Shambulio la Majeshi ya Wapanda-Farasi Linalokuhusu
1 “Na malaika wa sita akaipiga tarumbeta.” Baada ya hapo, “majeshi ya askari wapanda-farasi” wenye kuhesabika kuwa “makumi mawili ya maelfu ya makumi ya maelfu” wanatoa sauti kama ya ngurumo. Hilo si jeshi la kawaida. “Na vichwa vya farasi wale [ni] kama vichwa vya simba.” Moto, moshi, na moto wa kiberiti vinatoka katika vinywa vyao, na “mikia yao ni kama nyoka.” Shambulio hilo la ufananisho la majeshi ya wapanda-farasi linatokeza angamizo. (Ufu. 9:13-19) Je, unajua jinsi unavyohusika katika utimizo wa ono hilo la vita hivyo vya kiunabii?
2 Mabaki watiwa-mafuta na waandamani wao, kondoo wengine, kwa umoja wanajulisha hukumu za Mungu. Hilo linafanya hali ya Jumuiya ya wakristo ya kuwa wafu kiroho ionekane wazi. Acheni tuchunguze mambo mawili ya ono hilo yanayoonyesha kwa nini huduma ya watumishi wa Mungu ni yenye kuwa na matokeo hivyo.
3 Wamezoezwa na Kupewa Vifaa ili Kutangaza Ujumbe wa Mungu: Kupitia Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na mikutano mingine ya kutaniko, Wahudumu wa Mungu wamezoezwa kusema ujumbe wa Mungu kwa mamlaka. Wakiiga Yesu na wanafunzi wake, wanaenda kutafuta wale wanaostahili, wakihubiri mahali potepote ambapo watu wanaweza kupatikana. (Mt. 10:11; Marko 1:16; Luka 4:15; Mdo. 20:18-20) Njia hii yenye kutegemea Biblia imekuwa yenye matokeo kama nini!
4 Mamilioni ya Biblia, vitabu, broshua, na magazeti yamegawanywa na wahudumu wa Kikristo katika kutimiza utume wao wa kimungu wa kuhubiri. Vichapo hivyo vimeandaliwa katika lugha karibu 400, vikizungumzia habari nyingi mbalimbali na vikitumia njia zinazovutia aina mbalimbali ya watu. Je, wewe ni mwenye kutumia vichapo hivyo kama inavyofaa?
5 Mwongozo na Tegemezo la Mungu: Ono hilo la kiunabii pia linaonyesha wazi kwamba utendaji unaofananishwa na shambulio la majeshi ya wapanda-farasi la mfano linategemezwa na Mungu. (Ufu. 9:13-15) Kazi ya kuhubiri ya ulimwenguni pote si yenye kutimizwa kupitia hekima au uwezo wa mwanadamu, lakini kupitia roho ya Mungu. (Zek. 4:6) Yehova ni mwenye kutumia malaika waongoze kazi hiyo. (Ufu. 14:6) Kwa hiyo, pamoja na jitihada za mashahidi wake wa kidunia, Yehova anaandaa tegemezo lake ili kuvuta wapole kwake.—Yoh. 6:45, 65.
6 Wakiwa wenye kuzoezwa, kuwa na vifaa ili kutoa ujumbe wa Mungu, na kutumika chini ya uongozi wa kimalaika, watu wa Yehova wana nguvu isiyoweza kukomeshwa. Na tuendelee kutimiza sehemu yetu katika utimizo wa ono hili lenye kusisimua.
[Maulizo ya Funzo]
1, 2. Watumishi wa Mungu leo wanahusikaje katika utimizo wa ono la kiunabii linalosimuliwa katika Ufunuo 9:13-19?
3. Ni mazoezi gani ambayo umepata ili kusema ujumbe wa Mungu kwa matokeo?
4. Wahubiri wengi wana vifaa gani ili kuwawezesha watimize kazi yao?
5, 6. Ni nini kinachoonyesha kwamba watu wa Yehova wana tegemezo la Mungu?