Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/05 uku. 1
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Pili
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna ya Kusaidia Wengine Washike Amri za Kristo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Namna ya Kusaidia Wanafunzi wa Biblia Wafikie Kubatizwa—Sehemu ya Kwanza
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 5/05 uku. 1

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Sehemu 9: Kutayarisha Wanafunzi Kutoa Ushahidi wa Vivi Hivi

1 Andrea na Filipo walipotambua kwamba Yesu alikuwa Masihi aliyeahidiwa, hawakuepuka kuwaambia wengine habari hiyo yenye kusisimua. (Yoh. 1:40-45) Hivyohivyo leo, wanafunzi wa Biblia wanapoanza kuamini mambo wanayojifunza, wanachochewa kusema kuhusu hayo. (2 Kor. 4:13) Tunawezaje kuwatia moyo watoe ushahidi wa vivi hivi na kuwatayarisha wafanye hivyo kwa matokeo?

2 Unaweza tu kuuliza mwanafunzi ikiwa ameongea na wengine kuhusu yale ambayo amejifunza kutoka Biblia. Labda kuna marafiki na washiriki wa familia ambao anaweza kualika ili wahudhurie funzo lake. Umuulize ikiwa yeyote, wa wafanyakazi wenzake, wanashule wenzake, au watu anaofahamiana nao, ameonyesha kupendezwa na habari njema. Kwa kufanya hivyo anaweza kuanza kutoa ushahidi. Umsaidie aelewe uhitaji wa kuwa na ufahamu na kuwa mwenye heshima na fadhili anapoongea na wengine kuhusu Yehova Mungu na makusudi yake.—Kol. 4:6; 2 Tim. 2:24, 25.

3 Kuwaelezea Wengine Mambo Wanayoamini: Ni jambo la maana sana kuzoeza wanafunzi wa Biblia kutumia Neno la Mungu wanapowaelezea wengine mambo wanayoamini. Mnapofika kwenye mambo fulani uliyochagua wakati wa funzo lenu, uliza mwanafunzi: “Unawezaje kutumia Biblia ili kufafanua kweli hii kwa familia yako?” au “Ni andiko gani la Biblia unaloweza kutumia ili kutoa uhakikisho wa kweli hiyo kwa rafiki yako?” Sikiliza kwa makini jinsi anavyojibu, na umonyeshe jinsi ya kutegemeza mafundisho yake na Maandiko. (2 Tim. 2:15) Kwa kufanya hivyo, utakuwa ukimtayarisha mwanafunzi kutoa ushahidi wa vivi hivi na, wakati atakapokuwa na sifa ya kustahili, kutoa ushahidi katika kazi ya kuhubiri iliyopangwa na kutaniko.

4 Ni jambo la hekima kutayarisha wanafunzi wa Biblia kupambana na upinzani. (Mt. 10:36; Luka 8:13; 2 Tim. 3:12) Wakati wengine wanapouliza maulizo au kutoa maelezo kuhusu Mashahidi wa Yehova, hilo linaweza kufungua njia kwa wanafunzi kutoa ushahidi. Broshua Mashahidi wa Yehova—Wao Ni Nani? Wanaamini Nini? inaweza kuwatayarisha ili wawe “tayari kujitetea.” (1 Pet. 3:15) Inatoa habari sahihi ambazo wapya wanaweza kutumia ili kusaidia marafiki na washiriki wa familia wenye nia nzuri kuelewa mambo tunayoamini na shughuli zetu zinazotegemea Biblia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine