‘Wajaribiwe kuwa wanafaa’—jinsi gani?
1 Kwa kuwa kuna ongezeko lenye kuendelea katika tengenezo la Yehova, kuna uhitaji wenye kuendelea wa akina ndugu wenye sifa za kuwastahilisha ili kutumika wakiwa watumishi wa huduma. Ndugu wengi ambao bado hawajawekwa rasmi, kutia ndani matineja, wana tamaa ya kutumikia katika kutaniko. Wanapopewa mgawo wa kufanya kazi ya ziada, hao hujisikia wenye mafaa na wenye kutimiza kazi. Maendeleo yao mengine yanategemea ‘kujaribiwa juu ya kufaa’ kwao. (1 Tim. 3:10) Hilo hutimizwaje?
2 Daraka la Wazee: Ikiwa sehemu ya kumpima ndugu kwa msingi wa sifa za Kimaandiko za watumishi wa huduma zinazopatikana kwenye 1 Timotheo 3:8-13, wazee watajaribu waone ikiwa ndugu huyo anafaa ili kuchukua madaraka. Wanaweza kumpa mgawo wa kutimiza kazi zenye kusaidia kuhusiana na kugawa magazeti na vichapo, kushika maikrofoni, kutunza Jumba la Ufalme, na kadhalika. Wazee wataangalia jinsi anavyoitikia na kutimiza migawo yake. Watatafuta sifa za kutumainika, kuheshimu wakati, bidii, kiasi, roho yenye nia nzuri, na uwezo wa kushirikiana na wengine. (Flp. 2:20) Je, yeye ni mwenye mfano wa kuigwa katika kuvaa na kujipamba kwake? Je, yeye ni mtu awezaye kutimiza madaraka? Wanataka kuona “kutokana na mwenendo wake bora kazi zake kwa upole ulio wa hekima.” (Yak. 3:13) Je, yeye ni mwenye kujistahilisha kutoa msaada katika kutaniko? Je, yeye ni mwenye kutimiza amri ya Yesu ya ‘kufanya wanafunzi kutoka kwa watu’ kwa kushiriki kwa bidii katika huduma ya shambani?—Mt. 28:19; ona Mnara wa Mlinzi wa Septemba 1, 1990, kurasa 18-28.
3 Ingawa hakuna umri ulioamuliwa ambao kabla ya huo mtu hawezi kuwekwa rasmi kuwa mtumishi wa huduma, Biblia inasema kuhusu akina ndugu hao kuwa “[wanaume] wahudumuo.” Tunaweza kwa shida kuwatazamia kuwa katika miaka yao ya mwanzoni au ya katikati ya utineja, zaidi sana kwa kuwa uwezekano wa kuwa na mke na watoto unatajwa. (1 Tim. 3:12, 13) Wanaume kama hao hawapaswi kuwa wenye kujiacha waongozwe na “tamaa zenye kutukia ujanani” lakini wanapaswa kuwa wenye kujiendesha vizuri, wakiwa na msimamo mzuri na dhamiri safi mbele ya Mungu na mbele ya watu.—2 Tim. 2:22.
4 Ingawa uwezo wa kiasili ni wenye mafaa, mtazamo na roho ya mtu ndivyo vya maana zaidi. Je, ndugu fulani anatamani kwa unyenyekevu kumtukuza Mungu na kuhudumia ndugu zake? Ikiwa ni hivyo, Yehova atabariki jitihada zake za kufanya maendeleo katika kutaniko.