Onyesha Kupendezwa Kibinafsi na Wengine —Kwa Kuwafikiria
1 “Yehova ni mwenye neema.” (Zab 145:8) Ijapokuwa Yehova ni Mwenye Enzi Kuu ya Ulimwengu Wote, yeye anatendea wanadamu wasiokamilika kwa fazili na kwa kuwafikiria. (Mwa. 13:14; 19:18-21, 29) Kwa kuwa wenye fazili na kufikiria wengine kama Mungu wetu, tunaweza kufanya utoaji wetu wa habari njema uwe wenye kuvutia watu. (Kol. 4:6) Kuwa na adabu na pia heshima tunapozungumza na watu hakutoshi.
2 Tunapohubiri Mlango kwa Mlango: Tunaweza kufanya nini ikiwa tunatembelea mtu wakati usiofaa au wakati ambapo ana kazi nyingi? Kufikiria hali kama hizo kutatusaidia tufanye utoaji wetu uwe mfupi sana au tumuulize mtu ikiwa tunaweza kurudia wakati mwingine. Tutaonyesha kwamba sisi ni wenye fazili ikiwa hatulazimishi watu wakubali vitabu vyetu. Kuwafikiria wengine kutatuchochea tuheshimu vitu vyao, kama vile kukumbuka kufunga mlango wa lupango tunapoondoka na pia kuwazoeza watoto wetu ili waweze kufanya hivyo. Tunapoacha kitabu au trakti wakati mtu hayupo nyumbani, tunapaswa kufanya angalisho kwamba kisionekane na wapita-njia. Bila shaka, kufikiria wengine kutatuchochea tuwatendee kama vile tungetaka watutendee.—Luka 6:31.
3 Tunapohubiri Barabarani: Tunapohubiri barabarani, tunaweza kuonyesha kwamba tunawafikiria wengine kwa kutowafungia njia watu wanaotembea kwa miguu na kutokufanya vikundi nafasi za biashara. Ni vizuri kufikiria hali za wengine, kwa kuzungumza na wale walio na wakati mchache wa kutusikiliza badala ya kuzungumza na wale wanaoonekana kuwa haraka. Nyakati nyingine, kwa sababu ya makelele ya barabarani huenda tukalazimika kusema kwa sauti ili watu tunaozungumza nao watusikie. Hata hivyo tunapaswa kufanya hivyo kwa heshima, bila kufanya watu waanze kutuangalia sisi.—Mt. 12:19.
4 Tunapotoa Ushahidi kwa Njia ya Telefone: Kuwafikiria wengine kutatuchochea kutoa ushahidi kwa njia ya telefone mahali pa kimya. Tunaonyesha adabu tunapojitambulisha mara moja na kumwelezea mtu wazi sababu gani tunamuita kwenye telefone. Kutumia telefone inavyofaa na kwa sauti yenye kutulia kutasaidia ili wengine washiriki katika mazungumzo ya Kimaandiko yenye kujenga. (1 Kor. 14:8, 9) Kwa kuwa wenye fazili na wenye kufikiria wengine katika njia hizo mbalimbali, tunamuiga Mungu wetu Yehova mwenye kufikiria wengine.