Kuhubiri Kunatusaidia Kuvumilia
1 Neno la Mungu linatuhimiza “tukimbie kwa uvumilivu shindano la mbio lililowekwa mbele yetu.” (Ebr. 12:1) Kama vile mkimbiaji anavyohitaji uvumilivu ili kushindana kwa mafanikio, sisi pia tunahitaji uvumilivu ili kufikia zawadi ya uzima wa milele. (Ebr. 10:36) Huduma ya Kikristo inawezaje kutusaidia kuvumilia kwa uaminifu mpaka mwisho?—Mt. 24:13.
2 Tunatiwa Nguvu Kiroho: Kutangaza ahadi nzuri ajabu kutoka Biblia kuhusu ulimwengu mpya wenye uadilifu, kunatusaidia kulinda tumaini letu wenyewe likiwa hai. (1 The. 5:8) Tunaposhiriki kwa ukawaida katika huduma ya shambani, tunapata nafasi ya kujulisha kweli ambazo tumejifunza kutoka Biblia. Tuna nafasi ya kutetea imani yetu, na imani hiyo inatusaidia kuwa nguvu kiroho.
3 Ili kufundisha wengine kwa matokeo, tunapaswa sisi wenyewe kuelewa waziwazi kweli za Biblia. Tunapaswa kufanya utafiti na kutafakari juu ya habari tunayofundisha. Jitihada yenye bidii tunayofanya inaongeza kina cha ujuzi wetu, inaimarisha imani yetu, na kutuburudisha kiroho. (Met. 2:3-5) Hivyo, kadiri tunavyojaribu kusaidia wengine, ndivyo tunavyojiimarisha sisi wenyewe.—1 Tim. 4:15, 16.
4 Kushiriki kwa bidii katika huduma ni sehemu ya maana ya “mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu,” ambayo tunahitaji ili kusimama imara na kuwapinga Ibilisi na roho waovu. (Efe. 6:10-13, 15) Kuwa wenye shughuli nyingi katika utumishi mtakatifu, kunatusaidia tuendelee kukaza akili yetu juu ya mambo yenye kujenga na kuepuka kupotoshwa na ulimwengu wa Shetani. (Kol. 3:2) Tunapofundisha wengine njia za Yehova, tunakumbushwa sikuzote uhitaji wetu wa kudumisha mwenendo mtakatifu.—1 Pet. 2:12.
5 Tumepewa Nguvu na Mungu: Mwishowe, kushiriki kwetu katika kazi ya kueneza evanjeli kunatufundisha kumtegemea Yehova. (2 Kor. 4:1, 7) Jambo hilo ni baraka kweli! Kusitawisha tumaini kama hilo hakututolei tu vifaa ili kutimiza huduma yetu lakini pia ili kushughulika na hali zozote tunazoweza kupambana nazo maishani mwetu. (Flp. 4:11-13) Kwa kweli, kujifunza kumtegemea Yehova kikamili ndiyo siri ya kuvumilia. (Zab. 55:22) Katika njia nyingi, kuhubiri kunatusaidia kuvumilia.