Msaada Wako Unahitajiwa
1 “Asante kwa yote mnayofanya kwa ajili yetu. Kazi yenu inatufaidi sana.” Maelezo hayo yanaonyesha vizuri jinsi tulivyo wenye shukrani kuhusu wazee wetu na watumishi wa huduma. Kwa kuwa tengenezo la Mungu linaendelea kupanuka, bado kuna uhitaji wa wanaume wenye kukomaa ili kutumikia katika karibu makutaniko 100,000 ulimwenguni pote. Ikiwa wewe ni ndugu aliyebatizwa, msaada wako unahitajiwa.
2 ‘Kujitahidi Kufikia’: Unawezaje kufikia mapendeleo ya ziada ya utumishi? (1 Tim. 3:1) Hasa, ni kwa kuwa na mfano bora katika sehemu zote za maisha yako. (1 Tim. 4:12; Tito 2:6-8; 1 Pet. 5:3) Shiriki kikamili katika kazi ya kuhubiri, na usaidie wengine wafanye hivyo. (2 Tim. 4:5) Pendezwa kikweli na hali njema ya waamini wenzako. (Rom. 12:13) Uwe mwanafunzi mwenye bidii wa Neno la Mungu, na ukuze “ufundi [...] wa kufundisha.” (Tito 1:9; 1 Tim. 4:13) Shughulikia kwa bidii migawo ambayo wazee wanakukabidhi. (1 Tim. 3:10) Ikiwa wewe ni kichwa cha familia, ‘simamia nyumba yako kwa njia nzuri.’ —1 Tim. 3:4, 5, 12.
3 Kutumika ukiwa mtumishi wa huduma au mzee ni kazi ngumu na jambo hilo linaomba roho ya kujinyima. (1 Tim. 5:17) Kwa hiyo, unapofikia mapendeleo hayo, fikiria kutumikia wengine kwa unyenyekevu. (Mt. 20:25-28; Yoh. 13:3-5, 12-17) Tafakari juu ya mwelekeo wa akili wa Timotheo, na tafuta kuuiga. (Flp. 2:20-22) Kama Timotheo, acha mwenendo wako bora ukupendekeze. (Mdo. 16:1, 2) Kadiri unavyokuza sifa za kiroho zinazohitajiwa ili kuwa na mapendeleo ya ziada na kutumia shauri lolote unalopokea kutoka kwa wengine ili kufanya mambo yawe bora, ndivyo “maendeleo yako [yatakuwa] wazi kwa watu wote.”—1 Tim. 4:15.
4 Wazazi, Zoezeni Vijana Ili Wasaidie: Watoto wanaweza kujifunza kusaidia tangu umri wa mapema. Wazoeze kuwa waangalifu kwenye mikutano, kuhubiri, na kuwa mifano katika mwenendo kwenye Jumba la Ufalme na shuleni. Wafundishe kushiriki katika kutumikia wengine, kufanya mambo kama vile kushiriki katika usafi wa Jumba la Ufalme, kusaidia wazeewazee, n.k. Acha wapate furaha inayotokana na kutoa. (Mdo. 20:35) Mazoezi hayo yanaweza kuwasaidia wawe mapainia, watumishi wa huduma, na wazee wa kesho.