiki pamoja na watu kwenye nafasi hizo, tumekuwa na nafasi nyingi za kuendelea kuwatembelea.”

Mufano wa tatu ni juu ya kutoa ushahidi kupitia telefone. Dada mumoja mwenye kuitwa Judy alituma barua kwenye makao yetu makubwa ili kuonyesha shukrani yake kuhusu pendekezo la kuhubiria watu kupitia telefone. Alisema kwamba mama yake mwenye kuwa na miaka 86 iko na matatizo mengi ya afya, lakini anahubiri kwa ukawaida kupitia telefone, na anaongoza funzo la Biblia pamoja na mwanamuke fulani mwenye kuwa na miaka 92.

Bila shaka, mapendekezo yenye kupatikana katika vichapo vyetu inakuwa na matokeo mazuri katika mahubiri. Tumia mapendekezo hayo! Inaweza kukusaidia uendelee kuwa na furaha na bidii katika kazi ya kuhubiri.

UJIWEKEE MIRADI YENYE UNAWEZA KUFIKIA

Kupata matokeo mazuri katika kazi ya kuhubiri haimaanishe tu kutolea watu vichapo vingi, kuongoza mafunzo mengi, ao kusaidia watu wengi wakuwe Mashahidi wa Yehova. Sasa tujiulize, kutosha watu wa familia yake, ni watu ngapi wengine Noa alisaidia wakuwe watumishi wa Yehova? Lakini, alikuwa muhubiri mwenye matokeo. Jambo la lazima ni kumutumikia Yehova kwa uaminifu.​—1 Kor. 4:2.

Wahubiri wengi wa Ufalme wanaona kwamba ili waendelee kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri, ni lazima wajiwekee miradi yenye wanaweza kufikia. Wanaweza kujiwekea miradi gani? Kisanduku chenye kupatikana kwenye ukurasa huu kinaonyesha miradi fulani.

Utafute njia za kufanya kazi yako ya kuhuburi ikuletee furaha zaidi na ikue na matokeo mazuri zaidi; Yehova atakusaidia ili uweze kufanya hivyo. Wakati unafikia miradi yako utakuwa na furaha kwa sababu umetimiza jambo la maana, na utakuwa mwenye kutosheka kwa sababu unajua kwamba unafanya yote yenye unaweza ili kuhubiri habari njema.

Kwa kweli, inaweza kuwa vigumu kuhubiri habari njema. Lakini, kuna mambo yenye unaweza kufanya ili uendelee kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri Ufalme. Ukuwe na mazungumuzo yenye kutia moyo pamoja na yule mwenye unahubiri naye, uendelee kujifunza Neno la Mungu kwa ukawaida, utumikishe mapendekezo yenye kutolewa na mutumwa mwaminifu, na ujiwekee miradi yenye unaweza kufikia. Zaidi ya yote, usisahau kwamba Mungu amekupatia pendeleo kubwa la kuwa Shahidi wake na kutangaza habari njema. (Isa. 43:10) Bila shaka, utapata furaha nyingi kwa kuendelea kuwa na bidii katika kazi ya kuhubiri!

Sababu Gani Uendelee Kuwa Na Bidii Katika Kazi Ya Kuhuburi?

  • Kazi ya kuhubiri inatimiza unabii wa Biblia.​—Mk. 13:10.

  • Tunaonyesha kwamba tuko watiifu wakati tunafanya wanafunzi.​—Mt. 28:19, 20.

  • Yehova anapenda watu wabaya wajue mambo yenye itawapata ikiwa hawabadilishe mwenendo wao.​—Eze. 3:19.

  • Tuko na deni ya kuhubiria wengine habari njema.​—Mdo. 20:26, 27; Rom. 1:14, 15.

  • Kazi ya kuhubiri inatufanya tusikuwe na deni ya damu.​—Eze. 3:18.

  • Ni lazima tufundishe wengine kweli ya Biblia ili tuokolewe na kuokoa wengine.​—1 Tim. 4:16.

  • Kuzungumuza juu ya Yehova na kumusifu mbele ya watu wengine ni sehemu ya maana sana ya ibada yetu.​—Ebr. 13:15.

  • Tunaonyesha upendo wetu kwa Yehova na kwa Yesu wakati tunatii na kufanya kazi ya kuhubiri.​—Yoh. 14:15; 1 Yoh. 5:3.

  • Kazi ya kuhubiri inatusaidia kuonyesha kwamba Shetani ni muongo.​—Isa. 43:10-12; 2 Kor. 4:4.

Ujiwekee Miradi Yenye Unaweza Kufikia

  • Ujifanyie programu ya mahubiri ya kila juma, na ujikaze kuiheshimia.

  • Kila mara, ujikaze kuanzisha funzo la Biblia wakati unahubiria mutu fulani.

  • Ikiwa inawezekana, usome hata andiko moja wakati unahubiria mutu fulani.

  • Ongeza hesabu ya magazeti yenye unatolea watu.

  • Rudilia wale wote wenye wanasikiliza ujumbe wa ufalme.

  • Tumia njia mbalimbali za kuhubiri.

  • Tafuta nafasi zaidi za kuhubiri wakati haukupanga kufanya hivyo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine