Jinsi Ya Kununua Wakati Unaofaa
1 Tukiwa na mengi ya kufanya katika utumishi wa Yehova, sisi ni wenye kutumia vizuri wakati. (1 Kor. 15:58) Tunatambua ulazima wa kujifunza kibinafsi na katika familia, kusoma Biblia kila siku, kutayarisha mikutano na kuihudhuria, na pia kujitoa kabisa kikawaida katika mahubiri. Wangalizi wanatimiza daraka la wachungaji na wanashughulika na kazi nyingine kuhusu kutaniko. Wengine wana madaraka mazito ya kifamilia au mapaswa ya kila aina. Ni jambo la lazima kwamba kila mmoja wetu kuwa mwenye usawaziko na kupanga mambo vizuri ili kufikia kutimiza yote.
2 Tujiwekee Mambo ya Kufanya Kwanza: Imetupasa kuwa na utambuzi na uamuzi mzuri ikiwa tunataka kufaulu katika ‘kununua wenyewe wakati unaofaa.’ (Efe. 5:15, 16, NW) Tunapaswa kuhakikisha ni gani “mambo yaliyo ya maana zaidi” na kuyaweka nafasi ya kwanza kwenye orodha yetu ya mambo ya kufanya kwanza. (Flp. 1:10, NW) Wenzi wawili wa ndoa walieleza ya kwamba nyumba yao ni ya kitheokrasi kwa jinsi ifuatayo: “Tumejaza maisha yetu na ukweli . . . Ukweli si tu sehemu fulani ya maisha yetu, ni uhai wetu. Mengine yote yanayobaki yanaambatana nao.” Ni jambo la muhimu kwamba tutie ibada ya Yehova na utumishi Wake pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu.
3 Tutambue Kile Kinachotupotezea Wakati: Juma moja lina saa 168, na imetupasa kutumia kwa hekima wakati tulio nao. Ili kuwa na wakati wa kutosha kutumia kwa utendaji mbalimbali wa kitheokrasi, tunapaswa kutambua mambo yanayotupotezea wakati na kupunguza hesabu yayo. Kulingana na uchunguzi, mwamerika wa wastani anaangalia televisheni zaidi ya saa 30 kwa juma! Wengine wanapitisha wakati mwingi kusoma vitabu vinavyotolewa na ulimwengu. Wamoja wanaweza kuona kwamba wanapitisha wakati zaidi kuliko kawaida katika utendaji mbalimbali wa rika (kikundi), tafrija, vitumbuizo au mbele ya kompyuta. Labda imetupasa kuchunguza kwa makini matumizi yetu ya wakati ya kila siku ili kuona jinsi ya kutumia vizuri zaidi wakati wetu. Ikiwa tunatenda kwa hekima, tutapunguza wakati tunaotoa kwa utendaji mbalimbali wa ziada.
4 Tuwe na Matumizi Mazuri ya Wakati: Ijapo hali yetu iwe ni gani, tunapaswa sote kununua wakati ili kufikia miradi yetu ya kiroho. Wengine walitambua kwamba kwa kuanza kazi mapema kidogo kila siku, wangeweza kufanya mambo mengi zaidi. Ikiwa tunapitisha wakati mwingi tukiwa njiani kwenda kazini au kwa kungoja wengine, tunaweza kufaidika na wakati huo kwa kusoma Biblia, kutayarisha mikutano au kusikiliza kaseti mbalimbali ambazo Sosaiti inatuandalia. Ni jambo lenye faida sana kwa familia kujiwekea wakati kamili na kwa ukawaida ili kujifunza pamoja. Ikiwa washiriki wote wa familia ni wenye kuheshimu saa ya funzo la familia, kila mmoja atakuwa na wakati zaidi kwa ajili yake mwenyewe.
5 Kwa kadiri wakati unavyopita, tungepaswa kutambua zaidi na zaidi kwamba “wakati uliobaki umepunguzwa.” (1 Kor. 7:29, NW) Uhai wetu unategemea jinsi tunavyotumia wakati huo wenye thamani. Tutabarikiwa ikiwa tunanunua wakati ufaao katika kusudi la kuweka faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza.—Mt. 6:33.