Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/05 uku. 8
  • Saidia Wengine Wawe Wenye ‘Kutii Kutoka Moyoni’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Saidia Wengine Wawe Wenye ‘Kutii Kutoka Moyoni’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Kumupenda Mungu Kunamaanisha Hivi’
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Upendo wa Mungu Hauna Mwisho
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Yesu “Alijifunza Kutii”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2025
  • ‘Lazima Umupende Yehova Mungu Wako’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 9/05 uku. 8

Saidia Wengine Wawe Wenye ‘Kutii Kutoka Moyoni’

1 Utii ni jambo la msingi ili kumwabudu Yehova katika njia yenye kukubalika. (Kum. 12:28; 1 Pet. 1:14-16) Hivi karibuni, hukumu ya Mungu itakuja juu ya “wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema.” (2 Tes. 1:8) Tunawezaje kuwasaidia wengine wawe wenye ‘kutii kutoka moyoni’ mafundisho ya Neno la Mungu?—Rom. 6:17.

2 Kuwasaidia Wajenge Imani na Upendo: Katika Maandiko, utii unahusiana sana na imani. Mtume Paulo alizungumzia “amri ya Mungu anayedumu milele ili kuendeleza utii kwa njia ya imani.” (Rom. 16:26) Waebrania sura 11 inataja mifano mingi ya imani, mingi kati ya mifano hiyo inahusisha kutenda kulingana na mapenzi ya Yehova. (Ebr. 11:7, 8, 17) Kwa upande mwingine, ukosefu wa utii unahusiana na kukosa imani. (Yoh. 3:36; Ebr. 3:18, 19) Tunahitaji kusitawisha ufundi katika kutumia Neno la Mungu ili kusaidia wengine wasitawishe namna ya imani inayotokeza utii.—2 Tim. 2:15; Yak. 2:14, 17.

3 Utii unahusianishwa pia na upendo kwa Mungu. (Kum. 5:10; 11:1, 22; 30:16) Andiko la 1 Yohana 5:3 linasema: “Kwa maana kumpenda Mungu humaanisha hivi, kwamba tuzishike amri zake; na bado amri zake si mzigo mzito.” Tunawezaje kusaidia wanafunzi wa Biblia kusitawisha upendo kwa Yehova? Tafuta nafasi muda wa funzo ili kumsaidia athamini sifa za Yehova. Onyesha wewe mwenyewe hisia kuelekea Mungu. Saidia mwanafunzi afikiri jinsi ya kusitawisha uhusiano wa kibinafsi pamoja na Yehova. Zaidi ya yote, upendo kwa Yehova utachochea wengine—na sisi pia—kumtii kutoka moyoni.—Mt. 22:37.

4 Kupitia Mfano Wetu: Njia yenye nguvu ambayo kupitia hiyo tunaweza kutia wengine moyo watii habari njema ni kupitia mfano wetu. Hata hivyo, jitihada yenye kuendelea ni ya maana kwa upande wetu ili kukuza “moyo mtiifu.” (1 Fal. 3:9; Met. 4:23) Hilo linaomba nini? Lisha moyo wako kupitia funzo la Biblia la kawaida na udhurio kwenye mikutano. (Zab. 1:1, 2; Ebr. 10:24, 25) Tafuta kushirikiana na wale ambao mioyo yao inaunganishwa katika ibada ya kweli. (Met. 13:20) Shiriki kwa ukawaida katika huduma ya shambani, ukiwa na tamaa ya kweli ya kusaidia watu katika eneo lako. Sali upate msaada wa Yehova ili ukuongoze ukuze moyo mwema. (Zab. 86:11) Epuka mambo ambayo yanaweza kupotosha moyo wako, kama vile viburudisho visivyo vya adili au vyenye jeuri. Fuatilia mambo yanayokufanya uwe karibu na Mungu na kuimarisha uhusiano wako pamoja naye.—Yak. 4:7, 8.

5 Yehova alihakikishia watu wake wa zamani kwamba wangefikiwa na baraka ikiwa wangemsikiliza. (Kum. 28:1, 2) Hivyohivyo leo, Yehova anabariki sana “wale wanaomtii yeye akiwa mtawala.” (Mdo. 5:32) Kwa hiyo, Kupitia mafundisho yetu na mfano wetu, na tusaidie wengine wawe wenye kutii kutoka moyoni.

[Maulizo ya Funzo]

1. Yehova anataka waabudu wake wafanye nini?

2. Kwa nini ni jambo la maana kusaidia wengine wajenge imani iliyo nguvu?

3. (a) Jinsi gani utii unahusianishwa na upendo? (b) Tunawezaje kuwasaidia wanafunzi wa Biblia wasitawishe upendo kwa Yehova?

4. (a) Kwa nini mfano wetu ni wa maana? (b) Tunapaswa kufanya nini ili kukuza “moyo mtiifu”?

5. Namna gani watu wenye utii wanabarikiwa?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine