MUSEMWA WA BIBLIA
Yesu “Alijifunza Kutii”
Yesu anakuwaka tu mutiifu kwa Baba yake. (Yoh. 8:29) Sasa juu ya nini Biblia inasema: “Alijifunza kutii kutokana na mambo yenye aliteseka”?—Ebr. 5:8.
Wakati alikuwa ku dunia alijikuta mu hali zenye hazikukuwa mbinguni. Alikomalishwa na bazazi benye balimupenda Yehova, lakini habakukuwa bakamilifu. (Lu. 2:51) Viongozi wa dini na wa serikali balimutendea mubaya. (Mt. 26:59; Mk. 15:15) Zaidi ya ile “alijinyenyekeza mwenyewe na kuwa mutiifu mupaka kifo,” kifo ya maumivu sana.—Flp. 2:8.
Ile mambo yote ilimufundisha Yesu utii mu njia ya mupya yenye hakujifunzaka wakati alikuwa mbinguni. Kwa hiyo, angekuwa sasa Mufalme muzuri na Kuhani Mukubwa muzuri mwenye angeweza kujitia fasi yetu. (Ebr. 4:15; 5:9) Na juu alijifunza utiifu kupitia mateso, Yehova alimupenda zaidi na alimutumikisha zaidi. Na siye Yehova atatupenda zaidi na kututumikisha zaidi kama tunaendelea kuwa batiifu mu hali za nguvu.—Yak. 1:4.