Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 7/06 uku. 1
  • Tumwige Yehova ‘Mungu Wetu Mwenye Furaha’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tumwige Yehova ‘Mungu Wetu Mwenye Furaha’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sisi twahubiri habari njema
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Kuna Habari Njema Ambayo Watu Wote Wanahitaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Furahia Kutangaza Habari Njema
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
Huduma Yetu ya Ufalme—2006
km 7/06 uku. 1

Tumwige Yehova ‘Mungu Wetu Mwenye Furaha’

1 Yehova anataka watu wawe wenye furaha kwelikweli. Neno lake Biblia linatutolea kwa uwingi matumaini ya baraka nzuri ajabu ambazo anatayarishia wanadamu. (Isa. 65:21-25) Inafaa wengine waone waziwazi kwamba tuna furaha tunapowatolea “habari njema yenye utukufu ya Mungu mwenye furaha.” (1 Tim. 1:11) Namna tunavyosema kuhusu habari ya Ufalme inapaswa kuonyesha kwamba tunapenda ile kweli na kwamba tunapendezwa kikweli na watu tunaowahubiria.—Rom. 1:14-16.

2 Ni kweli kwamba nyakati fulani inaweza kuwa vigumu kuendelea kuonyesha hali yenye furaha. Katika maeneo fulani, tunapata watu wachache wanaofurahia habari ya Ufalme. Siku nyingine tunakuwa wenye kupambana na hali ngumu maishani. Ili kulinda furaha yetu, tunapaswa kufikiria jinsi ni jambo la lazima sana kwamba watu wa eneo letu wasikie na waelewe habari njema ya Ufalme tunayohubiri. (Rom. 10:13, 14, 17) Kufikiri sana juu ya jambo hilo kutatusaidia tuendelee kwa furaha kujulisha mipango ya Yehova yenye huruma kwa ajili ya wokovu

3 Zungumzia Zaidi Mambo Mazuri Yanayokuja: Tunapaswa pia kuwa waangalifu kuhusu mambo tunayosema. Ijapokuwa tunaweza kuanza mazungumzo kwa kuonyesha tatizo fulani au habari kuhusu jambo fulani ambalo linasumbua watu akilini, tunapaswa kuepuka kuzungumzia sana mambo yenye kusikitisha watu. Daraka letu linahusu kupelekea watu “habari njema ya mambo mema.” (Isa. 52:7; Rom. 10:15) Habari njema hiyo ni habari inayotegemea ahadi za Mungu kuhusu maisha bora ya wakati ujao. (2 Pet. 3:13) Ukiwa na jambo hilo katika akili, tumia Maandiko ili “kufunga majeraha ya waliovunjika moyo.” (Isa. 61:1, 2) Hilo litasaidia kila mmoja wetu kuendelea kuwa mwenye furaha na mwenye kutazamia mambo mazuri.

4 Bila shaka, tunapofanya kazi ya kuhubiri watu, watatambua hali yetu ya furaha. Kwa hiyo, basi, kila siku tuonyeshe hali ya Yehova ‘Mungu wetu mwenye furaha,’ tunapohubiria watu habari njema za Ufalme katika eneo letu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine