Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/05 uku. 7
  • Kutoa Ushahidi Bila Neno

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kutoa Ushahidi Bila Neno
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Tutoe Ushahidi Kupitia Mwenendo Mzuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Je, Unaruhusu Roho ya Mungu Ikuongoze?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Unaona Tofauti Yenye Kuwa Kati ya Watu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2018
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 8/05 uku. 7

Kutoa Ushahidi Bila Neno

1 Bila neno, vitu vinavyotokana na uumbaji wa Yehova vinafunua waziwazi sifa zake zisizoonekana. (Zab. 19:1-3; Rom. 1:20) Vivyo hivyo, mwenendo wetu mzuri, sifa za Kikristo, na mvalio wetu wenye kiasi vinatoa ushahidi bila neno. (1 Pet. 2:12; 3:1-4) Tamaa ya kila mmoja wetu inapaswa kuwa ile ya ‘kupamba fundisho la Mwokozi wetu, Mungu, katika mambo yote’ kwa namna tunavyojiendesha.—Tito 2:10.

2 Inawezekanaje kwa wanadamu wasiokamilika kuongezea uvutano kwenye mafundisho ya Biblia? Hilo linawezekana tu kupitia uongozi wa Neno la Mungu na uwezo wa roho takatifu. (Zab. 119:105; 143:10) Neno la Mungu “liko hai nalo lina nguvu na ni lenye makali zaidi kuliko upanga wowote wenye makali kuwili.” (Ebr. 4:12) Linapenya ndani yetu na kutusaidia kuvaa utu mpya. (Kol. 3:9, 10) Roho takatifu inatokeza ndani yetu sifa zenye kupendeza, kama vile fadhili, wema, upole, na kujizuia. (Gal. 5:22, 23) Je, sisi binafsi tunaruhusu Neno la Mungu na roho yake viwe na uvutano katika maisha zetu?—Efe. 4:30; 1 Tes. 2:13.

3 Wengine Wanatambua: Tunapoishi kulingana na viwango vya Yehova na kujitahidi kuonyesha sifa zake, wengine wanatambua hilo. Fikiria kwa mfano, mwanamume aliyedhihakiwa na wafanyakazi wenzake kwa kuwa alikuwa mfupi. Dada aliyetumika katika ofisi hiyohiyo wakati wote alimtendea kwa heshima na adabu. Hilo lilimchochea amuulize dada kwa nini alikuwa tofauti hivyo. Dada alieleza kwamba mwenendo wake wenye heshima ulikuwa matokeo ya kutumia kanuni za Biblia katika maisha yake. Alimzungumzia pia tumaini ajabu la Ufalme. Mwanamume huyo alianza kujifunza Biblia na mwishowe akafanya maendeleo mpaka kufikia ubatizo. Aliporudi kwenye mji wake wa kuzaliwa, watu wa familia yake walivutiwa na mwenendo wake, na wengi kati yao walikubali kweli.

4 Kazini, Shuleni, au katika kushirikiana na watu wa jamaa na majirani, tunaweza kwa mwenendo wetu mzuri, pamoja na ushahidi wetu, kufanya wengine wampe Mungu utukufu.—Mt. 5:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine