Tujenge Maisha Yetu Juu Ya Utumishi Wa Yehova
1 Yesu alilinganisha wasikilizaji wake na aina mbili za wajenzi. Mmoja alijenga namna yake ya maisha juu ya mwamba wa utii kwa Kristo na aliweza kushindana na dhoruba ya upinzani na dhiki. Mwingine alijenga juu ya mchanga wa ukosefu wa utii wenye ubinafsi na hakuweza kusimama aliposongwa. (Mt. 7:24-27)[1] Kwa kuwa tunaishi katika umalizio wa mfumo wa mambo, tunapatwa na dhoruba nyingi za upinzani. Mbali kule mawingu [Meaning: the appearance of the dismal]meusi ya dhiki kubwa ni yenye kukusanyika kwa uharaka. Je! tutavumilia hadi mwisho tukilinda imani yetu salama [W intact 1]? (Mt. 24:3, 13, 21) Mengi yategemea jinsi tunavyojenga maisha yetu sasa. Hivyo, ni jambo la lazima tujiulize wenyewe, ‘Je! mimi ninajenga kwa uthabiti maisha yangu ya Kikristo juu ya utumishi wenye utii kwa Mungu?’
2 Inamaanisha nini kujenga maisha yetu juu ya utumishi wa Yehova? Inamaanisha kufanya Yehova awe wa kwanza kabisa katika maisha yetu. Hilo latia ndani kukaza fikira juu ya Ufalme tukiufanya kuwa jambo la kushughulikia zaidi. Hilo lataka utii kwa Mungu katika utendaji wetu wote wa maisha ya kila siku. Laomba kujitoa kwa moyo wote katika funzo letu la Biblia la binafsi, la familia na la pamoja na kutaniko, na katika utumishi wa shambani, tukifanya hayo yawe mambo yetu ya kutangulizwa. (Muh. 12:13; Mt. 6:33) Mwendo kama huo usiobadilika-badilika na wenye utii hutokeza imani thabiti kama mwamba ambayo haitaangamia tunapopambana na dhoruba yoyote ya upinzani iwezayo kutokea.
3 Ni furaha kuona mamilioni ya watu wakijenga kwa uthabiti maisha yao na matumaini yao ya wakati ujao juu ya utumishi wa Mungu, kama alivyofanya Yesu. (Yn. 4:34) Wanashikamana na programu isiyobadilika-badilika ya utendaji mbalimbali wa kitheokrasi na kufurahia baraka tele kama matokeo. Mama mmoja alifasiria jinsi yeye na mume wake walivyofaulu kuwalea watoto wao wawili kusudi wamtumikie Yehova: see end: ref.2 “Sisi tulijaza maisha yetu ukweli—kwenda kwenye mikusanyiko yote, kujitayarisha kwa ajili ya mikutano na kuihudhuria, na kufanya utumishi wa shambani uwe sehemu ya kawaida ya maisha yetu.” Mume wake aliongeza hivi: “Ukweli si sehemu ya maisha yetu, bali huo ndiyo maisha yetu. Kila jambo jinginelo lote linaendeshwa kwa kuutegemea huo.” Je! wewe pia umeweka utumishi wa Yehova kuwa jambo la kwanza kwanza kutanguliza katika familia yako?[2]
4 Tufanye Programu ya Juma Inayoweza Kutumika: Tengenezo la Yehova hutusaidia kufuata desturi nzuri ya mambo ya kiroho kwa kupanga mikutano mitano kwa juma. Wakristo wanaojenga maisha yao juu ya ibada ya Yehova hupanga kazi yao ya kimwili na mambo yao ya kifamilia ili wahudhurie mikutano hiyo yote ya maana sana. Hawaachi mambo ya maana ndogo yazuie hudhurio lao la kawaida.—Flp. 1:10; Ebr. 10:25.
5 Wakristo wenye kukomaa hutambua kwamba, kama lilivyo jambo la maana kula chakula pa nyakati fulani kila siku, ndivyo lilivyo jambo la maana sana kufanya programu halisi kwa ajili ya funzo la binafsi na la familia, kutia ndani kujitayarisha kwa ajili ya mikutano. (Mt. 4:4) Je! unaweza kuweka kando kipindi cha angalau dakika 15 au 20 kila siku kwa ajili ya funzo la binafsi? Ufumbuzi ni kutoacha mambo mengine yachukue [W encroach 1] wakati uliowekwa kando kwa ajili ya funzo. Fanya hilo liwe zoea lenye mafaa. Hilo laweza kuomba kuamka mapema kuliko unavyofanya kila asubuhi. Wale washiriki 17,000 wa familia ya Betheli ulimwenguni pote huamka mapema asubuhi ili kuzungumzia andiko la siku. Bila shaka, kuamka mapema kwaomba kupanga saa nzuri ya kulala usiku ili kuanza siku ifuatayo katika hali yenye kufaa na ukiwa mwenye kupumzika.
6 Ikiwa wewe ni kichwa cha familia, fanya hatua ya kwanza ili ufikirie na kupanga programu ya utendaji wa kitheokrasi ya familia yako. Familia nyinginezo husoma pamoja Biblia, Kitabu-Mwaka, au kichapo kinginecho kadiri wanavyojiburudisha baada ya mlo wa jioni. Wazazi wengi walioona watoto wao wakikomaa na kuwa Wakristo wenye nguvu kiroho husema kwamba jambo moja lililochangia kufanikiwa kwao lilikuwa lile zoea la familia la kuweka kando jioni moja kila juma kwa ajili ya kufurahia pamoja wakati wenye kujenga kiroho. Mama mmoja wa aina hiyo alisema: “Ninahisi kwamba maendeleo ya kiroho ya watoto wetu ilitokana kwa sehemu kubwa na funzo letu la kawaida la Siku ya Tatu usiku, lililoanzishwa miaka 30 iliyopita.” Watoto wake watatu wote walibatizwa wakiwa na umri mdogo, na baadaye wote watatu waliingia utumishi wa wakati wote. Zaidi ya funzo la familia, migawo kwenye mikutano au utoaji mbalimbali wa habari katika utumishi wa shambani vyaweza kurudiliwa, na utendaji mwingine mbalimbali wenye kujenga waweza kufanywa mkiwa pamoja.
7 Katika programu yako ya kila juma, je! ‘umenunua wakati’ kwa ajili ya kuhubiri Ufalme? (Kol. 4:5) Wengi wetu wanayo maisha yenye shughuli nyingi, wakiwa na madaraka ya kushughulikia katika familia na katika kutaniko. Tusipofanya mipango halisi ili kushiriki kila juma katika kazi ya kuhubiri na kufundisha, itakuwa rahisi sana kwa mambo mengine kumeza utendaji huo wa maana sana. Mwanamume mmoja aliyekuwa na uwanda wa kufugia wanyama alisema: “Karibu na 1944, nilitambua kwamba njia moja ambayo kwa hiyo ningaliingia utumishi ilikuwa kupanga siku fulani kwa ajili ya huo. Mpaka leo ningali nikichukua siku moja katika juma kwa ajili ya utumishi.” Mzee mmoja Mkristo atambua kwamba kuwa na programu halisi kwa ajili ya kutoa ushahidi kwafanya iwezekane kwake kupitisha kwa wastani saa 15 katika kazi ya kuhubiri kila mwezi. Ikiwa anayo mambo ya kimwili ya kufanya Siku ya Posho, yeye anayapanga baada ya utumishi wake wa shambani wa asubuhi. Je! wewe na familia yako mwaweza kupanga angalau siku moja kila juma kwa ajili ya utumishi, mkifanya hilo liwe sehemu ya namna yenu ya maisha ya kiroho?—Flp. 3:16.
8 Tuchunguze [examine] Kawaida ya Kila Siku ya Maisha Yetu: Kuna mambo yanayotuzuia tusijenge maisha yetu juu ya utumishi wa Yehova. Matukio yasiyotazamiwa yanaweza kuvuruga programu yetu iliyopangwa kwa makini ya funzo, mikutano, na utumishi. Na adui yetu, Shetani, atafanya yote awezayo ili ‘akatize pito letu’ na kuzuia mipango yetu. (1 Thes. 2:18; Efe. 6:12, 13) Usiache vizuizi hivyo vikuvunje moyo, hivi kwamba ukate tamaa. Fanya marekebisho yoyote yanayohitajiwa ili kutimiza utendaji wako wa kitheokrasi uliopangwa. Kuazimia na kudumu ni vya lazima ili kutimiza yale ambayo ni yenye kustahili kwelikweli.
9 Hatupaswi kuacha mavutano ya ulimwengu na ushawishi mbaya wa mwili wetu wenye dhambi viingize utendaji mbalimbali usio wa kiroho ambao ungeanza kula zaidi na zaidi wakati na uangalifu wetu. Kujichunguza binafsi kwa kutumia maulizo yafuatayo ni kwa lazima: ‘Je! mwendo wa maisha yangu umekuwa usiosawazika au usio na shabaha? Je! nimeanza kujenga maisha yangu juu ya mambo ya ulimwengu huu unaopita? (1 Yn. 2:15-17) Ni kiasi gani cha wakati ninachopitisha katika vifuatio vya binafsi, safari za kujifurahisha, utendaji wa michezo, au tafrija nyingine—kutia ndani wakati unaopitishwa kwa kuangalia televisheni au kusoma habari kwenye Interneti [Translator: For expression, see g97 7/22 p. 6 par. 9.]—kwa kulinganisha na wakati unaopitishwa katika utendaji wa kiroho?’
10 Ikiwa unaona kwamba maisha yako yamekuwa yenye kulemewa na utendaji zaidi na zaidi usio wa lazima, ni jambo gani unalopaswa kufanya? Kama Paulo alivyosali kwamba ndugu zake waweze “kurekebishwa,” au “kuletwa kwenye mstari wenye kufaa,” kwa nini usimsihi Yehova akusaidie uwe tena mwenye kukaza fikira juu ya utumishi wake? (2 Kor. 13:9, 11, kielezi-chini) Kisha, uwe mwenye kuazimia kuishi kulingana na azimio lako na ufanye marekebisho yanayohitajiwa. (1 Kor. 9:26, 27) Yehova atakusaidia uepuke kugeukia upande wa kuume au wa kushoto wa utumishi wenye utii kwake.—Linganisha Isaya 30:20, 21.
11 Tubaki Wenye Shughuli Katika Utumishi Wenye Shangwe wa Mungu: Mamilioni hutafuta furaha kwa vyo vyote, kisha hutambua kwamba, kadiri mwisho wa maisha unavyokaribia, vitu vya kimwili walivyovitafuta kwa hamu havikuwaletea furaha ya kudumu. Imekuwa “kujilisha upepo.” (Muh. 2:11, UV) Kwa upande mwingine, tunapofanya maisha yetu yategemee Yehova, ‘tukimweka yeye mbele yetu daima,’ tunapata uradhi wenye kina kirefu. (Zab. 16:8, 11) Mambo ni hivyo kwa maana Yehova ndiye sababu ya kuishi kwetu. (Ufu. 4:11) Bila yeye, Mkusudiaji Mkuu, uhai hauna maana. Kumtumikia Yehova hujaza maisha yetu utendaji wenye kufaa, wenye kusudi ambao hunufaisha wengine na sisi wenyewe kwa namna yenye kudumu, ndiyo, kwa namna yenye kudumu milele.
12 Ni jambo la maana kutokuwa wenye kula raha na kupoteza wazo la uharaka kuhusiana na mwisho wa ulimwengu wa Shetani unaokaribia sana. Maoni yetu ya wakati ujao huwa na uvutano juu ya maisha yetu ya kila siku. Watu wa siku za Noa ambao hawakuamini kwamba kungekuwako gharika ya ulimwenguni pote, “hawakujali” kwa kuwa walifanya maisha yao ya kila siku yategemee vifuatio vyao binafsi—kula, kunywa, na kuoa—hadi gharika ilipokuja “kuwafagilia mbali wote.” (Mt. 24:37-39) Leo, wale wanaofanya maisha yao yategemee ulimwengu huu wataona matazamio yao ya wakati ujao yakisambaratika mbele yao katika uharibifu mkubwa zaidi ambao haujampata mwanadamu wakati mwingine wowote, “siku ya Yehova.”—2 Pet. 3:10-12.
13 Kwa hiyo, endeleeni kujenga maisha yenu juu ya Mungu aliye hai, Yehova, na juu ya kufanya mapenzi yake. Hakuna akiba nyingine uwezayo kujirundikia katika maisha haya iliyo na Mtegemezaji wa aina hiyo mwenye kutumainiwa kama Yehova. Hawezi kusema uwongo—atatimiza ahadi zake. (Tito 1:2) Hawezi kufa—hakuna kitu kinachowekwa kwa Yehova kitakachopotea. (Hab. 1:12; 2 Tim. 1:12) Maisha ya utii na imani tunayojenga sasa ni mwanzo tu wa maisha yatakayodumu milele katika utumishi wenye shangwe wa Mungu wetu mwenye furaha!—1 Tim. 1:11; 6:19.
[Caption on page 3]
“Ukweli si sehemu
ya maisha yetu, bali huo ndiyo maisha yetu.
Kila jambo linginelo lolote linaendeshwa kwa kuutegemea huo.”