Fanyeni Programu ya Familia Yenye Kufaa
1 Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu alihimiza wasikilizaji wake hivi: “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.” (Mt. 6:33) Njia yenye kufaa ya kupanga shughuli za familia hivi kwamba mambo ya kiroho yatangulizwe ni kuwa na programu iliyoandikwa. Chukueni dakika chache ili kujifanyia programu yenu ya familia ya kila juma, mkitumia programu iliyo wazi kwenye ukurasa wa 6 wa nyongeza hii. Kama mradi wa familia, wengine wanaweza kufanya karatasi ndogo ndogo zilizo na programu zao na kuzibandika juu ya programu hiyo iliyo wazi. Wengine pia wanaweza kuandika tu shughuli zao katika programu hiyo.
2 Programu ya kielelezo inayoonyeshwa hapo chini inaweza kusaidia mnapofanya programu yenu. Mtatambua kwamba inatia ndani shughuli za msingi nne tu: (1) hudhurio kwenye mikutano ya kutaniko, (2) utumishi wa shambani pamoja na familia, (3) funzo la familia, na (4) kuchunguza andiko la siku. Kutia ndani shughuli hizo katika programu yenu kunaweza kuwasaidia ili “mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10) Mapendekezo zaidi kuhusu sehemu hizo nne yanapatikana kwenye kurasa 4-5.
3 Programu ya familia yenu haifanyizwi tu na shughuli hizo nne. Ikiwa mnajitayarisha kwa ajili ya mikutano fulani mkiwa familia, andikeni hilo kwenye programu yenu. Ikiwa mnasoma pamoja sehemu ya Biblia baada ya kuchunguza andiko la siku au mnafanya hivyo wakati mwingine, onyesheni hilo kwenye programu. Ikiwa kwa kawaida mnashiriki katika pindi za kujiburudisha mkiwa familia mnaweza kutaka kutia ndani jambo hilo katika programu yenu.
4 Pangeni programu yenu ya familia ili kuipatanisha na mahitaji na hali za watu wote wa nyumbani. Pindi kwa pindi, kadirieni jinsi inavyotumika, na fanyeni marekebisho kadiri inavyohitajiwa.
[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 3]
Kielelezo cha Programu ya Familia
Asubuhi Kisha Mchana-Kati Jioni
Siku ya Yen. Andiko la Siku
Hotuba ya
Watu Wote
na Funzo
la Mnara
wa Mlinzi
Siku ya Kwa. Andiko la Siku Funzo la
Familia
Siku ya Pil. Andiko la Siku Funzo la
Kitabu la
Kutaniko
Siku ya Tat. Andiko la Siku
Siku ya Nne Andiko la Siku Shule ya
Huduma ya
Kitheokrasi
na Mkutano
wa Utumishi
Siku ya Tan. Andiko la Siku
Siku ya Pos. Andiko la Siku
Utumishi wa
Shambani
Pamoja na Familia
(Siku ya Magazeti)
[Picture on page 6]
Programu ya Familia
Asubuhi Kisha Mchana-Kati Jioni
Siku ya Yen.
Siku ya Kwa.
Siku ya Pil.
Siku ya Tat.
Siku ya Nne
Siku ya Tan.
Siku ya Pos.
................................................
Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko
la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku
Hotuba Shule Funzo la Funzo la Utumi- Uso- Kujibu-
ya Watu ya Kitabu Familia shi wa maji rudisha
Wote na Huduma la Kuta- Sha- wa Katika
Funzo la ya niko mbani Biblia Familia
Mnara wa Kithe- pamoja Katika
Mlinzi okrasi na Fa- Familia
na Mku- milia
tano wa
Utumishi