Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 5/05 uku. 3-6
  • Fanyeni Programu ya Familia Yenye Kufaa

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Fanyeni Programu ya Familia Yenye Kufaa
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Programu ya Familia—Andiko la Siku
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Tujenge Maisha Yetu Juu Ya Utumishi Wa Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Jinsi Washiriki wa Familia Wanavyofanya Kazi Pamoja ili Kushiriki Kikamili—Katika Funzo la Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Usijizuie Kuanzisha Funzo kwa Sababu Una Kazi Nyingi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2005
km 5/05 uku. 3-6

Fanyeni Programu ya Familia Yenye Kufaa

1 Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu alihimiza wasikilizaji wake hivi: “Basi, endeleeni kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.” (Mt. 6:33) Njia yenye kufaa ya kupanga shughuli za familia hivi kwamba mambo ya kiroho yatangulizwe ni kuwa na programu iliyoandikwa. Chukueni dakika chache ili kujifanyia programu yenu ya familia ya kila juma, mkitumia programu iliyo wazi kwenye ukurasa wa 6 wa nyongeza hii. Kama mradi wa familia, wengine wanaweza kufanya karatasi ndogo ndogo zilizo na programu zao na kuzibandika juu ya programu hiyo iliyo wazi. Wengine pia wanaweza kuandika tu shughuli zao katika programu hiyo.

2 Programu ya kielelezo inayoonyeshwa hapo chini inaweza kusaidia mnapofanya programu yenu. Mtatambua kwamba inatia ndani shughuli za msingi nne tu: (1) hudhurio kwenye mikutano ya kutaniko, (2) utumishi wa shambani pamoja na familia, (3) funzo la familia, na (4) kuchunguza andiko la siku. Kutia ndani shughuli hizo katika programu yenu kunaweza kuwasaidia ili “mhakikishe mambo yaliyo ya maana zaidi.” (Flp. 1:10) Mapendekezo zaidi kuhusu sehemu hizo nne yanapatikana kwenye kurasa 4-5.

3 Programu ya familia yenu haifanyizwi tu na shughuli hizo nne. Ikiwa mnajitayarisha kwa ajili ya mikutano fulani mkiwa familia, andikeni hilo kwenye programu yenu. Ikiwa mnasoma pamoja sehemu ya Biblia baada ya kuchunguza andiko la siku au mnafanya hivyo wakati mwingine, onyesheni hilo kwenye programu. Ikiwa kwa kawaida mnashiriki katika pindi za kujiburudisha mkiwa familia mnaweza kutaka kutia ndani jambo hilo katika programu yenu.

4 Pangeni programu yenu ya familia ili kuipatanisha na mahitaji na hali za watu wote wa nyumbani. Pindi kwa pindi, kadirieni jinsi inavyotumika, na fanyeni marekebisho kadiri inavyohitajiwa.

[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 3]

Kielelezo cha Programu ya Familia

Asubuhi Kisha Mchana-Kati Jioni

Siku ya Yen. Andiko la Siku

Hotuba ya

Watu Wote

na Funzo

la Mnara

wa Mlinzi

Siku ya Kwa. Andiko la Siku Funzo la

Familia

Siku ya Pil. Andiko la Siku Funzo la

Kitabu la

Kutaniko

Siku ya Tat. Andiko la Siku

Siku ya Nne Andiko la Siku Shule ya

Huduma ya

Kitheokrasi

na Mkutano

wa Utumishi

Siku ya Tan. Andiko la Siku

Siku ya Pos. Andiko la Siku

Utumishi wa

Shambani

Pamoja na Familia

(Siku ya Magazeti)

[Picture on page 6]

Programu ya Familia

Asubuhi Kisha Mchana-Kati Jioni

Siku ya Yen.

Siku ya Kwa.

Siku ya Pil.

Siku ya Tat.

Siku ya Nne

Siku ya Tan.

Siku ya Pos.

................................................

Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko Andiko

la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku la Siku

Hotuba Shule Funzo la Funzo la Utumi- Uso- Kujibu-

ya Watu ya Kitabu Familia shi wa maji rudisha

Wote na Huduma la Kuta- Sha- wa Katika

Funzo la ya niko mbani Biblia Familia

Mnara wa Kithe- pamoja Katika

Mlinzi okrasi na Fa- Familia

na Mku- milia

tano wa

Utumishi

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine