Tumia Wakati Wako kwa Hekima
1 Tamaa yetu ya kumpendeza Yehova inatuchochea kufanya maisha zetu zijae na utendaji wa kiroho. Neno lake linatuagiza ‘kuendelea kutafuta kwanza ufalme’ na ‘kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi.’ (Mt. 6:33; Flp. 1:10) Tunawezaje kununua wakati kwa ajili ya faida za Ufalme na kuweka utendaji mbalimbali usio wa lazima pa nafasi yao?—Efe. 5:15-17.
2 Tanguliza Utendaji wa Ufalme: Panga wakati wako ili usipotezwe katika mambo yasiyo ya lazima. Watu fulani wanaanza kila mwezi kwa kupangia wakati kamili kwenye kalenda zao kwa ajili ya huduma ya shambani. Kisha, wanakuwa waangalifu ili wasiruhusu mambo mengine kuingilia mipango hiyo. Jambo hilo linaweza pia kufanywa ili kununua wakati kwa ajili ya mikutano, funzo la kibinafsi, na mikusanyiko. Wengi wana programu ya kila siku inayoanza au kumalizika kwa usomaji wa Biblia. Tia pembeni wakati kamili kwa ajili ya kila utendaji wa maana, na usiache mambo mengine yasiyo ya lazima kuingilia programu hiyo.—Mhu. 3:1; 1 Kor. 14:40.
3 Punguza Matumizi ya Ulimwengu: Katika nchi fulani, ni vyepesi kuwa na michezo, viburudisho, mapumziko, shughuli za kujifurahisha, na ufuatiaji mwingine wa mambo mbalimbali. Wengi wanatumia wakati mwingi sana katika kutazama televisheni au wakitumia kompyuta. Hata hivyo, kushughulika sana na utendaji mbalimbali wenye kuburudisha na vifaa vya kisasa ambavyo ulimwengu huu unatoa kutaongoza bila shaka kwenye kuvunjika moyo. (1 Yoh. 2:15-17) Kwa sababu hiyo, Maandiko yanatuhimiza kutotumia ulimwengu kwa ukamili. (1 Kor. 7:31) Kwa kusikiliza shauri hilo nzuri, unaweza kuonyesha Yehova kwamba ibada yake inachukua nafasi ya kwanza katika maisha yako.—Mt. 6:19-21.
4 Wakati unaobaki kwa mfumo huu ni wenye kufikia mwisho. Wale wanaotanguliza faida za Ufalme watakuwa wenye furaha na watapata kibali cha Mungu. (Met. 8:32-35; Yak. 1:25) Kwa hiyo, na tufanye matumizi ya hekima ya mali hii yenye thamani, yaani wakati wetu.