Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Juni 15
“Wengi wetu tutapitisha sehemu kubwa ya maisha yetu tukifanya kazi. Watu fulani wanaona jambo hilo kuwa nzuri; wengine wanaliona kuwa jambo lenye kusumbua. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mhubiri 2:24.] Gazeti hili linaonyesha jinsi Biblia inavyoweza kutusaidia tuwe na maoni yenye kusawazika kuhusu kazi. Linazungumzia pia jinsi ya kushughulika na mikazo kazini.”
Amkeni! Juni 22
“Je, unafikiri kwamba maisha yangekuwa bora ikiwa kila mtu angetumia maneno haya? [Soma Waefeso 4:28. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi wizi dukani unavyofanya tuwe wenye kulemewa sana. Linaonyesha pia jinsi tatizo la wizi dukani, na uhalifu mwingine wote, vitakavyokomeshwa hivi karibuni.”
Mnara wa Mlinzi Julai 1
“Sisi wote tunajua watu ambao wanaonekana kuwa wenye kufanikiwa na bado wanajisikia kwamba wanakosa kitu fulani maishani mwao. Unafikiri wanatafuta nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mathayo 5:3.] Gazeti hili linazungumzia jambo la maana ili kupata amani ya moyoni—kutosheleza mahitaji yetu ya kiroho.”
Amkeni! Julai 8
“Leo kupata kazi ni vita kweli, ukosefu wa kazi ni tatizo kubwa. Gazeti hili linaonyesha mambo matano yanayosaidia ili kupata kazi. [Onyesha vichwa vidogo vinavyoandikwa kwa herufi nzito nyeusi katika makala ‘Mambo Matano Yanayosaidia Ili Kupata Kazi.’] Linatoa pia mapendekezo yenye kufaa kuhusu jinsi ya kulinda kazi.” Soma Methali 22:29, inayonukuliwa kwenye ukurasa wa 10.