Kazi ya Kuhubiri Inatufanya Tuendelee Kuwa Nguvu Kiroho
1. Kazi ya kuhubiri inatutolea faida gani?
1 Kufanya kazi ya kuhubiri kwa bidii kunaweza kututia nguvu kiroho na kuongeza furaha yetu. Bila shaka, tunafanya kazi ya kuhubiri ili kumpendeza kwanza Yehova. Pia, kwa kutii amri ya ‘kuhubiri neno,’ tunabarikiwa na Yehova na tunajifaidi wenyewe katika njia zingine. (2 Tim. 4:2; Isa. 48:17, 18) Namna gani basi kuhubiri kunaweza kututia nguvu na kutufanya tuwe na furaha?
2. Kazi ya kuhubiri inatutia nguvu katika njia gani?
2 Tunabarikiwa na Kutiwa Nguvu: Kazi ya kuhubiri inatusaidia tukazie macho baraka zitakazoletwa na Ufalme kuliko kukazia macho mahangaiko ya leo. (2 Kor. 4:18) Tunapoelezea watu mafundisho ya Biblia, imani yetu inatiwa nguvu katika ahadi za Yehova na tunakuwa wenye shukrani kwa kuwa tunaijua kweli ya Biblia. (Isa. 65:13, 14) Tunaposaidia wengine kukomaa kiroho ili wasiwe “sehemu ya ulimwengu,” kusudi letu la kujitenga na ulimwengu linakuwa nguvu pia.—Yoh. 17:14, 16; Rom. 12:2.
3. Namna gani kazi yetu ya kuhubiri inatusaidia kukomaza sifa za Kikristo?
3 Kufanya kazi ya kuhubiri kunatusaidia kukomaza sifa za Kikristo. Kwa mfano, kujikaza ‘kuwa mambo yote kwa watu wa namna zote’ kunatusaidia kuwa wanyenyekevu zaidi. (1 Kor. 9:19-23) Tunapozungumza na wale ambao “wamechunwa ngozi na kutupwa huku na huku kama kondoo wasio na mchungaji,” tunakuwa wenye huruma na wenye kujitia pa nafasi ya wengine. (Mt. 9:36) Tunajifunza uvumilivu tunapoendelea kuhubiri ijapokuwa tunakutana na watu wasiopendezwa ao wanaopinga. Furaha yetu inaongezeka tunapojitoa ili kusaidia wengine.—Mdo. 20:35.
4. Unaona namna gani kazi yako ya kuhubiri?
4 Ni baraka kubwa sana kufanya utumishi unaomletea sifa yule Mmoja tu anayestahili ibada yetu. Kazi ya kuhubiri inatutia nguvu. Inawatolea baraka nyingi wale ambao wanajihusisha kabisa katika “kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema.”—Mdo. 20:24.