Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/05 uku. 6
  • Yale Ambayo Huduma Yetu Inatimiza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yale Ambayo Huduma Yetu Inatimiza
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Unatimiza kwa Ukamili Utumishi Wako?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
  • Kutambua Umaana wa Kutenda kwa Haraka!
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 11/05 uku. 6

Yale Ambayo Huduma Yetu Inatimiza

1 Neno la Mungu linafafanua Wakristo kuwa wenye kutembea kwa ushindi katika utumishi wa Yehova, kana kwamba ni katika maandamano ya ushindi. (2 Kor. 2:14-16) Kwa kuwa tunajulisha ujuzi wa Mungu, huduma yetu ni kama uvumba wenye kumpendeza Yehova. Watu fulani wanavutiwa na utamu wa habari njema; nao wengine wanaikataa. Lakini itikio lisilofaa la watu wengi halimaanishi kwamba kazi yetu si yenye mafanikio. Fikiria yale ambayo huduma yetu inatimiza.

2 Kumtukuza Yehova: Shetani anadai kwamba wanadamu wanamtumikia Yehova kwa sababu za ubinafsi. (Ayu. 1:9-11) Huduma ya Kikristo inatutolea nafasi ya kuonyesha kwamba ujitoaji wetu kwa Mungu ni wa kweli. Wahubiri wengi wanaendelea kutii amri ya kuhubiri na kufanya wanafunzi ijapokuwa hali ngumu zinazowapata kibinafsi au ubaridi wa watu kwa ujumla. Uvumilivu wenye ushikamanifu kama huo unafanya moyo wa Yehova ushangilie!—Met. 27:11.

3 Kwa kuongezea, huduma yetu inatimiza pia fungu fulani katika utimizo wa kusudi la Mungu. Kuhusiana na uharibifu wa ulimwengu wa Shetani unaokuja, Yehova anasema: “Mataifa watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.” (Eze. 39:7) Ili mataifa wajue hilo, ni lazima kwamba watumishi wa Mungu waendelee kutangaza jina lake na kusudi lake “kwa kila taifa na kabila na lugha na watu.”—Ufu. 14:6, 7.

4 Msingi wa Hukumu: Kuhubiri habari njema ni pia msingi wa hukumu. Mtume Paulo alisema kwamba Kristo Yesu ataleta kisasi juu ya “wale wasiomjua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.” (2 The. 1:8, 9) Watu watahukumiwa kutokana na itikio lao kuelekea habari njema. Hilo linawatia watumishi wa Mungu chini ya daraka nzito kabisa. Ili kuepuka hatia ya damu, hatupaswi kujizuia kujulisha ujumbe wa Ufalme unaookoa uzima.—Mdo. 20:26, 27.

5 Jitihada zetu zenye kuendelea za kusaidia majirani zetu wapate kibali cha Mungu ni onyesho la rehema ya Yehova. (1 Tim. 2:3, 4) Tukijua kwamba maisha za watu ni zenye kubadilika kwa ukawaida, tunawaendea mara kwa mara na kuwahimiza wamtafute Yehova kukiwa bado na wakati. Kwa kufanya hivyo, tunaonyesha “huruma nyororo za Mungu wetu,” ambaye “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.”—Luka 1:78; 2 Pet. 3:9.

6 Tunafaidika Sisi Wenyewe: Kuwa wenye shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova kunatulinda. Kunatusaidia kuweka “karibu akilini kuwapo kwa siku ya Yehova” na kuepuka kutiwa unajisi na mfumo huu wa mambo. (2 Pet. 3:11-14; Tito 2:11, 12) Kwa hiyo, tuweni ‘imara, thabiti, sikuzote tukiwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana,’ tukijua kwamba jitihada zetu katika huduma ya Kikristo si za bure.—1 Kor. 15:58.

[Maulizo ya Funzo]

1. Yehova anaona huduma yetu namna gani, na itikio la wanadamu ni gani?

2. Huduma yetu inatuwezesha kuonyesha nini?

3. Kwa nini ni jambo la maana sana kwetu kuendelea kujulisha jina la Mungu na kusudi lake?

4. Kazi ya kuhubiri inakuwa namna gani msingi wa hukumu?

5. Rehema ya Mungu inaonyeshwa namna gani katika huduma yetu?

6. Namna gani kuwa wenye shughuli nyingi katika utumishi wa Yehova kunatufaidi?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine