Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 11/02 uku. 5-6
  • Vichwa vya Familia—Dumisheni Kawaida Nzuri ya Kiroho

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichwa vya Familia—Dumisheni Kawaida Nzuri ya Kiroho
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Msaada kwa Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Jinsi Washiriki wa Familia Wanavyofanya Kazi Pamoja ili Kushiriki Kikamili—Katika Funzo la Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Unaendelea Kumutumikia Yehova?
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2017
  • Endelea Kuwa na Mazoezi Mazuri, Utapata Baraka Nyingi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 11/02 uku. 5-6

Vichwa vya Familia—Dumisheni Kawaida Nzuri ya Kiroho

1 Ijapokuwa aliishi kwa makumi ya miaka miongoni mwa ibada ya sanamu na ufisadi wa Babuloni, Danieli alijulikana kwa kumtumikia Yehova “daima.” (Dan. 6:16, 20) Alidumishaje hali yake ya kiroho? Simulizi la Biblia linaonyesha kwamba alikuwa na kawaida yenye utaratibu ili kutimiza utendaji uliohusiana na ibada ya kweli. Kwa mfano, alikuwa na desturi ya kusali mara tatu kila siku katika chumba chake cha paa. (Dan. 6:10) Bila shaka, alikuwa pia na utaratibu kuhusu utendaji mwengine wa kiroho, kama vile kusoma Sheria. Hivyo, alipokabili jaribu lenye kuhatarisha uhai, Danieli alikuwa imara katika ujitoaji wake kwa Yehova, naye aliokolewa kimuujiza.—Dan. 6:4-22.

2 Vivyohivyo leo, tunapaswa kujitahidi sana ‘kufuliza kuwa macho kwa udumifu.’ (Efe. 6:18) Ulimwengu tunamoishi “unakaa katika nguvu ya mwovu.” (1 Yh. 5:19) Upinzani au majaribu yanaweza kutokea kwa ghafula na kutia imani yetu katika jaribu. Wakati wa dhiki kubwa, watumishi wa Mungu watakuwa lengo la shambulizi kali la Gogu wa Magogu, ambalo litaonekana kuwa vigumu kuponyoka. Jambo hilo litaomba tumaini kamili katika Yehova.—Ezek. 38:14-16.

3 “Jambo moja la maana ni kufanya usomaji wa Biblia wa familia wenye matokeo, funzo, na mazungumzo njia ya maisha.” Ndivyo ulivyoanza utangulizi wa drama kwenye kusanyiko la wilaya la 1998 yenye kichwa ‘Familia—Fanyeni Usomaji wa Biblia kwa Ukawaida Kuwa Njia Yenu ya Maisha!’ Utangulizi huo uliendelea kusema: ‘Familia zinapofuata mpango kama huo kikawaida na katika njia inayofanya Biblia kuwa hai, kawaida hii yenye kuongozwa Kibiblia inaweza kuwa na uvutano mkubwa sana kwa familia. Inaongeza ujuzi wetu. Inatia nguvu imani yetu. Na inatuandalia mifano ya watu wa kuiga—wanaume na wanawake wa zamani wenye imani kabisa—wanaoweza kutupulizia nguvu, itakayotusukuma tusimame imara kwa ajili ya kweli.’ Tunapochunguza sehemu mbalimbali za mpango mzuri wa kawaida wa kiroho, vichwa vya familia wanapaswa kutafuta njia moja au mbili ili kuboresha programu ya kiroho ya familia yao.

4 Chunguza Neno la Mungu Kila Siku: “Ufalme wa Mungu utakapotawala bila upinzani na mapenzi yake kutendeka kama ilivyo katika mbingu, pia juu ya dunia, hakuna wanadamu wakatili—wala hata wanyama wakali—‘watakaodhuru wala kuharibu.’ (Isa. 11:9; Mt. 6:9, 10)” Maneno hayo yalipatikana katika Kuyachunguza Maandiko Kila Siku—2001 katika maelezo ya andiko la siku kwa ajili ya Septemba 11. Kikumbusha hicho kilikuwa chenye kutia moyo kama nini! Ukiwa kichwa cha familia, je, unayo desturi ya kuchunguza andiko la Biblia kila siku na kutoa maelezo pamoja na familia yako? Jambo hilo ni lenye faida sana. Ikiwa haiwezekani kuwa pamoja asubuhi, huenda mnaweza kufanya hivyo jioni. Baba mmoja alisema: “Mlo wa jioni umekuwa wakati mzuri kwetu sisi kuzungumzia andiko la Biblia la kila siku.”

5 Ikiwa mna kawaida ya kuchunguza andiko la siku mkiwa familia, mnastahili pongezi. Huenda mnaweza kufaidika zaidi kwa kusoma sehemu moja ya Biblia wakati uleule. Watu fulani wana desturi ya kusoma sura nzima ambayo kutoka kwayo andiko la siku lilichukuliwa. Wengine wanafanya usomaji mfululizo, wakifanya hivyo hatua kwa hatua kupitia kitabu cha Biblia kilichochaguliwa. Usomaji wa Biblia wa kila siku utasaidia familia yako ikuze woga unaofaa wa kutomchukiza Yehova na itaongeza tamaa yao ya kufanya mapenzi yake.—Kumb. 17:18-20.

6 Programu yako ya usomaji wa Biblia wa familia na kuchunguza maandiko kila siku itakuwa na faida hata zaidi ikiwa unaweza kuchukua dakika chache kuzungumzia thamani ya matumizi ya habari. Kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 35, kinatoa madokezo haya: “Ili kupata faida kutokana na kusoma huku, . . . tumia wakati utafakari juu ya wazo linaloelezwa, namna linavyopatana na sura nyingine na namna linavyohusu wewe mwenyewe.” Unaweza kuuliza maswali kama haya: Jinsi gani jambo hili linatutolea mwongozo? Tunawezaje kutumia mistari hii katika huduma? Yanafunua nini kuhusu Yehova na njia yake ya kufanya mambo, na jinsi gani hilo linaongeza uthamini wetu kwake? Mazungumzo ya kiroho kama hayo yatasaidia wote katika nyumba ‘waendelee kufahamu mapenzi ya Yehova ni nini.’—Efe. 5:17.

7 Funzo la Familia: Kuongoza funzo la familia kwa njia yenye kudumu kila juma ni njia nzuri kwa vichwa vya familia ya kuonyesha watoto wao kwamba mambo ya kiroho yanatangulia kwanza. Mwanamume kijana moja anakumbuka: “Nyakati nyingine baba angekuwa amechoka sana kwa sababu ya kazi hivi kwamba ilikuwa vigumu aepuke kusinzia lakini hata hivyo funzo lilifanywa, na jambo hilo lilitusaidia sisi tuthamini uzito walo.” Watoto pia wanaweza kutimiza fungu lao ili kufanya mpango huo uwe na mafanikio. Familia moja ya watoto tisa iliamka kikawaida saa kumi na moja kamili kwa ajili ya funzo lao la familia kwani haikuwezekana wafanye funzo hilo wakati mwingine.

8 Ili funzo la familia liwe lenye matokeo, kichwa cha familia anapaswa ‘daima kukaza uangalifu kwake mwenyewe na kwa kufundisha kwake.’ (1 Tim. 4:16) Kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 38, kinasema: “Habari yote inayofaa mahitaji ya jamaa inaweza kutumiwa kama msingi wa funzo.” Jiulize: Jinsi gani washiriki wa familia yangu wanasonga mbele kiroho? Ninapokuwa katika huduma ya shambani pamoja na watoto wangu, je, wanajisikia kuwa huru wakijitambulisha kwa wenzao kama Mashahidi wa Yehova? Je, wanafurahia programu yetu ya usomi na funzo la Biblia la familia? Je, wanafanya kweli njia ya Yehova kuwa njia yao ya maisha? Uchunguzi wa makini utaonyesha unalohitaji, kama kichwa cha familia, kufanya ili kusimamisha na kujenga sifa za kiroho katika kila mshiriki wa familia.

9 Mikutano ya Kutaniko: Kutayarisha na kushiriki mikutano ya kutaniko kunapaswa kuwa sehemu yenye maana ya kawaida yenu ya kila juma. (Ebr. 10:24, 25) Mara kwa mara, mnaweza kujitayarisha kwa ajili ya sehemu ya mikutano fulani mkiwa familia. Kuliko kungojea mpaka dakika ya mwisho, je, mnaweza kufanya mpango ili kutayarisha vizuri kimbele? Mpango wa kawaida wenye utaratibu katika njia hii utaboresha ubora wa matayarisho yenu na faida mtakayopata kutokana na mikutano.—Mez. 21:5.

10 Ubora na kutobadilika-badilika ni alama ya mpango wa kawaida wa kiroho wenye matokeo. Ni vipi, ikiwa hali zinafanya iwe vigumu kwenu kutayarisha mikutano yote? Kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 34 kinatoa madokezo haya: “Usipange kujifunza habari nyingi zaidi ya unavyoweza ama utaona funzo lako kuwa halina maana na halithawabishi.” Epuka mitego ya kupitia kwa uharaka habari ili kuimaliza tu, au vibaya zaidi, kutojifunza yoyote ya habari kwani hauwezi kuimaliza yote. Badala ya hayo, amua ni kiasi gani cha habari mnaweza kujifunza, na mjifunje hicho vizuri. Fanyeni hivyo kila juma. Halafu, mjitahidi kupanua programu yenu ya funzo kutia ndani mikutano mingine.”

11 Familia zinapofika kwenye mikutano mapema, hilo linawasaidia kuwa katika hali inayofaa kiakili ili kumsifu Yehova na kufaidika na mafundisho anayoandaa. Je, familia yako ina desturi hiyo? Inaomba mpangilio mzuri na ushirikiano wa kila mmoja katika nyumba. Ikiwa mara nyingi unatambua kwamba familia yako inafanya mambo harakaharaka na kuwa katika hali ya mkazo kwenye mikutano jioni, je, mabadiliko yanaweza kufanywa katika kawaida yenu? Je, kuna mambo yanayoweza kufanywa kimbele? Ikiwa mshiriki mmoja wa familia analemewa na kazi nyingi ya kufanya, je, wengine wangeweza kusaidia? Je, ingepunguza mkazo ikiwa kila mmoja alikuwa tayari kuondoka dakika chache mapema kuelekea kwenye mikutano? Kupanga mambo vizuri kunachangia kuendeleza amani ya kiroho katika familia na katika kutaniko.—1 Kor. 14:33, 40.

12 Utumishi wa Shambani: Kuweka wakati kamili kwa ajili ya kushiriki katika huduma ni sehemu ingine ya kawaida nzuri ya kiroho. Kijana mmoja anayeitwa Jayson anakumbuka: “Familia yetu ilishiriki utumishi wa shambani kila Jumamosi asubuhi. Jambo hilo lilinisaidia kwa kuwa kadiri nilivyoshiriki katika huduma, ndivyo nilivyozidi kuona manufaa yake na kuifurahia zaidi.” Wengi waliolelewa katika nyumba za Mashahidi wametambua pia kwamba kuwa na wakati uliotiwa kikamili kwa ajili ya huduma kila juma kuliwasaidia kusonga mbele wakiwa wahudumu Wakristo.

13 Mpango wa kawaida wenye utaratibu unaweza kusaidia pia kufanya wakati ambao familia yako inatumia katika shamba kuwa wenye kufurahisha zaidi na wenye kuzaa matunda zaidi. Jambo hilo linaweza kutimizwaje? Mnara wa Mlinzi wa Julai 1, 1999, ukurasa wa 21, unatoa pendekezo hili: “Je, wewe mara kwa mara hutumia wakati wa funzo la familia ili kusaidia washiriki wa jamaa yako wajitayarishe kwa ajili ya utumishi wa shambani? Kufanya hivyo kwaweza kuwa na manufaa makubwa. (2 Timotheo 2:15) Kwaweza kusaidia kufanya utumishi wao uwe wenye maana na wenye matokeo. Mara kwa mara, huenda ukatenga kipindi chote cha funzo kwa ajili ya kujitayarisha huko. Huenda ukashughulikia mara nyingi zaidi sehemu za huduma ya shambani katika mazungumzo mafupi-mafupi mwishoni mwa kila funzo la familia au wakati mwingineo katika juma.” Je, familia yako imejaribu hilo?

14  Endeleeni Kusonga Mbele: Kutokana na uchunguzi huu, je, umetambua sehemu ambazo katika hizo familia yako inafanya vema? Uwapongeze, na ujitahidi kuboresha sehemu hizo. Ikiwa unaona sehemu nyingi ambazo zinahitaji kuboreshwa, chagua sehemu moja au mbili za kushughulikia kwanza. Zitakapokuwa sehemu ya kawaida yenu ya kiroho, shughulikia nyingine moja au mbili. Uwe mwenye kutazamia mema na mwenye kukubali sababu. (Flp. 4:4, 5) Kuweka kawaida nzuri ya kiroho kwa ajili ya nyumba yako inachukua jitihada nyingi, lakini jitihada hiyo inastahili, kwani Yehova anatuhakikishia: “Naye anayetengeneza mwenendo wake, nitamwonyesha wokovu wa Mungu.”—Zab. 50:23.  

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine