Deni Letu kwa Wengine
1 Mtume Paulo alijisikia kuwa mwenye kulazimishwa kuhubiri watu. Alijua kwamba Yehova alifanya iwezekane kwa watu wa namna zote kuokolewa kupitia damu yenye thamani ya Mwana Wake. (1 Tim. 2:3-6) Kwa hiyo, Paulo alisema: “Mimi nina deni kwa Wagiriki na kwa Wabaribari pia, kwa wenye hekima na kwa wasio na akili pia.” Alifanya kazi ya jasho kwa hamu na bila kuchoka ili kulipa deni lake kwa wanadamu wenzake kwa kuwahubiria habari njema.—Rom. 1:14, 15.
2 Kama Paulo, leo Wakristo wanajitahidi kuhubiria majirani wao habari njema kila mara nafasi inapojitokeza. Kwa kuwa “dhiki kuu” inakaribia sana, ni jambo la haraka kutafuta watu wenye mioyo minyofu. Upendo wa kweli tunao kwa watu na utuchochee kuwa wenye bidii katika kazi hiyo inayookoa uzima.—Mt. 24:21; Eze. 33:8.
3 Jinsi ya Kulipa Deni Letu: Njia kuu ambayo katika hiyo tunafikia watu ni kwa kuhubiri mlango kwa mlango. Katika maeneo ambayo watu wengi hawapatikani nyumbani, tunaweza kuonana na wengi zaidi ikiwa tunalinda maandishi sahihi na kurudi wakati tofauti-tofauti. (1 Kor. 10:33) Tunaweza pia kufikia watu kwa kutoa ushahidi katika eneo la biashara, barabarani, katika mashamba ya wanyama, mahali pa kuegeshea magari, na kwa njia ya simu. Tunaweza kujiuliza, ‘Je, mimi ninafanya yote niwezayo ili kutumia njia zote za kuhubiri ili kuwatolea wengine ujumbe wa uzima?’—Mt. 10:11.
4 Painia moja alijisikia kuwa na daraka nzito la kufikia watu wote katika eneo lake. Kwenye nyumba moja, madirisha yalikuwa sikuzote yenye kufungwa na hakukuwa mtu nyumbani wakati wowote. Lakini, siku moja ambayo painia huyo hakuwa katika utumishi wa shambani, aliona gari mbele ya nyumba hiyo ambako yeye hakuwahi kamwe kukuta mtu. Kwa kuwa yeye hakupenda kukosa nafasi hiyo, alipiga kengele ya mlangoni. Mwanamume mmoja akajibu, na mazungumzo hayo ya kwanza yakaongoza kwenye ziara za kurudia nyingi zilizofanywa na dada huyo pamoja na mume wake. Mwishowe, mtu huyo akakubali funzo la Biblia, na sasa yeye ni ndugu aliyebatizwa. Yeye ni mwenye shukrani kuona kwamba dada huyo alijisikia kuwa na daraka na deni la kuhubiria wengine.
5 Kwa kuwa tunakaribia sana mwisho, sasa ndio wakati wa kulipa deni letu kwa binadamu wenzetu kwa kujitahidi sana katika kazi ya kuhubiri.—2 Kor. 6:1, 2.