Wahubiri Wapendwa wa Ufalme:
Tuna furaha ya kuwajulisha habari fulani kuhusu ujenzi wa nyumba tatu mpya za makao ya wanabetheli mjini Kinshasa. Kwa sasa sehemu kubwa ya kazi imekwisha kumalizika, sehemu za juu zenye kufunika nyumba hizo zimekwisha kuwekwa na kazi ya kumalizia sehemu za ndani inaendelea vizuri. Tunafurahi pia kuwajulisha kwamba katika mwezi wa 6, 2006 kazi nyingine ilianzishwa, yaani kuchimba msingi wa chumba kipya cha kulia chakula chenye nafasi 450 na chumba cha kupikia. Kazi yote inafanywa na shirika fulani la ujenzi. Kamati yetu ya Ujenzi ya Betheli ndio yenye kuongoza kazi na kuchunguza vizuri na kwa kawaida aina ya vifaa vinavyotumiwa. Kupitia kazi nzuri hiyo na maendeleo yanayofanywa katika ujenzi kwenye makao ya Betheli, tunaweza kuona kwamba Yehova amebariki mpanuko wa nyumba yake.
Zaidi ya hayo, tunapenda kuonyesha shukrani zetu kwa ajili ya msaada wenye upendo uliotolewa kwa maelfu ya ndugu na dada waliopatwa na vita na matokeo yake.—Yoh. 13:35.
Katika mwaka huu wa 2006, tumetolea makutaniko 845 msaada wa mavazi, hasa katika sehemu zilizopatwa na vita. Baraza Linaloongoza lilikubali tutume msaada ambao ndugu zetu wa Ulaya walituma, karibu tone 21 za mavazi na viatu. Katika miaka ya 2003/2004, tulifanya vivyo hivyo kwa ajili ya makutaniko yaliyo katika sehemu zingine za eneo letu.
Tunawaomba mwendelee kusali kwa ajili ya ndugu wote hao—wale wenye kupatwa na vita na wale wanaotoa msaada.—2 Kor. 1:11.
Ndugu zenu,
Ofisi ya Tawi ya Congo Kinshasa