Programu ya Familia—Andiko la Siku
1 Wazazi wenye upendo wanafanya jitihada nyingi kila siku ili kuwatolea watoto wao chakula kizuri. Kuwatolea chakula cha kiroho kutoka Neno la Mungu ni jambo la maana hata zaidi. (Mt. 4:4) Njia moja ambayo katika hiyo mnaweza kusaidia watoto wenu kusitawisha hamu ya chakula cha kiroho na ‘kukua kufikia wokovu’ ni kuchukua wakati kila siku ili kuchunguza andiko la siku na maelezo mkiwa familia. (1 Pet. 2:2) Ni wakati gani mnapoweza kutia uchunguzi huo katika programu yenu ya familia?
2 Wakati wa Chakula: Kuanza siku na mazungumzo ya andiko kunaweza kusaidia familia yenu kulinda Yehova akilini siku mzima. (Zab. 16:8) Mama mmoja alikusudia kusoma na kuzungumzia andiko na maelezo pamoja na mwana wake wakati huyo alipokuwa akila chakula cha asubuhi na kusali pamoja naye kabla ya kwenda shuleni. Hilo lilimtia nguvu ili kuchukua msimamo imara alipopambana na jaribu la utukuzo wa taifa, kupinga vishawishi vya ukosefu wa adili, na kutoa ushahidi wenye ujasiri kwa wanafunzi na walimu pia. Ingawa alikuwa Shahidi pekee kwenye shule hiyo, hakujisikia kamwe akiwa peke yake.
3 Ikiwa si jambo lenye kufaa kuzungumzia andiko asubuhi, mnaweza kulichunguza baadaye mchana mkiwa familia, labda wakati wa chakula cha jioni. Wakati huo wengine pia wanazungumzia mambo yaliyoonwa kutoka katika huduma ya shambani na mambo waliyofurahia kutoka usomaji wao wa Biblia. Wengi wanakumbuka kwa upendo kwamba pindi hizo walipokuwa wakila chakula cha jioni ni kati ya nyakati zenye furaha zaidi walizopitisha pamoja wakiwa familia.
4 Usiku: Kwa familia zingine, wakati ulio bora zaidi wa kuchunguza andiko la siku ni kabla tu ya kulala. Huo unaweza pia kuwa wakati bora wa kusali pamoja. Watoto wenu wanaposikia kila siku mkisema kuhusu Yehova na kumwomba katika sala, yeye anakuwa mtu halisi kwao.
5 Yehova na abariki jitihada zenu katika kufundisha watoto wenu kweli mnapotumia vizuri broshua Kuyachunguza Maandiko Kila Siku.