Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/01/07
“Unafikiri ni wapi ambapo watu wenye kuoana wanaweza kupata mashauri yenye kutegemeka? [Acha mtu ajibu.] Ona ni nani alyeanzisha ndoa. [Soma Mwanzo 2:22.] Mungu alitoa pia maagizo kuhusu daraka lenye heshima la mume na mke. Gazeti hili linaeleza jambo hilo.”
Amkeni! Mwezi wa 1
“Je, umetambua kwamba watu wengi wanaojiita kuwa Wakristo hawafuati mafundisho ya Yesu? [Acha mtu ajibu.] Kwa mfano, watu wengi hawafuati maneno haya ya Yesu. [Soma Yohana 13:35.] Habari hii inazungumzia jinsi mafundisho ya Yesu yalivyo tofauti na maoni ya watu wengi wanaojiita kuwa Wakristo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi 1/02/07
“Je, unafikiri kwamba mahali tunapoishi pangekuwa pazuri sana ikiwa kila mtu angetii maneno haya? [Soma Waefeso 4:25. Kisha acha mtu ajibu.] Watu wengi wanafikiri kwamba kusema uongo kunakubaliwa katika hali fulani. Gazeti hili linaeleza faida za kusema kweli sikuzote.”
Amkeni! Mwezi wa 2
“Inaonekana kwamba mahali fulani mawazo ya watu kuhusu dini ni yenye kubadilika. Je, unafikiri kwamba makanisa yanapoteza nguvu yayo? [Acha mtu ajibu.] Maneno haya ya mtume Paulo yanaonyesha kwa nini watu fulani hawatumainie tena dini. [Soma Matendo 20:29, 30.] Gazeti hili linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusu yale yatakayopata Ukristo.”