Endelea Kuwa na Mazoezi Mazuri, Utapata Baraka Nyingi
1 Wakati ulipokubali kuwa Mkristo, labda wakati huo ulijikaza kuwa na programu nzuri inayohusiana na utumishi wako kwa Mungu, programu kama vile funzo la Biblia, mikutano, mahubiri, na sala. Kwa kufanya hivyo, Yehova alibariki bidii yako kwa kuwa wewe ni mwenye kuendelea katika urafiki wako pamoja naye. Labda kumepita miaka mingi sasa tangu ubatiziwe. Je, unaendelea kulinda mazoezi yako mazuri ya kiroho kama wakati huo ulipokubali kuwa Mkristo?
2 Chunguza Programu Yako: Je, una zoezi la kusoma sehemu fulani ya Neno la Mungu kila siku? Tutapata faida nyingi kabisa tunapofanya hivyo. (Yos. 1:8; Zab. 1:2, 3) Zamani katika Israeli, kila mfalme alipaswa kusoma “siku zote za maisha yake” nakala (kopi) ya kitabu cha Sheria alichokuwa nacho. Wafalme hao walibarikiwa namna gani kwa kufanya hivyo? Mfalme angekuwa na roho ya unyenyekevu na angejifunza kumwogopa Yehova ili asiende pembeni ya amri Zake. (Kumb. 17:18-20) Hivyohivyo leo, kusoma Biblia kila siku kunatusaidia kuwa bila kosa na kuwa pasipo laumu katika ulimwengu huu mwovu. Usomaji huo unatusaidia pia tuwe na vifaa vyote vinavyostahili kwa ajili ya kazi ya kuhubiri.—Flp. 2:15; 2 Tim. 3:17.
3 Yesu alizoea kwenda kwenye sinagogi, mahali ambapo Maandiko yalizungumziwa. (Luka 4:16) Bila shaka, jambo hilo lilimtia nguvu ili kupambana na majaribu ambayo alipata. Sisi pia tunatiwa nguvu na mafundisho ya Mungu tunayopokea kupitia mikutano ya kutaniko na “ubadilishanaji wa kitia-moyo” unaofaa. (Rom. 1:12) Kukusanyika pamoja na ndugu zetu kunatusaidia tuvumilie magumu ya siku hizi za mwisho. (Ebr. 10:24, 25) Je, ungali bado na zoezi la kuhuzuria mikutano yote?
4 Biblia inatuelezea kwamba mitume waliendelea kuhubiri habari njema “kila siku na nyumba kwa nyumba.” (Mdo. 5:42) Kwa kuwa hatuwezi kuhubiri kila siku, je, tunaweza kufanya liwe zoezi letu kushiriki katika aina fulani ya mahubiri kila juma? Tukifanya hivyo, bila shaka tutakuwa na ufundi wa kutumia Neno la Mungu, na labda tutapata vitia moyo vyenye kufurahisha tunapoelezea wengine kweli za Biblia.
5 Nabii Danieli alibarikiwa sana kwa kuwa alimtumikia Yehova “kwa ukawaida” maishani mwake. Alikuwa pia na zoezi la kusali Yehova kwa ukawaida. (Dan. 6:10, 16, 20) Kama Danieli, tunaposali Yehova kwa ukawadia kutoka moyoni, atatubariki kwa kutupatia roho takatifu yake. (Luka 11:9-13) Zaidi ya hilo, Yehova atachukua hatua ya kutukaribia sana, akitutolea nafasi ya kufurahia urafiki wa karibu pamoja naye. (Zab. 25:14; Yak. 4:8) Ni baraka kubwa kabisa! Kwa hiyo, tufanye nguvu ili kulinda mazoezi yetu mazuri kuhusiana na utumishi wetu kwa Mungu na kupata hivyo baraka nyingi kutoka kwa Yehova.
[Maulizo ya Funzo]
1. Kwa nini kuchunguza programu yako inayohusiana na utumishi wako kwa Mungu kutakuletea faida nyingi?
2. Namna gani tunafaidika kutokana na usomaji wa Biblia wa kila siku?
3. Tunapohuzuria mikutano kwa ukawaida tunapata faida gani?
4. Kuhubiri kila juma kunatuletea faida namna gani?
5. Kwa nini ni jambo la maana kusali Yehova kikawaida?