Ni Mambo Gani Unayotia pa Nafasi ya Kwanza?
1 Ungejibu ulizo hilo namna gani? Kwa kweli, sisi wote tunataka kutia pa nafasi ya kwanza faida za Ufalme. (Mt. 6:33) Lakini tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, namna ninavyochagua mambo inaonyesha kwamba ninafanya hivyo?’ Biblia inatutia moyo ‘tuendelee [kujiangalia] sisi wenyewe jinsi tulivyo.’ (2 Kor. 13:5) Namna gani tunaweza kuonyesha kwamba tunatia Ufalme pa nafasi ya kwanza?
2 Jinsi Tunavyotumia Wakati Wetu: Kwanza tunaweza kuchunguza jinsi tunavyotumia wakati wetu. (Efe. 5:15, 16) Unatumia kiasi gani cha wakati kila juma katika kufurahia mazungumzo pamoja na marafiki, kuangalia televizyo, kutumia Internet au kufuatia mambo ya kujifurahisha? Tukiandika wakati tunaotumia kwa ajili ya mambo hayo na kuulinganisha na wakati tunaotumia kwa ajili ya mambo ya kiroho, labda tunaweza kushangaa. Je, tunatumika saa nyingi za ziada kazini (heures supplémentaires) ili kutosheleza tu tamaa yetu ya kupata vitu vingi vya kimwili bila kujali utumishi wetu mtakatifu? Je, mara nyingi tunakosa mikutano au kazi ya kuhubiri ili kujiburudisha miisho-juma?
3 Panga Mambo ya Kutia pa Nafasi ya Kwanza: Wengi wetu tunakosewa na wakati ili kufanya kila kitu ambacho tungependa kufanya. Kwa hiyo, ili kutanguliza faida za Ufalme, tunahitaji kufikiria mambo tunayotia pa nafasi ya kwanza na kisha kupanga wakati kwa ajili ya “mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10) Mambo hayo yanatia ndani kujifunza Neno la Mungu, kuhubiri, kutunza watu wa familia yako na kushiriki mikutano ya Kikristo. (Zab. 1:1, 2; Rom. 10:13, 14; 1 Tim. 5:8; Ebr. 10:24, 25) Utendaji mwingine kama vile kufanya mazoezi ya kimwili kwa kiasi na kujiburudisha kwa njia yenye kufaa, ni mambo yenye kuleta faida. (Marko 6:31; 1 Tim. 4:8) Lakini mambo hayo yasiyo ya maana sana yasituzuie kutia pa nafasi ya kwanza faida za Ufalme.
4 Ndugu mmoja kijana alitia pa nafasi ya kwanza faida za Ufame kwa kuanza utumishi wa wakati wote kuliko kufuatia masomo ya juu katika kusudi la kupata kazi ya kimwili. Alijifunza luga nyingine na akahama ili kutumikia mahali palipokuwa na lazima kubwa ya wahubiri wa Ufalme. Alisema: “Ninafurahia kabisa maisha huku. Utumishi unatia nguvu sana! Ningependa vijana wote wafanye jambo hilo na wapate kutosheka kama ninavyotosheka. Hakuna jambo linalopita kumtumikia Yehova kwa nafsi yote.” Ndiyo, kutia pa nafasi ya kwanza faida za Ufalme kunatuletea baraka, lakini jambo la maana sana ni kwamba kufanya hivyo kunamfurahisha Yehova, Baba yetu wa mbinguni.—Ebr. 6:10.