Mkusanyiko wa Wilaya Unatuchochea Kutembea Pamoja na Mungu
“Hii ndiyo njia. Tembeeni ndani yake”! (Isa. 30:21) Mkusanyiko wa Wilaya “Tembea Pamoja na Mungu” ulifanya maneno hayo ya mwelekezo wa Yehova ulio wazi yarudiliwe. Kutumia maagizo tuliyopokea kutatusaidia ‘tuendelee kuangalia sana jinsi tunavyotembea.’ (Efe. 5:15) Kutafakari juu ya yale tuliyojifunza kutatusaidia kadiri ‘tunavyoendelea kutembea katika kweli.’—3 Yohana 3.
Tumieni maulizo yanayofuata pamoja na maandishi binafsi tuliyochukua kwenye mkusanyiko ili kutayarisha na kushiriki katika kujikumbusha programu ya mkusanyiko wa mwaka huu. Kujikumbusha huko kutafanywa kwenye Mkutano wa Utumishi mnamo juma la Oktoba 18.
1. Namna gani Enoko aliweza kutembea pamoja na Mungu ijapokuwa aliishi katika nyakati za misukosuko? (Ebr. 11:1, 5, 6; Yuda 14, 15; kutokana na habari “Tembea Pamoja na Mungu Nyakati za Misukosuko”)
2. Kanuni kwenye Luka 16:10 inaweza kutumiwa katika sehemu gani za maisha? (Kutokana na habari “Je, Wewe Ni ‘Mwaminifu Katika Lililo Dogo Zaidi’?”)
3. (a) Taja mafundisho manne yenye kufaa yanayopatikana katika Hosea sura 6 mpaka 9 ambayo yatatusaidia kutembea pamoja na Mungu. (Hos. 6:6, 7; 7:14; 8:7) (b) Ni mambo gani ya ziada kutoka Hosea sura 10 mpaka 14 yanayotusaidia kutembea pamoja na Mungu? (Kutokana na habari “Unabii wa Hosea Hutusaidia Kutembea Pamoja na Mungu”—Mfululizo)
4. Ni mambo gani yenye kufaa ambayo waume na wake Wakristo wanaweza kufanya ili kulinda ndoa yao iwe yenye nguvu? (Met. 12:4; Efe. 5:29; kutokana na habari “Usitenganishe ‘Kile Ambacho Mungu Ameunganisha’”)
5. Tunaonyesha namna gani kwamba tunaheshimu mikusanyiko yetu mitakatifu? (Mhu. 5:1; Isa. 66:23; kutokana na habari “Kuheshimu Mikusanyiko Yetu Mitakatifu”)
6. (a) Ni sehemu gani tatu za maana kuhusu kazi yetu ya kuhubiri tunazopaswa kufikiria ili kuhakikisha kwamba kushiriki kwetu katika kazi hiyo ni kwa maana? (Isa. 52:7; Zek. 8:23; Marko 6:34) (b) Ni sehemu gani za kichapo Habari Njema kwa Watu wa Mataifa Yote ambazo mnaona kuwa hasa zenye faida? (kutokana na habari “Habari Njema kwa Watu wa Mataifa Yote”; “Kuwasaidia Wale Wanaoongea Lugha Nyingine”)
7. Namna gani tunaweza kuwasaidia wapya kuwa na uhakika wanapotoa ujumbe wa Ufalme? (Amu. 7:17; kutokana na habari “Kuwasaidia Wengi Kujiunga Nasi Katika Huduma”)
8. Tunaonyesha namna gani usadikisho wetu kwamba “ile siku kuu ya Yehova iko karibu”? (Sef. 1:14; kutokana na habari “Tunatembea kwa Imani, Si kwa Kuona”)
9. (a) Jambo la Kukwaza au kukwazika ni lenye uzito kadiri gani? (Marko 9:42-48) (b) Tunawezaje kuepuka kukwazika? (Zab. 119:165) (c) Tunawezaje kuepuka kuwakwaza wengine? (1 Kor. 10:24; kutokana na habari “Epuka ‘Sababu Yoyote ya Kukwaza’”)
10. Namna gani tunaweza kudumisha usawaziko wetu katika kutafuta mwenzi wa ndoa, kufuatia afya njema, na kushughulikia mambo ya biashara? (Zab. 26:4; Mt. 6:25; 1 Tim. 6:9; kutokana na habari “Tunzeni Akili Zenu kwa Ukamili”)
11. (a) Ni jambo gani la maana linalojitokeza kuhusu vipindi Yesu alipotolewa ukaribishaji? (Luka 10:42; 24:32) (b) Namna gani tunaweza kutosheleza mahitaji ya kujiburudisha kwa namna inayotufanya sisi na wengine tujisikie kuwa wenye kustarehe? (1 Kor. 10:31-33; kutokana na habari “Utendaji Unaojenga na Kuburudisha”)
12. Kulingana na Zaburi ya 23, ni baraka gani tunazopokea tukiwa kondoo za Yehova, na tuna madaraka gani? (1 Kor. 10:21; kutokana na habari “Yehova Ni Mchungaji Wetu”)
13. Namna gani Wakristo wanatoa uangalifu kwenye shauri linaloongozwa na roho ya Mungu la ‘kujinunulia wakati unaofaa’? (Efe. 5:16; kutokana na habari “Kununua Wakati Unaofaa”)
14. (a) ‘Saa ya hukumu’ ambayo inatajwa kwenye Ufunuo 14:7 inatia ndani nini? (b) Tunatoa uthibitisho namna gani kwamba tumejitenga kwelikweli na Babiloni Mkubwa? (kutokana na habari “‘Endeleeni Kukesha’—Saa ya Hukumu Imefika”) (c) Katika broshua Endeleeni Kukesha!, ni mambo gani mliyofurahia?
15. Taja sifa tatu zinazohitajiwa ili kutulinda ‘tusiiache njia iliyo nyoofu.’ (2 Pet. 2:15; kutokana na habari “Jilinde ‘Usiiache Njia Iliyo Nyoofu’”)
16. Namna gani vijana wanaweza kuepuka “pito la waovu”? (Met. 4:14; kutokana na habari “Enyi Vijana, Tembeeni Katika Njia ya Uadilifu”)
17. (a) Ni njia gani ambazo katika hizo Paulo alikuwa mfano bora kabisa wa uvumilivu? (Mdo. 14:19, 20; 16:25-33) (b) Kwa nini si lazima kuwaogopa wapinzani wa ibada ya kweli? (Drama na hotuba “Toa Ushahidi Kamili Leo Licha ya Upinzani”)
18. Ni baraka gani zinazowajia wale wanaotembea pamoja na Mungu? (kutokana na habari “Kutembea Pamoja na Mungu Huleta Baraka Sasa na Milele”)
Na tuazimie kusikiliza ‘neno nyuma yetu’ ili tupate kutembea pamoja na Baba yetu aliye mbinguni kwa milele.—Isa. 30:21; Yoh. 3:36.