Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/00 uku. 3-4
  • Je, wewe ni mwenye kujipatia faida?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, wewe ni mwenye kujipatia faida?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mikutano Yenye Inatuchocheaka Katika “Upendo na Matendo ya Muzuri”
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Kukusanyika Pamoja kwa Ajili ya Ibada
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
  • Mikutano hufaidi vijana
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Kufaidika Kabisa na Mikutano kwa Ajili ya Mahubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2000
km 8/00 uku. 3-4

Je, wewe ni mwenye kujipatia faida?

1 Mamilioni ya watu leo wanataka kujua jinsi ya kushinda matatizo na kupata maisha yenye furaha. Wanafurahia kwa pupa vitabu vyenye mwongozo wa kujisaidia au wanaendea vikundi au matengenezo ili kupata shauri juu ya jinsi ya kufanya maisha yao yawe bora. Labda wengine wanaweza kusema juu ya faida chache ambazo wamepata. Lakini, tunapoamua mambo kwa kuangalia hali ya maisha leo, je, watu kwa ujumla wamejifunza kufurahia maisha yenye amani, na yenye kutosheleza kwa kina kirefu kupitia programu za kibinadamu za kutoa elimu? Sivyo bila shaka!—1 Kor. 3:18-20.

2 Kwa upande mwingine, Muumba wetu anatoa bila malipo elimu yenye kusaidia zaidi kwa wote watakaosikiliza. Yehova anataka kila mmoja afaidike na mafundisho yake. Yeye ametoa kwa ukarimu Neno lake lililoongozwa na roho yake ili kuongoza wanadamu katika unyofu, naye amefanya habari njema ya Ufalme wake itangazwe katika dunia yote. (Zab. 19:7, 8; Mt. 24:14; 2 Tim. 3:16) Maisha yenye furaha kwelikweli yanahusiana moja kwa moja na kusikiliza amri za Yehova.—Isa. 48:17, 18.

3 Mwongozo wa Yehova ni wa juu zaidi sana kuliko ule unaotolewa na vitabu vyovyote vyenye mwongozo wa kujisaidia au mipango yoyote ya kusaidia mtu afanye hali yake mwenyewe kuwa bora, vitabu na mipango inayotolewa na ulimwengu huu. Tunaweza kupata msaada wa kweli na faida zenye kudumu ikiwa tunafaidika kikamili na maandalizi ya Yehova kama vile yanavyoonyeshwa katika Neno lake na kufundishwa na tengenezo lake.—1 Pet. 3:10-12.

4 Jipatie faida kwenye mikutano ya kutaniko: Leo, Yehova anaonyesha kwamba anapendezwa nasi kwa kweli kwa kutufundisha njia zake, nasi tunafaidika kwa kusikiliza maagizo yake. Mikutano yetu mitano ya kila juma inaonyesha kwamba Yehova anatujali kwa upendo. Wakati tunapohudhuria mikutano ya kutaniko, ujuzi wetu juu ya Mungu huongezeka. Tunajifunza jinsi ya kujilinda kutokana na lililo baya kwa kumkaribia Yehova. Katika njia hiyo, roho zetu huinuliwa.

5 Kuna mengi kuliko hayo. Kwenye mikutano ya kutaniko tuna uwezo wa ‘kupanuka.’ (2 Kor. 6:13) Hilo linahusisha kupata kujua wengine katika kutaniko. Tunafaidika na badilishano la kitia-moyo, kama lile ambalo kuhusu hilo mtume Paulo aliandika katika barua yake kwa Waroma. (Rom. 1:11, 12) Alipokuwa akiandikia Waebrania, yeye alionya kwa nguvu wale ambao huenda walikuwa wakisitawisha zoea la kuachilia mbali ushirika wa Kikristo.—Ebr. 10:24, 25.

6 Kutosheka kwenye furaha katika maisha kunahusiana moja kwa moja na kupendezwa na hali njema ya wengine. Tunatiwa moyo kutafuta njia za kuchangia katika furaha ya wengine. Kwa hiyo, mikutano yetu ya Kikristo bila shaka ni kwa ajili ya faida yetu binafsi na kwa ajili ya faida ya wale tunaoshirikiana nao kwa njia yenye kufaa. Kile tunachoombwa ni kule kushiriki kwetu kwa moyo wote.

7 Mtume Paulo alisema juu ya jambo hilohilo katika shauri lake kwa Timotheo wakati alipoandika: “Uwe ukijizoeza mwenyewe ujitoaji-kimungu ukiwa shabaha yako.” (1 Tim. 4:7) Tunaweza kujiuliza: ‘Je, mimi ni mwenye kujizoeza mwenyewe? Je, ninajifunza kufaidika na yale ninayosikia kwenye mikutano ya kutaniko?’ Majibu yetu yatakuwa ndiyo ikiwa sisi ni waangalifu kwa yale tunayosikia kwenye mikutano na kujitahidi kutumikisha yale tunayojifunza. Kupitia macho ya imani, tunapaswa kuwa na uwezo wa kuona zaidi ya ndugu wanaofundisha na kuona Yehova kuwa ndiye Mwalimu Mkuu wa watu wake.—Isa. 30:20.

8 Shule ya huduma ya Kitheokrasi na mkutano wa utumishi: Shabaha ya mikutano hiyo miwili ni kutusaidia kuwa wenye matokeo katika huduma ya Kikristo. Hilo ndilo kusudi kabisa la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi—shule iliyo na wanafunzi ambao hupokea maagizo na shauri kwa ukawaida. Unayo nafasi ya kuonyesha maendeleo yako ukiwa msemaji wa peupe na mwalimu wa Neno la Mungu. Lakini ili kufaidika zaidi kutokana na shule hiyo, unapaswa kujiandikisha, kuhudhuria, kushiriki kikawaida, na kuchukua migawo yako kwa uzito. Kukubali na kutumikisha shauri linalotolewa kutakusaidia kufanya maendeleo.

9 Mkutano wa Utumishi unatufundisha umaana wa huduma ya Kikristo na unatuonyesha jinsi tunavyoweza kushiriki katika kazi ya kufanya wanafunzi. Je, wewe na familia yako mnafaidika kikamili na yale yanayotolewa kwenye mikutano hiyo miwili? Mume na mke Wakristo wenye kuoana wanasema: “Kwenye Mkutano mmoja wa Utumishi, tulisikia kwamba tunapaswa kuchunguza andiko la siku tukiwa familia. Sisi hatukuwa tukifanya jambo hilo, lakini sasa tunalifanya.” Namna gani wamejipatia faida? Wanasema: “Tunatambua kwamba mazungumzo yetu tunapozunguka meza ya chakula ni yenye kufurahisha zaidi. Hakuna tena mabishano wakati wa chakula cha mchana.” Je, hata watoto wadogo wanafaidika na mikutano? Ndiyo. Mama anasema: “Ni wazi kwamba mikutano ina uvutano sana juu ya watoto wetu. Juma moja hasa tulikuta mwana wetu mwenye umri wa miaka sita akisema uwongo. Lakini kwenye mkutano juma hilo, hotuba ya maagizo ilihusu kusema uwongo. Akionyesha kwenye sura yake alama yenye hatia zaidi, mwana wetu alimwangalia baba yake na kujikunja katika kiti chake. Alipata somo, nasi hatukuwa na tatizo lolote baada ya hapo.”

10 Dada mmoja painia anasema kwamba yeye ni mwenye furaha kuona kwamba madokezo kwa ajili ya kufanya huduma yetu iwe bora yanatolewa kwenye Mkutano wa Utumishi. Kwa nini? Anaeleza: “Nimekuwa nikifikiri kwa namna isiyoweza kuruhusu maendeleo. Nyakati nyingine ninafikiri kwamba yale yanayopendekezwa katika Huduma Yetu ya Ufalme hayatatumika. Lakini kwenye Mkutano wa Utumishi, ninaposikia kwamba tunapaswa kuyajaribu, ninajaa shauku ya kutumikisha madokezo hayo. Inafanya huduma iwe yenye kusisimua!” Baada ya majuma mengi akitumikisha dokezo la kujaribu kuanzisha funzo la Biblia wakati wa ziara ya kwanza, yeye alianzisha funzo kwenye ziara ya kwanza pamoja na msichana ambaye mbele ya hapo alikuwa akisali ili apate msaada.

11 Wakati unaposikia hotuba yenye kutia ndani shauri la Biblia kuhusu maamuzi ya kibinafsi unayofanya, je, unasikia moyoni kwamba Yehova ni mwenye kusema nawe moja kwa moja? Ndugu mmoja alijisikia hivyo moyoni. Alisema: “Hivi juzijuzi kwenye mkutano mmoja, kulikuwa hotuba ambayo ndani yake ndugu alizungumzia aina za viburudisho zilizokuwa zenye kufaa kwa Wakristo na zile ambazo hazikuwa zenye kufaa. Nilikuwa na zoea la kupenda kuangalia mchezo wa ngumi kwenye televisheni. Lakini baada ya mkutano huo, niliamua kwamba mchezo huo ulikuwa katika ile aina ya kiburudisho ambayo haingekuwa yenye kufaa kwa Wakristo. Kwa hiyo siuangalii tena kamwe.” Ndiyo, ingawa ndugu huyo alikuwa amesitawisha kupenda sana kitu ambacho ni chenye jeuri, yeye aliitikia kwa unyenyekevu uongozi wa Yehova.—Zab. 11:5.

12 Mkutano wa watu wote, funzo la Mnara wa Mlinzi, na funzo la kitabu la kutaniko: Hotuba za watu wote tunazosikia kila juma zinazungumzia habari mbalimbali za Biblia. Ni nini unalopata kutokana na hotuba hizo? Mume mmoja Mkristo alitoa maelezo kuhusu faida alizokuwa amepata: “Hotuba moja ya watu wote ilikazia yale matunda yote ya roho. Msemaji alisema kwamba, ili kujitahidi kukuza matunda hayo, yeye binafsi alichagua sifa moja hasa na kujitahidi kuikomaza muda wa juma moja. Mwishoni mwa juma, alitafakari jinsi alivyofanya ili kuonyesha tunda hilo katika utendaji wake mbalimbali wa kila siku. Kisha alijitahidi kukomaza sifa nyingine muda wa juma lenye kufuata. Nilifurahia wazo hilo, nami nikaanza kufanya hivyo mimi mwenyewe.” Ni matumizi mazuri kama nini ya yale aliyojifunza!

13 Funzo la Mnara wa Mlinzi linatufundisha kutumikisha kanuni za Biblia katika hali mbalimbali za maisha. Hilo linatusaidia kudumisha akili na mioyo yenye kutulia ijapokuwa mahangaiko ya maisha. Funzo la Mnara wa Mlinzi hutufanya pia tutembee sambamba na kweli yenye kuendelea. Kwa mfano, je, hatukufaidika na makala za funzo la Mnara wa Mlinzi wa Mei 1, 1999, makala zenye vichwa: “Mambo Haya Lazima Yatukie,” “Mwacheni Msomaji Atumie Ufahamu,” na “Kesheni na Mwe na Bidii Yenye Kuendelea!” Mafunzo hayo yalikuwa na uvutano gani juu yako binafsi? Je, unaonyesha kupitia matendo yako kwamba onyo la Yesu kuhusu wakati ujao lina matokeo juu yako? Je, wewe ni mwenye kujitayarisha kwa ajili ya majaribu yaliyo huko mbele wakati tunapoona “kitu chenye kuchukiza sana ambacho husababisha ukiwa . . . kikiwa kimesimama katika mahali patakatifu”? (Mt. 24:15-22) Je, miradi na mwendo wako wa maisha vinaonyesha kwamba jambo la maana zaidi kwako si kurundika vitu vya kimwili lakini utakaso wa jina la Yehova? Kwenye Funzo la Mnara wa Mlinzi, je, hatujifunzi kujipatia faida sasa?

14 Fikiri juu ya yale mambo mengi tunayojifunza kwenye Funzo la Kitabu la Kutaniko kila juma. Sasa tunajifunza kitabu cha Biblia cha Danieli. Muda wa ile miezi minne ambayo katika hiyo tumekuwa tukijifunza kitabu hicho cha Biblia, je, hatukuona imani yetu ikikomaa kila juma? Kama vile Danieli, nabii mpendwa wa Yehova, tunatia nguvu imani yetu kusudi tuweze kuvumilia.

15 Yehova anatufundisha kuishi kwa furaha: Tunaepuka maumivu mengi ya moyoni wakati tunaposikiliza amri za Mungu. Zaidi ya hayo, tunaishi maisha yenye furaha kwelikweli. Kwa kufuata uongozi wa Yehova, tunakuwa washiriki katika kazi yake, si watazamaji tu. Na wale wanaofanya kazi ya Mungu ni watu wenye furaha.—1 Kor. 3:9; Yak. 1:25.

16 Kwenye mikutano ya kutaniko, tenda kwa kufikiria jinsi utakavyotumikisha mambo unayosikia kwenye mikutano ya kutaniko. (Yn. 13:17) Mtumikie Mungu kwa shauku na kwa moyo wako wote. Furaha yako itakuwa kubwa sana. Maisha yako yatakuwa yenye kutajirika na yenye maana zaidi. Ndiyo, utakuwa mwenye kujipatia faida.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine