Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/05 uku. 3-5
  • Majira ya Ukumbusho—Wakati wa Utendaji Wenye Kuongezeka

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Majira ya Ukumbusho—Wakati wa Utendaji Wenye Kuongezeka
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je! Tutafanya Hilo Tena?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • ‘Toa Ushahidi Kamili Kuhusu Habari Njema’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Tutafute Mapainia Wasaidizi 100,000
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • ‘Hubiri Neno la Mungu Kikamili’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 2/05 uku. 3-5

Majira ya Ukumbusho—Wakati wa Utendaji Wenye Kuongezeka

1. “Sherehe za majira” zilikuwa na uvutano gani juu ya Waisraeli waliomwogopa Mungu?

1 Kwa wakati uliochaguliwa mnamo mwaka, Waisraeli wa kale waliadhimisha “sherehe za majira za Yehova.” (Law. 23:2) Kuchukua wakati ili kutafakari juu ya wema wa Mungu wao kulitokeza furaha kubwa na kuliwachochea kuwa wenye bidii kwa ajili ya ibada safi. —2 Sik. 30:21–31:2.

2, 3. Kwa nini ni jambo lenye kufaa kwamba tuongeze utendaji wetu wa kiroho mnamo majira ya Ukumbusho, na tutaadhimisha Ukumbusho wakati gani?

2 Katika nyakati za kisasa, utendaji wetu wa kitheokrasi wenye kuleta furaha unaongezeka kila mwaka mnamo majira ya Ukumbusho. Ni wakati ambapo tunatafakari kabisa juu ya zawadi yenye thamani ambayo Yehova alitoa kwa ajili yetu—Mwana wake mzaliwa-pekee. (Yoh. 3:16; 1 Pet. 1:18, 19) Tunapotafakari juu ya upendo ambao Yehova na Mwana wake wametuonyesha, tunachochewa kumtolea Yehova sifa na kujitahidi katika kufanya mapenzi yake.—2 Kor. 5:14, 15.

3 Mwaka huu Mlo wa Bwana wa Jioni utaadhimishwa siku ya Nne, Machi 24, baada ya jua kutua. Namna gani tunaweza kuongeza kushiri kwetu katika huduma mnamo miezi ya Machi, Aprili, na Mei?

4, 5. (a) Ni jambo gani ambalo limesaidia wahubiri wengine kufikishia watu wengi habari njema? (b) Ni njia gani ambayo umeona kwamba ina matokeo katika eneo lenu?

4 Kufikia Watu Zaidi: Tafuta njia za kukutana na watu wengi zaidi iwezekanavyo unaposhiriki katika utumishi wa shambani. Je, unaweza kufanya mpango ili kushiriki katika kazi ya nyumba kwa nyumba wakati watu wengi zaidi wanapatikana nyumbani, kama vile saa za kisha mchana-kati au jioni? Ikiwa ndugu wengine katika kikundi chenu cha funzo la kitabu wangependa kushiriki katika utumishi kabla ya funzo la kitabu, mwangalizi wa funzo la kitabu anaweza kufanya mpango kuwe na mkutano mfupi kwa ajili ya utumishi wa shambani ili kutumika katika eneo la kandokando.

5 Njia nyingine ya kufikia watu wengi ni kutoa ushahidi mahali pa watu wote. Dada mmoja katika Japani alitaka kufanya upainia msaidizi ijapokuwa alikuwa na kazi ya kimwili ya wakati wote. Mzee mmoja alimtolea pendekezo la kutoa ushahidi wa barabarani, kando ya kituo cha gari-moshi, kila siku kabla ya kwenda kwenye kazi yake ya kimwili. Kisha kushinda utu wake wa haya na zihaka ya wafanyakazi wengine wanaosafiri naye, alipata watu 40 wakuachia magazeti kwa ukawaida, kutia ndani wafanyakazi wengine wanaosafiri naye, watu wanaofanya kazi kwenye kituo cha gari-moshi, na wenye maduka ya kandokando ya kituo hicho. Alitolea watu magazeti 235 kila mwezi kwa wastani. Kwa kuzungumza na watu habari za Kimaandiko kwa muda mfupi tu kila siku, aliweza kuanzisha mafunzo sita ya Biblia.

6. Namna gani vijana wanaweza kuongeza utendaji wao wa kiroho?

6 Nafasi za Kutoa Ushahidi: Wahubiri wengi ambao bado wanaenda shuleni wanavyo vipindi vya mapumziko katika mwaka. Vipindi hivyo vinaweza kukutolea nafasi nzuri ya kufanya upainia msaidizi. Kwa kuongezea, vijana Wakristo wanaweza kuongeza utendaji wao kwa kutoa ushahidi shuleni. Huenda ukashangazwa kuona jinsi wanashule wenzako watakavyopendezwa na mambo yenye kuhusu imani yako. Kwa nini usichukue nafasi wakati wa mazungumzo ya darasani au mnapoombwa kuandika jambo fulani ili kutoa ushahidi? Wengine waliweza kutoa ushahidi hivyo wakitumia vidio zetu. Wengine wameanzisha mafunzo ya Biblia na wanashule wenzao na kuwasaidia kuendelea mpaka wakfu na ubatizo. Hizo ni njia nzuri za ‘kusifu jina la Yehova.’—Zab. 148:12, 13.

7. (a) Namna gani ndugu mmoja alitumia nafasi za kutolea wengine ushahidi? (b) Je, umekwisha kupata jambo lilionwa kama hilo?

7 Katika programu yako ya kila siku, tafuta njia za kuzungumza na watu kuhusu Mungu wetu wa ajabu na ahadi zake za ajabu. Ndugu mmoja aliyesafiri katika gari-moshi kila siku alitoa ushahidi kwa wasafiri wenzake ilipowezekana. Kwa mfano, alipokuwa akingojea ili achukue gari-moshi lingine kwenye kituo kingine, alitoa ushahidi kwa kijana mmoja kila siku kwa dakika tano hivi. Matokeo yalikuwa kwamba, kijana huyo na mfanyakazi mwenzake walikubali funzo la Biblia. Funzo la Biblia liliongozwa katika gari-moshi walipokuwa wakisafiri. Wakati fulani baadaye, mwanamke mmoja mzeemzee aliyesikiliza mazungumzo yao akakaribia ndugu na kuomba funzo la Biblia. Yeye pia ni mwenye kujifunza mnamo siku anazosafiri katika gari-moshi hilo. Katika njia hiyo, ndugu amejifunza na watu kumi tofauti katika gari-moshi hilo wanaposafiri.

8. Ni njia gani ya utumishi inayoweza kusaidia wale walio na vizuizi kwa sababu ya umri mkubwa au matatizo ya afya kuongeza ushirika wao katika huduma?

8 Unaweza kufanya nini ikiwa una kizuizi katika yale ambayo unaweza kufanya kwa sababu ya umri mkubwa au matatizo ya kiafya? Bado kungali njia za kuongeza sifa yako kwa Yehova. Je, umejaribu kutoa ushahidi kwa njia ya simu? Ikiwa hauna uhakika kuhusu jinsi ya kufanya hilo, mwelezee mwangalizi wa funzo lenu la kitabu. Anaweza kuchukua mpango ili wahubiri wanaotumia njia hiyo watumike nawe. Kwa kutumika pamoja kama waandamani, mnaweza kujifunza kutoka kwa mmoja na mwengine na kusaidiana ili kutoa ushahidi wenye matokeo. Mapendekezo bora kuhusu kutoa ushahidi kwa njia ya simu yanaweza kupatikana katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Februari 2001, ukurasa wa 5-6.

9. Namna gani tunaweza kusaidia wanafunzi wa Biblia kutimiza matakwa ili kushiriki pamoja na kutaniko katika huduma ya watu wote?

9 Kuhudhuria Ukumbusho kunaweza kuchochea wapya kumsifu Yehova zaidi. Unaweza kuwasaidia kushinda woga wowote wanaoweza kuwa nao kuhusu kushiriki katika mahubiri ya vivihivi kwa kuwaelezea mambo yaliyoonwa yenye kutia moyo na kwa kuwazoeza hatua kwa hatua kueleza mafundisho ya Biblia na kutetea imani yao. (1 Pet. 3:15) Ikiwa mwanafunzi fulani wa Biblia anaanza kuonyesha tamaa ya kuanza kutangaza habari njema, zungumza na mwangalizi msimamizi. Atachukua mipango ya kukutana na mwanafunzi huyo ili kuona ikiwa anatimiza matakwa ya kushiriki pamoja na kutaniko katika huduma ya watu wote. Hakika hilo litafurahisha moyo wa Yehova kabisa kuona wapya wakisimama upande wake katika kutetea enzi kuu yake.—Met. 27:11.

10. (a) Namna gani programu nzuri inaweza kutusaidia tufanye utimishi wa painia msaidizi? (b) Je, mwaka uliopita mnamo majira ya Ukumbusho, uliweza kufanya mpango wa kupainia? Namna gani ulifikia kufanya hivyo?

10 Je, Unaweza Kuwa Painia Msaidizi? Takwa la painia msaidizi la saa 50 linapaswa kufikiriwa kwa makini. (Mt. 5:37) Hilo linamaanisha kwamba unahitaji kufanya mpango ili kufanya saa 12 katika utumishi wa shambani kila juma. Je, kuna programu ya utumishi wa painia msaidizi, kati ya zile zinazopendekezwa kwenye ukurasa wa 5, inayofaa hali zako? Ikiwa sivyo, je, unaweza kufanya mpango fulani wako mwenyewe utakaokuwezesha kufanya upainia msaidizi katika Machi, Aprili, au Mei? Mwombe Yehova abariki jitihada zako za kuongeza utendaji wa utumishi wako.—Met. 16:3.

11. Namna gani wazee na watumishi wa huduma wanaweza kutegemeza wale watakaotumika kama mapainia wasaidizi?

11 Wazee na watumishi wa huduma watategemeza kikamili jitihada zako za kufanya majira haya ya Ukumbusho kuwa njia moja ya pekee ya kumsifu Yehova. Yaelekea kwamba wengi wao watakuwa mapainia wasaidizi. Wazee watafanya mpango ili kuwe na mikutano ya utumishi ya ziada, kama vile saa za kisha mchana-kati, jioni ya Siku ya Kwanza mpaka Siku ya Tano, na kwenye miisho-juma, kulingana na uhitaji. Ili kukadiria mahali na wakati wa mikutano hiyo na nani atakayekuwa tayari kuongoza, wazee wanaweza kuzungumza na wale walio tayari ili kuanza kupainia au wale wanaofikiria kufanya hivyo. Wazee watajitahidi kuchukua mipango ili kuwe na wahubiri wengine watakaotumika pamoja nawe mnamo siku na wakati uliopanga kwa ajili ya utumishi. Katika njia hiyo, miradi inaweza kusimamishwa kwa nguvu na mambo mengi mazuri yanaweza kutimizwa.—Met. 20:18.

12. Ni nini kinachotuchochea kumsifu Yehova wakati wote?

12 7Fanya Yote Uwezayo: Ikiwa hali zako hazikuruhusu kufanya upainia msaidizi, kumbuka kwamba Yehova anakubali jitihada na dhabihu zetu ‘kulingana na kile ambacho tunacho, si kulingana na kile ambacho hatuna.’ (2 Kor. 8:12) Tuna mambo mengi sana yanayotuchochea tumshukuru Yehova. Kwa sababu nzuri Daudi aliandika: “Nitambariki Yehova nyakati zote, daima sifa yake itakuwa katika kinywa changu.” (Zab. 34:1) Hilo na liwe azimio letu mnamo majira haya ya Ukumbusho.

[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 3]

Utaongezaje Utendaji Wako?

◼ Hubiri wakati watu wanapatikana nyumbani

◼ Toa ushahidi mahali pa watu wote

◼ Hubiri kazini au shuleni

◼ Toa ushahidi kwa njia ya simu

◼ Tumikia ukiwa painia msaidizi

[Muchoro kwenye ukurasa wa 5]

Kielelezo cha Programu Mbalimbali za Utumishi wa Painia Msaidizi​—Njia Mbalimbali za Kufanya Programu Ili Kutimiza Saa 12 Katika Utumishi wa Shambani Kila Juma

Asubuhi​—Siku ya Kwanza Mpaka Siku ya Posho

Siku ya Yenga inaweza kuchukua nafasi ya siku haidhuru gani inayopendekezwa hapo juu.

Siku Wakati Saa

Siku ya Kwanza Asubuhi 2

Siku ya Pili Asubuhi 2

Siku ya Tatu Asubuhi 2

Siku ya Nne Asubuhi 2

Siku ya Tano Asubuhi 2

Siku ya Posho Asubuhi 2

Jumla Saa: 12

Siku Mbili Nzima

Haidhuru siku mbili gani za juma zinaweza kuchaguliwa.

(Ikilingana na siku zilizochaguliwa, programu hii inaweza kufanya tu jumla ya saa 48 kwa mwezi.)

Siku Wakati Saa

Siku ya Tatu Siku Nzima 6

Siku ya Posho Siku Nzima 6

Jumla Saa: 12

Jioni Mbili na Mwisho-Juma

Haidhuru siku gani mbili toka Siku ya Kwanza jioni mpaka Siku ya Tano jioni zinaweza kuchaguliwa.

Siku Wakati Saa

Siku ya Kwanza Jioni 1 1⁄2

Siku ya Tatu Jioni 1 1⁄2

Siku ya Posho Siku Nzima 6

Siku ya Yenga Nusu Siku 3

Jumla Saa: 12

Kisha-Mchana Kati Tatu na Siku ya Posho

Siku ya Yenga inaweza kuchukua nafasi ya haidhuru siku gani.

Siku Wakati Saa

Siku ya Kwanza Kisha Mchana-Kati 2

Siku ya Tatu Kisha Mchana-Kati 2

Siku ya Tano Kisha Mchana-Kati 2

Siku ya Posho Siku Nzima 6

Jumla Saa: 12

Programu Yangu Binafsi ya Utumishi

Amua hesabu ya saa kwa ajili ya kila wakati.

Siku Wakati Saa

Siku ya Kwanza

Siku ya Pili

Siku ya Tatu

Siku ya Nne

Siku ya Tano

Siku ya Posho

Siku ya Yenga

Jumla Saa: 12

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine