Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Jan. 15
“Sisi sote tunatamani kuwa na maisha bora kwa ajili yetu wenyewe na watoto wetu pia, lakini wengi wanakosa uwezo wa kutimiza jambo hilo. Je, unafikiri kwamba tunaweza kuwa na uwezo wa kuamua kuhusu wakati wetu ujao? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaonyesha kutoka Biblia kwamba sisi tuna uwezo, pia kwamba wakati wetu ujao unategemea jinsi tunavyochagua mambo sasa.” Soma Kumbukumbu la Torati 30:19.
Amkeni! Jan. 22
“Tunapopambana na matatizo ya afya, sisi sote tunathamini daktari anayefikiria mawazo yetu. Lakini je, unafikiri kwamba wagonjwa wengi hawafikirii mawazo ya madaktari wao? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linachunguza magumu ambayo madaktari wanapambana nayo na tumaini la wakati ujao kuhusu matunzo.” Soma Isaya 33:24.
Mnara wa Mlinzi Feb. 1
“Je, si jambo lenye kusumbua kuona kwamba watu wengi leo wanapatwa na uonevu na jeuri? [Taja mfano mmoja wa karibuni unaojulikana kwenu, na acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi Mungu anavyoona maisha ya kibinadamu. Linaeleza pia jinsi atakavyotuokoa kutoka mateso yaliyopo leo.” Soma Zaburi 72:12-14.
Amkeni! Feb. 8
“Moja kati ya magumu makubwa tunayopambana nayo leo ni kukabiliana na mikazo (stress). Je, haukubaliani na hilo? [Acha mtu ajibu.] Biblia ilitabiri kwa usahihi kwamba hilo lingekuwa hivyo. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Gazeti hili linatoa mapendekezo yenye kufaa yanayoweza kukusaidia wewe na familia yako kupambana na mikazo.”