Tunapaswa Kuheshimu Mamlaka ya Yehova
Ni jambo gani linalokujia akilini unaposikia majina haya ya zamani: Kora, Dathani, na Abiramu? Uasi! Waliasi nini? Mamlaka ya Kimungu. Maelezo kuhusu mwenendo wao wenye kuhuzunisha yanapatikana katika Hesabu sura ya 16, na habari hiyo inazungumziwa katika makala “Tii kwa Uaminifu Mamlaka ya Kimungu” katika Mnara wa Mlinzi wa Agosti 1, 2002. Litakuwa jambo lenye faida ikiwa utasoma kwanza habari hii na kisha utazame vidio Respecter l’autorité de Jéhovah (Kiingereza). Utaona pambano lililotokea kati ya wana waaminifu wa Kora na baba yao mwasi, aliyeingia katika mapambano na Mwenye Enzi Kuu ya ulimwengu mzima. (Hes. 26:9-11) Drama hiyo inayohusu maisha halisi inapasa kutuchochea sisi sote kukuza ushikamanifu wetu kwa Yehova hata kikamili zaidi.
Unapotazama vidio hiyo, tafuta uhakikisho kwamba Kora na waasi wenzake walishindwa na jaribu la ushikamanifu katika mambo sita ya maana: (1) Namna gani walikosa utii kwa mamlaka ya Kimungu? (2) Namna gani waliacha kiburi, kutaka makuu, na wivu viwaongoze? (3) Namna gani walikazia fikira hali za kutokamilika za wale waliochaguliwa na Yehova? (4) Ni mtazamo gani wa kulalamika waliositawisha? (5) Kwa nini hawakutosheka na mapendeleo yao ya utumishi? (6) Namna gani waliacha urafiki wao au uhusiano wa familia utangulie ushikamanifu wao kwa Mungu?
Fikiria jinsi mambo tunayojifunza katika drama hii ya Biblia yanavyoweza kutumika kuhusu maoni tuliyo nayo kuelekea mamlaka ya Kimungu leo: (1) Namna gani tunapaswa kuitikia maamuzi ya wazee katika kutaniko, na kwa nini? (2) Namna gani tunaweza kuzuia nia isiyofaa inapoingia moyoni mwetu? (3) Namna gani tunapaswa kuitikia hali za kutokamilika za wale waliotiwa ili kutuongoza? (4) Tutafanya nini ikiwa roho ya kulalamika inaanza kusitawishwa katika moyo wetu? (5) Tunapaswa kujisikia namna gani kuhusu mapendeleo yoyote ambayo tumepewa? (6) Ni nani ambao hatupaswi kutanguliza mbele ya ushikamanifu wetu kwa Mungu, na jambo hilo linaweza kuwa jaribu kwetu wakati gani?
Kisha kuzungumzia habari hii katika kutaniko, kwa nini usitazame vidio tena? Acha vidio hiyo ichochee hata zaidi katika akili yako sababu zinazotulazimisha kuheshimu mamlaka ya Yehova kila wakati!—Zab. 18:25; 37:28.