Je, wewe unahubiri kwa uhodari?
1 Ijapokuwa kufungwa na kuogopeshwa na wapinzani, Petro na Yohana waliendelea kutangaza ujumbe wa Ufalme kwa uhodari. (Mdo. 4:17, 21, 31) Kuhubiri kwa uhodari kunamaanisha nini kwetu leo?
2 Kutoa Ushahidi kwa Uhodari: Neno lenye maana moja na “hodari” ni “shujaa,” ambalo linamaanisha “mtu mwenye moyo thabiti anayeweza kukabili mambo, hata kama ni ya hatari, bila ya hofu.” Kwa Wakristo wa kweli, kuhubiri kwa uhodari kunamaanisha mtu kutoogopa kusema maoni yake wakati wowote kunapokuwa nafasi ya kushiriki habari njema pamoja na wengine. (Mdo. 4:20; 1 Pet. 3:15) Kunamaanisha kwamba hatusikii haya ya kushiriki habari njema. (Zab. 119:46; Rom. 1:16; 2 Tim. 1:8) Hivyo, uhodari ni sifa inayohitajiwa ili kutimiza utume wetu wa kuhubiri habari njema ya Ufalme katika wakati huu wa mwisho. Huo unatuchochea kushiriki habari njema na watu mahali popote wanapoweza kupatikana.—Mdo. 4:29; 1 Kor. 9:23.
3 Uhodari Shuleni: Je, mwelekeo wa kuogopa au kusikia haya unafanya iwe vigumu kuhubiria wanashule wenzako? Nyakati nyingine, hilo si jambo jepesi; kwa kweli, linaweza kuwa tatizo kabisa. Hata hivyo, Yehova atakutia nguvu ikiwa unaomba uhodari wa kuhubiria wengine. (Zab. 138:3) Uhodari utakusaidia kujitambulisha kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova na kushindana na dhihaka. Kama tokeo, huenda kuhubiri kwako shuleni kukaokoa wale wanaokusikiliza.—1 Tim. 4:16.
4 Uhodari Kazini: Je, unajulikana kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova kazini? Njia pekee ambayo kwa hiyo wafanyakazi wenzako wanaweza kufikiwa na habari njema huenda ikawa kwa kuwahubiria kwako. Uhodari wako utakusaidia pia kuchukua mapumziko kwa ajili ya mikutano yenu ya Kikristo na mikusanyiko.
5 Hodari Wakati Unapojaribiwa: Kujipatia uhodari ni kwa lazima sana wakati tunapokabiliana na upinzani. (1 Thes. 2:1, 2) Huo unatusaidia kushikamana na imani yetu wakati tunapopatwa na maogopesho, dhihaka, au mateso ya moja kwa moja. (Flp. 1:27, 28) Unatutia nguvu ili kusimama imara wakati tunapokuwa chini ya mkazo wa kukubali mambo yanayovunja ushikamanifu wetu kwa viwango vya Mungu wetu, Yehova. Unatutia nguvu ili kuendeleza hali yetu yenye amani wakati wengine wanapotokeza mabishano.—Rom. 12:18.
6 Hata magumu tunayokabiliana nayo yawe nini, acheni tuendelee kuhubiri habari njema kwa uhodari.—Efe. 6:18-20.