Kuhudhuria Mikutano kwa Ukawaida—Jambo la Kutanguliza
1 Familia za Kikristo zinatanguliza jambo la kuhudhuria mikutano ya kutaniko kwa ukawaida. Lakini mambo ambayo maisha yanadai leo yanaweza kuleta tatizo. Je, kazi za nyumbani, kazi ya kimwili, au kazi ya shuleni zinaanza kuingilia wakati uliowekwa kwa ajili ya ibada ya Yehova? Kuona mambo kama vile Yehova anavyoyaona kutatusaidia tulinde akilini mambo ya kutanguliza.—1 Sam. 24:6; 26:11.
2 Kwa kukusanya kuni siku ya Sabato, Mwisraeli mmoja alishindwa kwa makusudi kuona mambo kama vile Yehova anavyoyaona. Huenda alifikiri kwamba alikuwa akifanya hivyo kwa ajili ya familia yake au kwamba lilikuwa tu jambo dogo. Hata hivyo, kupitia hukumu iliyotolewa, Yehova alionyesha kwamba kufuatia shughuli za kawaida mnamo nyakati zilizowekwa kwa ajili ya ibada ni jambo nzito.—Hes. 15:32-36.
3 Jinsi ya Kupambana na Matatizo: Kwa wengi ni pambano kufanya kazi ya kimwili isiwazuie kuhudhuria mikutano. Wengi wamepambana na tatizo hilo kwa kuongea na bwana wao wa kazi, kwa kubadilishana nyakati na wafanyakazi wenzao, kwa kutafuta kazi inayofaa zaidi, au kwa kurahisisha mtindo-maisha wao. Kwa hakika, dhabihu hizo kwa ajili ya ibada ya kweli ni zenye kumpendeza vema Mungu.—Ebr. 13:16.
4 Kazi ya shule pia inaweza kuleta tatizo. “Ninafanya sehemu moja ya kazi ya shule kabla ya mikutano, na kufanya ile yenye kubaki baada ya mikutano,” alisema binti mmoja. Ikiwa kazi ya kufanyia nyumbani ambayo mtu anapewa shuleni haiwezi yote kumalizwa siku ya mikutano, wazazi fulani wameelezea walimu kwamba kuhudhuria mikutano ya Kikristo ni jambo ambalo familia yao inatanguliza.
5 Kushirikiana na kuwa na mpango mzuri ni kwa maana kwa kutimiza kazi za nyumbani za kila siku ili kujitayarisha katika familia kwa ajili ya kuhudhuria mikutano pa wakati. (Met. 20:18) Hata watoto wenye umri mdogo zaidi wanaweza kufundishwa kuvaa na kuwa tayari pa wakati kamili ili kwenda kwenye mikutano. Kupitia mfano wao, wazazi wanaweza kukazia umaana wa mikutano kwa watoto wao.—Met. 20:7.
6 Kwa kuwa mikazo ya mfumo wa mambo wa sasa inaongezeka, ni jambo la maana kwamba tuhudhurie mikutano ya kutaniko kwa ukawaida. Acheni tuendelee kuona mambo kama vile Yehova anavyoyaona na tufanye kuhudhuria mikutano kwa ukawaida liwe jambo la kutanguliza.—Ebr. 10:24, 25.