Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/04 uku. 8
  • Tuige Mtazamo wa Akili wa Yesu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuige Mtazamo wa Akili wa Yesu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uige Yesu kwa Kuwa Tayari Kutumikia Wengine
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Mradi Unaofaa kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Tutafute Mapainia Wasaidizi 100,000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Tumuige Ule Mwenye Ametuahidi Uzima wa Milele
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 4/04 uku. 8

Tuige Mtazamo wa Akili wa Yesu

1 Ijapokuwa hatujapata kumuona Yesu, Mwana wa Mungu, kupitia simulizi lililoandikwa kuhusu maisha na huduma yake, tumekuja kumpenda kweli. (1 Pet. 1:8) Kwa kutii mapenzi ya Baba yake, aliacha cheo chake cha juu sana cha kimbingu na kuja duniani. Akiwa mwanadamu, alihudumia wengine bila ubinafsi na hivyo kutoa uzima wake kwa ajili ya wanadamu. (Mt. 20:28) Neno la Mungu linatusihi: “Iweni na mtazamo huu wa akili ndani yenu ambao ulikuwa pia ndani ya Kristo Yesu.” Tunawezaje kuiga roho yake ya kujinyima?—Flp. 2:5-8.

2 Tunapojisikia Kuchoka: Ijapokuwa Yesu alikuwa mkamilifu, bado alijisikia kuchoka. Kwenye pindi moja, alipokuwa “amechoka kwa sababu ya safari,” alitoa ushahidi kamili kwa mwanamke Msamaria. (Yoh. 4:6) Wakristo wengi leo wanapambana na tatizo lenye kufanana na hilo. Baada ya kazi yenye kuchosha katika juma, inaweza kuwa vigumu kupata nguvu ya kushiriki katika kazi ya kuhubiri. Lakini, ikiwa tunashiriki katika kazi hiyo kwa ukawaida, tutavumbua kwamba huduma ya Kikristo inatuburudisha kiroho.—Yoh. 4:32-34.

3 Kwenye pindi nyingine, Yesu na wanafunzi wake walienda mahali pasipo na watu ili kupumzika kidogo. Hata hivyo, umati mkubwa ulipata kujua hilo na ukakimbia mbele yao ili kuwatangulia. Badala ya kusumbuliwa na jambo hilo, Yesu “akawasikitikia” naye akaanza “kuwafundisha mambo mengi.” (Marko 6:30-34) Mtazamo kama huo unahitajiwa ili kuanzisha na kuongoza mafunzo ya Biblia. Jambo hilo linaomba jitihada yenye kudumu na upendo wa kweli kwa watu. Ikiwa wewe si mwenye kuongoza funzo la Biblia kwa sasa, usikate tamaa katika kujaribu kutafuta funzo la Biblia.

4 Tutangulize Faida za Kiroho: Kufanya upainia msaidizi kunaweza kutusaidia tukaze fikira zaidi juu ya utendaji mbalimbali wa kiroho. Dada mmoja kijana aliandika: “Mama ya mmoja wa marafiki wangu alitutia moyo sisi wawili kufanya upainia msaidizi pamoja naye kwa mwezi mmoja. Mimi ni mwenye furaha kweli kwamba tuliambatana naye. Nilifurahia kupata kujua ndugu na dada vizuri zaidi, na baada ya muda kidogo tukawa kama watu wa jamaa moja. Nilifurahia pia kuwa na nafasi zaidi ya kuongea na wengine kuhusu Yehova na kuwafundisha kweli nzuri ajabu za Ufalme. Yote hayo yalifanya nijisikie kuwa karibu sana na Yehova na tengenezo lake.”—Zab. 34:8.

5 Sisi sote tunapambana na pigano kati ya mwili wetu usiokamilika na tamaa yetu ya kumpendeza Yehova. (Rom. 7:21-23) Tunapaswa kupinga roho ya ulimwengu ya kutokujitahidi mwenyewe. (Mt. 16:22, 23) Yehova anaweza kutusaidia tufanikiwe katika jambo hilo kwa njia ya roho takatifu yake. (Gal. 5:16, 17) Tunapongojea wokovu wetu kuingia katika ulimwengu mpya wa Mungu wenye haki, na tuige mtazamo wa akili wa Yesu kwa kutanguliza faida za Ufalme na za wengine mbele ya faida zetu.—Mt. 6:33; Rom. 15:1-3.

[Maulizo ya Funzo]

1. Ni mtazamo gani wa akili ambao Yesu alionyesha?

2. Wakristo wengi wanapambana na tatizo gani, na ni nini kinachoweza kuwasaidia kulishinda?

3. Tunawezaje kuiga roho ya Yesu ya kuwa tayari kufundisha?

4. Kufanya upainia msaidizi kunaweza kutusaidiaje tuige mtazamo wa akili wa Yesu?

5. Kwa nini tunapaswa kuendelea kujitahidi ili kuiga mtazamo wa akili wa Yesu?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine