SURA YA 7
Mikutano Yenye Inatuchocheaka Katika “Upendo na Matendo ya Muzuri”
TANGU zamani, watu wa Yehova wanakusanyikaka mu njia yenye kupangwa muzuri. Zamani, mu Israeli, wanaume wote walipaswa kuenda Yerusalemu juu ya kufanya sikukuu kubwa tatu. (Kum. 16:16) Mu siku za mitume, mara mingi Wakristo walikuwa nakusanyika kwa ukawaida mu nyumba ya mutu fulani. (Flm. 1, 2) Na leo, juu tuko watumishi wa Mungu tuko nafurahia mikutano na mikusanyiko yetu mikubwa. Juu ya nini watumishi wa Mungu wanakusanyikaka? Kwanza ni juu kukusanyika ni sehemu ya maana sana ya ibada yetu.—Zb. 95:6; Kol. 3:16.
2 Pia, ile mikutano inaleteaka faida sana wale wenye wanaihuzuria. Juu ya Sikukuu ya Vibanda ya kila mwaka wa saba, Waisraeli waliambiwa hivi: “Kusanya watu pamoja, wanaume, wanamuke, watoto, na mukaaji wako mugeni mwenye kuwa katika miji yako, ili wasikilize na kujifunza juu ya Yehova Mungu wenu na kumuogopa na kuwa waangalifu kutimiza maneno yote ya Sheria hii.” (Kum. 31:12) Ni wazi kwamba, sababu ya maana yenye inatuchochea kukusanyika ni ili ‘tufundishwe na Yehova.’ (Isa. 54:13) Pia kukusanyika kunatusaidia tujuane, tutiane moyo, na tupate nguvu kutoka kwa wengine.
MIKUTANO YA KUTANIKO
3 Wanafunzi wenye walikusanyika kisha Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y., walisikiliza kwa uangalifu mafundisho ya mitume, “na kila siku waliendelea kuwa katika hekalu wakiwa na kusudi moja.” (Mdo. 2:42, 46) Kisha, wakati Wakristo walikusanyika kwa ajili ya ibada, walisoma maandiko yenye iliongozwa na roho ya Mungu, walisoma pia mabarua yenye iliandikwa na mitume na wanafunzi wengine Wakristo. (1 Ko. 1:1, 2; Kol. 4:16; 1 Te. 1:1; Yak. 1:1) Pia, ile wakati kutaniko yote ilikuwa nasali kwa Mungu. (Mdo. 4:24-29; 20:36) Wakati fulani, wamisionere walizungumuzia mambo yenye walikutana nayo mu kazi ya kuhubiri. (Mdo. 11:5-18; 14:27, 28) Tena, ku ile mikutano, walikuwa najifunza mafundisho ya Biblia na kuchunguza utimizo wa unabii mbalimbali wenye uliandikwa kwa musaada wa roho ya Mungu. Walipewa mashauri juu ya mwenendo wenye Wakristo wanapaswa kuwa nao na kuhusu kujitoa kwa Mungu. Wote walitiwa moyo kuhubiri habari njema kwa bidii.—Ro. 10:9, 10; 1 Ko. 11:23-26; 15:58; Efe. 5:1-33.
Tuko na lazima ya kukusanyika kwa ukawaida ili tutiane moyo mu hizi siku za mwisho
4 Leo, mikutano ya Kikristo inafanywa sawa vile ilikuwa inafanywa wakati wa mitume. Tunatii kabisa shauri yenye iliongozwa na roho ya Mungu, yenye kuwa mu Waebrania 10:24, 25. Ile shauri inasema hivi: “Na tufikiriane . . . , bila kuacha kukutana pamoja, kama vile wengine wako na desturi, lakini tutiane moyo, na kufanya vile zaidi sana kwa kadiri munaona siku ile kuwa inakaribia.” Tuko naishi mu hizi siku za mwisho zenye kuwa ngumu. Tunapaswa kukusanyika kwa ukawaida ili tuendelee kuwa nguvu kiroho, kuwa washikamanifu kwa Yehova na kutiana moyo. (Ro. 1:11, 12) Siye Wakristo, tuko naishi katikati ya kizazi yenye kupotoka. Tunakatala kabisa mambo yenye kuonyesha kwamba hatumuogope Mungu na tunakatala kabisa tamaa za ulimwengu. (Flp. 2:15, 16; Tit. 2:12-14) Kwa hiyo basi, unawaza kuko fasi ingine kwenye tunaweza kupata marafiki wazuri kuliko kuwa pamoya na watu wa Yehova ku mikutano? (Zb. 84:10) Na unawaza kuko jambo ingine inaweza kutuletea faida zaidi kuliko kujifunza na kuzungumuza juu ya Neno ya Mungu? Kwa hiyo, acha sasa tuchunguze mikutano mbalimbali yenye ilishapangwa kwa faida yetu.
MUKUTANO YA MWISHO YA JUMA
5 Mukutano ya mwisho ya juma inaanzaka na hotuba yenye kutegemea Biblia. Ile hotuba inafanywa zaidi sana kwa ajili ya watu wote, kutia ndani wale wenye pengine njo mara yao ya kwanza kukusanyika. Ni hotuba yenye inasaidiaka kabisa wapya na wahubiri wengine mu kutaniko.—Mdo. 18:4; 19:9, 10.
6 Yesu Kristo, mitume wake, na wengine wenye walijiunga nao, walikuwa nafanya mikutano kwa ajili ya watu wote sawa vile watu wa Yehova wanafanyaka leo. Bila shaka, Yesu alikuwa musemaji mukubwa zaidi kuliko wasemaji wote hapa ku dunia. Watu walisema hivi juu yake: “Hakuna mutu mwenye amekwisha kusema kama mutu huyu.” (Yoh. 7:46) Yesu alifundisha kwa mamlaka, na watu walikuwa wanashangaa sana. (Mt. 7:28, 29) Watu wenye walitii kwa moyo wote mafundisho yake walipata faida mingi. (Mt. 13:16, 17) Mitume walifuata mufano wa Yesu. Mu andiko ya Matendo 2:14-36, muko hotuba moto-moto yenye Petro alitoa siku ya Pentekoste ya mwaka wa 33 K.K.Y. Watu wengi sana wenye walisikiliza ile hotuba, waliguswa moyo na kuanza kutenda kulingana na mambo yenye walisikia. Kisha wakati fulani, mutume Paulo alitoa hotuba ya muzuri kule Atene. Ile hotuba nayo ilifanya watu wengi wakuwe waamini.—Mdo. 17:22-34.
7 Vilevile leo, watu wengi sana wanapataka faida wakati wanahuzuria mikutano kwa ajili ya watu wote na wakati wanasikiliza hotuba zenye kutolewa ku mikusanyiko yetu mikubwa. Zile hotuba zinatusaidia tuendelee kujua muzuri mafundisho ya Kikristo na tuendelee kuwa na bidii mu kazi ya Ufalme. Wakati tunawaalika wale wenye kupendezwa, na pia watu wengine, tunaweza kusaidia sana watu wengi wajue mafundisho ya musingi ya Biblia.
8 Mu hotuba ya watu wote munazungumuziwaka habari mbalimbali. Kwa mufano, habari juu ya mafundisho na unabii wa Biblia, kanuni za Maandiko na mashauri juu ya maisha ya familia, mambo ya ndoa, magumu mbalimbali yenye vijana wanapambanaka nayo, na mwenendo muzuri wenye Mukristo anapaswa kuwa nao. Hotuba zingine zinazungumuzia kazi za uumbaji za Yehova zenye kupendeza sana. Zingine zinazungumuzia mifano ya imani, bidii, na uaminifu wa watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia, na kukazia masomo yenye ile mifano inaweza kutufundisha.
9 Juu hotuba za watu wote zituletee faida, ni lazima tusikilize kwa uangalifu, tufungule Biblia wakati musemaji anatuomba tufanye vile, na kufuatana naye wakati iko nasoma na kufasiria maandiko fulani. (Lu. 8:18) Kwa hiyo, wakati tunaelewa muzuri mafundisho, tutapenda kuifuata na kuitumikisha mu maisha yetu.—1 Te. 5:21.
10 Kama kuko wasemaji, bila shaka hotuba ya watu wote itatolewa kila juma. Juu ya kufanya vile, mara mingi wasemaji wenye kuwa mu makutaniko ya karibu wanaalikwa. Kama hakuna wasemaji wa kutosha, hotuba zitatolewa kila mara wakati inawezekana.
11 Sehemu ya pili ya mukutano ya mwisho ya juma ni Funzo ya Munara wa Mulinzi, ni kusema tunazungumuzia kwa njia ya maulizo na majibu habari fulani yenye kuchapishwa mu gazeti ya funzo ya Munara wa Mulinzi. Yehova anatupatiaka chakula ya kiroho kwa wakati yenye kufaa kupitia Munara wa Mulinzi.
12 Mara mingi, habari za kujifunza zinaonyesha namna tunaweza kutumikisha kanuni zenye kuwa mu Biblia mu maisha yetu ya kila siku. Zile habari zinapatia Wakristo nguvu ya kuepuka “roho ya ulimwengu” na kuepuka mwenendo mubaya. (1 Ko. 2:12) Habari za kujifunza zenye kuwa mu Munara wa Mulinzi zinatupatiaka mafasirio ya mupya juu ya mafundisho na unabii yenye kuwa mu Biblia. Ile inatusaidia kutembea hatua kwa hatua na ile kweli na kuendelea kutembea mu njia ya wenye haki. (Zb. 97:11; Mez. 4:18) Kukusanyika na kutoa maelezo wakati ya Funzo ya Munara wa Mulinzi, kunaweza kutusaidia tufurahie tumaini yenye tuko nayo ya dunia mupya yenye haki yenye Yehova alishatuahidi. (Ro. 12:12; 2 Pe. 3:13) Kukusanyika na ndugu na dada kunatusaidia tuendelee kuonyesha tunda ya roho na tukuwe na tamaa zaidi ya kumutumikia Yehova kwa bidii. (Gal. 5:22, 23) Mikutano inatupatia nguvu ya kuvumilia majaribu na kujenga “musingi muzuri kwa ajili ya wakati wenye kuja” ili ‘tushike sana uzima wa kwelikweli.’—1 Ti. 6:19; 1 Pe. 1:6, 7.
13 Tunaweza kufanya nini ili ile mupango kuhusu chakula ya kiroho ituletee faida? Kila mutu anapaswa kutayarisha mbele ya wakati habari ya kujifunza. Unaweza kuitayarisha weye peke, lakini mwenye kuwa na familia ni muzuri afanye vile pamoya na familia yake. Chunguza maandiko yenye kupatikana mu ile habari. Wakati ya mukutano, toa maelezo mu maneno yako kuliko kusoma vile inaandikwa. Ile itafanya ile kweli iingie kabisa mu moyo wako, na maelezo yako yenye kuonyesha imani itasaidia wengine. Ni muzuri pia tukuwe nasikiliza kwa uangalifu maelezo ya wengine. Tukifanya vile, habari yenye tutajifunza kila juma itatusaidia kabisa.
MUKUTANO YA KATIKATI YA JUMA
14 Kila juma kutaniko inakutanaka ku Jumba ya Ufalme juu ya kufuata programu yenye inaitwa Utumishi na Maisha ya Mukristo. Ile mukutano iko na sehemu tatu zenye ziko na kusudi ya kutusaidia “tustahili kabisa” kuwa watumishi wa Mungu. (2 Ko. 3:5, 6) Programu na habari kwa ajili ya ile mukutano vinatolewaka kila mwezi mu Buku ya Mukutano—Utumishi na Maisha ya Mukristo. Mu ile buku muko pia namna mbalimbali za kuanzisha mazungumuzo zenye zinatumiwa mu mahubiri.
15 Sehemu ya kwanza ya ile mukutano inaitwa: Utajiri wa Neno ya Mungu. Ile sehemu inatusaidia kujua hali na tabia za watu wenye kuzungumuziwa mu Biblia, na mambo yenye mifano yao inaweza kutufundisha mu maisha yetu. Muko hotuba, usomaji wa Biblia, na mazungumuzo yenye kutegemea usomaji wa Biblia wa kila juma. Mambo sawa vile picha na karte, na kurasa za mazoezi ili kusaidia kufundisha zile habari inapatikana mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha. Kujifunza vile Biblia kwa undani na kuchunguza kwa uangalifu ile mambo yote, kunatusaidia mu maisha yetu na mu kazi yetu ya kuhubiri na ya kufundisha ili ‘tukuwe na uwezo kamili, na vifaa kamili kwa ajili ya kila kazi njema.’—2 Ti. 3:16, 17.
16 Sehemu ya pili ya ile mukutano inaitwa: Tujitoe Kabisa mu Kazi ya Kuhubiri. Iko na kusudi ya kusaidia kila mutu ajizoeze na kukomalisha ufundi wake mu kazi ya kuhubiri na kufundisha. Muko pia migawo ya wanafunzi na video mbalimbali juu ya namna ya kuanzisha mazungumuzo. Hii sehemu ya mukutano inatusaidia tukuwe na “ulimi wa wale wenye kufundishwa” ili ‘tujue namna ya kumujibu mwenye kuchoka kupitia neno yenye kufaa.’—Isa. 50:4.
17 Sehemu ya tatu inaitwa: Maisha ya Mukristo. Inafasiria namna ya kutumikisha kanuni mbalimbali zenye kuwa mu Biblia mu maisha yetu ya kila siku. (Zb. 119:105) Kitu ya maana ya hii sehemu ya mukutano ni Funzo ya Biblia ya Kutaniko. Ni funzo yenye inaongozwaka sawa vile Funzo ya Munara wa Mulinzi, ni kusema kwa njia ya maulizo na majibu.
18 Kila mwezi wakati Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha inafika, muratibu wa baraza ya wazee ao ndugu mwingine mwenye kumusaidia, ataichunguza kwa uangalifu sana na kufanya programu, ni kusema kupatia ndugu migawo. Kila juma, muzee fulani mwenye kuwa na uwezo wa kufundisha muzuri na mwenye kukubaliwa na baraza ya wazee, anasimamia mukutano. Kazi yake inatia ndani kuhakikisha kwamba mukutano inaanza na kumalizika kwa wakati. Tena iko na kazi ya kupongeza na kushauria wanafunzi wenye wanapitisha vipindi.
19 Kukusanyika kwa ukawaida na kutoa maelezo ku mukutano Utumishi na Maisha kunatusaidiaka sana. Tunajua maandiko muzuri, tunaelewa kanuni za Biblia, tunahubiri habari njema bila kuogopa na tunakuwa na ufundi mu kazi ya kufanya wanafunzi. Watu wenye bado hawayabatizwa lakini wako nakusanyika, wanapataka pia faida kwa kuona sifa za kiroho za ndugu na dada na kwa kusikiliza mazungumuzo yenye kujenga. Vifaa sawa vile Watchtower Library, JW Library®, Watchtower MAKTABA KU ENTERNETE (kama inapatikana mu luga yenu), vinatusaidiaka kutayarisha muzuri ile mukutano na mikutano ingine. Maktaba yenye kuwa mu Jumba ya Ufalme inaweza kutusaidia pia. Mu ile maktaba munakuwaka vichapo vya Mashahidi wa Yehova, kama vile Index des Publications des Témoins de Jéhovah ao kitabu Musaada wa Kutafuta Habari kwa Ajili ya Mashahidi wa Yehova, na pia tafsiri mbalimbali za Biblia, konkordanse, diksionere na vichapo vingine vya kutusaidia kutafuta habari. Kila mutu anaweza kutumia ile maktaba mbele ao kisha mikutano.
MIKUTANO KWA AJILI YA MAHUBIRI
20 Wakati mbalimbali mu juma na Siku ya Posho ao Siku ya Yenga, vikundi vya wahubiri vinakutanaka kwa wakati mufupi ili kufanya mukutano kwa ajili ya mahubiri. Mara mingi mikutano ya vile inafanyiwaka mu manyumba ya ndugu na dada ao fasi ingine yenye kufaa. Inaweza kufanyiwa pia mu Jumba ya Ufalme. Kufanya mikutano ya vikundi vidogo-vidogo mu fasi mbalimbali mu eneo, inaweza kufanya ikuwe mwepesi kwa wahubiri kufika ku mukutano kwa ajili ya mahubiri na hata kuhubiri mu eneo. Bila kuchelewa, mwenye kuongoza ile mukutano atapanga wahubiri, na kisha palepale wanaenda mu eneo. Mwangalizi wa kikundi anaweza pia kuhangaikia kwa uangalifu kila muhubiri wa mu kikundi yake. Kuko faida mingi kama kila kikundi iko nafanyia mukutano kwa ajili ya mahubiri fasi yake. Lakini wakati fulani kunaweza kuwa hali fulani zenye zinaweza kufanya ikuwe lazima vikundi mbalimbali vikusanyike pamoya juu ya kufanya ile mukutano. Kwa mufano, kama ni wahubiri kidogo tu njo wanakuwaka wanahubiri katikati ya juma, ni muzuri kutia vikundi vya wahubiri pamoya ao kuwakusanya wote ku Jumba ya Ufalme ao fasi ingine yenye kufaa. Ile itasaidia kila muhubiri apate mutu wa kuhubiri naye. Tena, kutaniko inaweza kuona kama ni muzuri mukutano kwa ajili ya mahubiri ifanyiwe ku Jumba ya Ufalme wakati ya sikukuu mbalimbali zenye watu wanazoea kufanya. Ao inaweza kuamuliwa kama kutaniko yote ifanye ile mukutano kisha Funzo ya Munara wa Mulinzi.
21 Kama kila kikundi iko nafanyia mukutano kwa ajili ya mahubiri fasi yake, ni mwangalizi wa kikundi njo ataiongoza. Wakati fulani, mwangalizi wa kikundi anaweza kuomba musaidizi wake ao ndugu mwingine mwenye kustahili aongoze ile mukutano. Ndugu mwenye kuongoza anapaswa kutayarisha habari fulani yenye kufaa na yenye itasaidia mu kazi ya kuhubiri. Kisha kupanga namna mahubiri itafanywa, ndugu moya atatoa sala, kisha wahubiri wataenda mu eneo bila kukawia. Ile mukutano inafanywa kwa dakika 5 ao 7, lakini inapaswa kufupishwa zaidi kama inafanywa kisha mukutano ingine ya kutaniko. Ile mukutano inapaswa kuwa yenye kutia moyo, yenye kuwa na maagizo ya muzuri na miongozo ya muzuri kwa wale wenye wataenda mu mahubiri. Wahubiri wapya na wengine wenye kuwa na lazima ya musaada wanaweza kutumika na wahubiri wenye kuwa na uzoefu ili wapate mazoezi.
MIPANGO YA MIKUTANO KWA AJILI YA MAKUTANIKO YA MUPYA AO YA KIDOGO
22 Juu watu wengi wanaendelea kuwa wanafunzi wa Yesu, hesabu ya makutaniko iko naongezeka. Kwa kawaida, mwangalizi wa muzunguko njo anajazaka ombi ili kutaniko ya mupya ianzishwe. Mu hali fulani, inaweza kuwa muzuri zaidi vikundi vidogo-vidogo vikuwe tu pamoya na kutaniko yenye kuwa karibu zaidi.
23 Wakati fulani, mu makutaniko ya kidogo munaweza kuwa tu wadada. Mu hali ya vile, kulingana na maagizo yenye kuwa mu Biblia, dada mwenye anatoa sala ao kuongoza mikutano anapaswa kufunika kichwa yake. (1 Ko. 11:3-16) Mara mingi wakati anaongoza, anapaswa kuwa mwenye kuikala mbele ya kikundi. Wadada hawafanyake hotuba ku mikutano. Lakini, wanasoma habari zenye kutolewa na tengenezo na kutoa maelezo juu ya zile habari, ao wakati fulani wanaweza kufanya vile kwa njia ya mazungumuzo ao maonyesho. Biro ya tawi itaomba dada moya kati yao akuwe napanga programu ya mikutano na kushugulikia mambo ya kuandikiana na kupokea barua zenye biro inatuma. Sasa kama mu ile kutaniko munakuwa ndugu wenye wanastahili kufanya ile kazi, wao njo wataanza kushugulikia ile mambo yote.
MIKUSANYIKO YA MUZUNGUKO
24 Kila mwaka, mipango inafanywaka ili makutaniko yenye kuwa mu muzunguko moya ifanye mikusanyiko mbili ya muzunguko, kila mukusanyiko unafanyaka siku moya. Inakuwaka wakati ya kufurahisha sana yenye inatoleaka wote nafasi ya ‘kufungua mioyo yao wazi’ kuelekea Wakristo wenzao. (2 Ko. 6:11-13) Kulingana na mahitaji ya pekee, tengenezo ya Yehova inatayarishaka programu yenye kuwa na vichwa mbalimbali vya hotuba vyenye kutegemea Biblia. Mafundisho inatolewa kwa njia ya hotuba, maonyesho, sehemu za kucheza upya mambo yenye ndugu walikutana nayo, sehemu za watu wenye kujisemesha, na sehemu za kuuliza mutu maulizo. Wale wenye wanakusanyika wanatiwaka moyo sana na ile mafundisho yenye inatolewaka kwa wakati yenye kufaa. Ku ile mikusanyiko, wanafunzi wapya wanabatizwaka ili kuonyesha kwamba walishajitoa kwa Yehova katika sala.
MIKUSANYIKO YA ENEO
25 Mara moya kila mwaka, mikusanyiko mikubwa zaidi inafanywa. Kwa kawaida, ile ni mikusanyiko ya eneo yenye inafanyaka siku tatu, yenye ndani munakuwaka makutaniko ya mizunguko mbalimbali. Pengine tawi za kidogo-kidogo zinaweza kuona kama ni muzuri makutaniko yote ya eneo yao ikusanyikie fasi moya. Mu inchi fulani, mipango kwa ajili ya ile mikusanyiko inaweza kubadilika kulingana na hali ao kulingana na miongozo yenye tengenezo inaweza kutoa. Wakati fulani, mu inchi mbalimbali munafanywa mikusanyiko ya kimataifa ao ya pekee. Mashahidi wa Yehova wengi sana wa kutoka mu inchi mingi wanaweza kuhuzuria. Kusema kweli, kwa miaka mingi watu wengi wamesikia habari njema ya Ufalme kupitia matangazo yenye inafanywaka kuhusu ile mikusanyiko mikubwa ya Mashahidi wa Yehova.
26 Watu wenye kujitoa kwa Yehova wanaona ile mikusanyiko kuwa nafasi ya muzuri kabisa ya kumuabudu Yehova mu umoja. Kwa kawaida mafasirio ya sasa juu ya kweli inatolewa. Wakati ingine kunaweza kutolewa vichapo vya sasa. Ni vichapo vyenye vinatusaidia mu funzo yetu ya kipekee, ku mikutano na hata mu kazi ya kuhubiri. Kunakuwaka pia ubatizo. Ile mikusanyiko ni ya lazima sana juu inafanya kukuwe maendeleo ya kiroho. Ile mikusanyiko inaonyesha wazi kwamba watu wa Yehova ni familia ya Kikristo yenye kujitoa kwa Mungu na yenye kuwa na umoja mu dunia yote. Na inaonyesha kama ni ndugu na dada wenye kuwa na alama yenye inawatambulisha kuwa wanafunzi wa Kristo.—Yoh. 13:35.
27 Mikutano ya kutaniko na mikusanyiko mikubwa inatutia moyo kabisa ili tuendelee kufanya mapenzi ya Yehova. Ile inatulinda pia tusiingie mu tabia ya mubaya yenye kuwa mu hii dunia yenye inaweza kufanya imani yetu ya Kikristo isikuwe nguvu. Ni mikusanyiko yenye iko namuletea Yehova sifa na utukufu. (Zb. 35:18; Mez. 14:28) Mu hizi siku za mwisho, tunamushukuru sana Yehova kwa kupatia watu wenye kujitoa kwake hizi nafasi za kukulishwa kiroho.
CHAKULA YA BWANA YA MANGARIBI
28 Mara moya kila mwaka, tarehe yenye Yesu Kristo alikufa, makutaniko ya Mashahidi wa Yehova mu dunia yote inafanyaka Ukumbusho wa kifo ya Kristo ao Chakula ya Bwana ya Mangaribi. (1 Ko. 11:20, 23, 24) Ile njo mukutano ya maana sana ya watumishi wa Yehova mu mwaka. Kusema kweli, kufanya Ukumbusho ni amri yenye tulipewa.—Lu. 22:19.
29 Tarehe ya Ukumbusho inapatana na tarehe ya Pasaka yenye inazungumuziwa mu Biblia. (Kut. 12:2, 6; Mt. 26:17, 20, 26) Kila mwaka Waisraeli walikuwa nafanya Pasaka ili kukumbuka siku walitoka mu inchi ya Misri, mu mwaka wa 1513 M.K.Y. Ile wakati, Yehova alichagua siku ya 14 ya mwezi wao wa kwanza kuwa tarehe ya kukumbuka kutoka kwao mu utumwa wa Misri. Mu ile tarehe walikuwa nakula mwana-kondoo wa Pasaka. (Kut. 12:1-51) Juu ya kujua ile tarehe, ni kuhesabia siku 13 kuanzia wakati mwezi mupya unaonekana kule Yerusalemu karibu na mwisho wa Mwezi wa 3 ao mwanzo wa Mwezi wa 4. Kwa kawaida, kila mwaka Ukumbusho unafanywa mu tarehe yenye mwezi wa kuenea unaonekana kwa mara ya kwanza kisha siku yenye usiku na muchana vinakuwaka na urefu moya.
30 Mu andiko ya Matayo 26:26-28, Yesu mwenyewe alisema namna Ukumbusho unapaswa kufanywa. Ukumbusho haiko sherehe yenye kuwa na mambo ya fumbo ao mambo yenye haieleweke. Ni chakula ya mufano, na ni wale wenye kuchaguliwa ili kutawala na Yesu Kristo mbinguni mu Ufalme wake njo wanakula mukate na kunywa divai. (Lu. 22:28-30) Wakristo wengine wote wenye walishajitoa kwa Yehova, na watu wote wenye kupendezwa wanaalikwa kuhuzuria Chakula ya Bwana ya Mangaribi; lakini wao ni watazamaji, ni kusema, hawatakula mukate wala kunywa divai. Kwa kuhuzuria Ukumbusho, wanaonyesha kwamba wanapendezwa sana na mupango wenye Yehova Mungu alifanya kupitia Mwana wake Yesu Kristo kwa faida ya wanadamu wote. Mbele ya kufanya Ukumbusho, hotuba ya pekee kwa ajili ya watu wote inatolewaka ili kutayarisha watu wafurahie ile tukio na ili kuchochea zaidi wale wenye kupendezwa wajifunze sana Biblia.
31 Mashahidi wa Yehova wanangojeaka kwa hamu na kwa furaha mikutano yao, juu ni kule njo ‘wanafikiriana ili kuchocheana katika upendo na matendo ya mazuri.’ (Ebr. 10:24) Kila mara mutumwa muaminifu na mwenye busara anatayarisha ile mikutano na mikusanyiko kulingana na mahitaji yetu ya kiroho. Watumishi wote wa Yehova na watu wengine wenye kupendezwa wanatiwa moyo kusamini ile mipango ya kukusanyika kwa ukawaida juu iwaletee faida. Wakati watu wa Mungu wanaonyesha kwamba wanapendezwa kwa moyo wote na mipango yenye Yehova anafanya kupitia tengenezo yake, wanaendelea kuungana na kuwa mu umoja. Lakini, jambo ya maana zaidi ni kwamba wakati tunakusanyika, tunamusifu na kumutukuza Yehova.—Zb. 111:1.