Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 10/05 uku. 1
  • Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, wewe unahubiri kwa uhodari?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Andika Majibu ya Maulizo Haya
    Programu ya Mukusanyiko wa Muzunguko wa 2018-2019—Pamoja na Mwangalizi wa Muzunguko
  • Ujasiri
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Utusaidie Tusiogope
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 10/05 uku. 1

Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri

1 Tukiwa wahudumu Wakristo, tunajua kwamba si wote watakaotusikiliza tunapohubiri. (Mt. 10:14) Hata hivyo, haturuhusu itikio lisilofaa la watu fulani lituzuie kutangaza habari njema. (Met. 29:25) Ni jambo gani linalotusaidia tuendelee kusema Neno la Mungu kwa ujasiri?

2 Mtume Paulo alithamini sana “thamani bora zaidi ya kumjua Kristo Yesu.” Jambo hilo lilimchochea kusema kwa “usadikisho wenye nguvu.” (Flp. 3:8; 1 The. 1:5) Ijapokuwa watu fulani waliona ujumbe aliotangaza kuwa kitu dhaifu na cha upumbavu, yeye alielewa kwamba ilikuwa “nguvu za Mungu kwa ajili ya wokovu kwa kila mtu aliye na imani.” (Rom. 1:16) Kwa hiyo, hata wakati alipopambana na upinzani, aliendelea ‘kusema kwa ujasiri kwa mamlaka ya Yehova.’—Mdo. 14:1-7; 20:18-21, 24.

3 Chanzo cha Nguvu Yetu: Haikuwa kwa nguvu zake mwenyewe kwamba Paulo aliweza kutoa ushahidi kwa ujasiri. Akizungumza juu yake mwenyewe na Sila, Paulo aliandika: “Baada ya sisi kuwa tumeteseka kwanza na kutendewa kwa dharau . . . katika Filipi, tulijipa ujasiri kwa njia ya Mungu wetu ili kuwaambia ninyi habari njema ya Mungu kwa kupambana sana.” (1 The. 2:2; Mdo. 16:12, 37) Pia, alipotiwa gerezani huko Roma, Paulo aliomba kwamba wengine wasali kwa ajili yake ili kwamba aendelee kusema habari njema ‘kwa ujasiri kama alivyopaswa kusema.’ (Efe. 6:18-20) Kwa kumtegemea Yehova badala ya kujitegemea, Paulo aliweza kuendelea kusema neno la Mungu kwa ujasiri.—2 Kor. 4:7; Flp. 4:13.

4 Ndivyo ilivyo leo. Ndugu mmoja aliyekuwa na matatizo ya kujitambulisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova mahali pake pa kazi na ya kutoa ushahidi wa vivi hivi alisali kuhusu jambo hilo na kuanza kutoa ushahidi. Mfanyakazi mwenzake alipinga jitihada zake mwanzoni, lakini aliposikia kuhusu tumaini la ufufuo alichochewa kujifunza Biblia. Tangu wakati huo, ndugu anatumia kila nafasi ili kutoa ushahidi. Alipokwenda kutumikia mahali pengine, alisaidia watu 34 wapate ubatizo mnamo kipindi cha miaka 14. Tunaweza kuwa hakika kwamba Yehova atatuimarisha sisi pia ili ‘tuendelee kusema neno lake kwa ujasiri wote.’—Mdo. 4:29.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine