Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/12/06
“Mnamo kipindi hiki cha mwaka, watu wengi wanafikiria sana maneno ambayo malaika walitangaza wakati wa kuzaliwa kwa Yesu. [Soma Luka 2:14.] Je, unafikiri kwamba amani duniani itapatikana kweli? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia namna Yesu ataleta amani ya kweli duniani hivi karibuni.”
Amkeni! Mwezi wa 12
“Kuna maoni mengi ya kidini yenye kupingana kuhusu matumizi ya pombe. Unafikiri maoni ya Mungu ni nini kuhusu kunywa pombe? [Acha mtu ajibu.] Ijapokuwa muujiza wa kwanza wa Yesu ulikuwa kugeuza maji kuwa divai, Biblia inatoa pia onyo hili. [Soma Methali 20:1.] Gazeti hili linafasiria maoni ya Biblia yenye kusawazika kuhusu jambo hilo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 18.
Mnara wa Mlinzi 01/1/07
“Je, unafikiri kwamba ni mali ya mtu inayoonyesha kwamba anafanikiwa? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 1 Timotheo 6:9, 10.] Ijapokuwa Biblia haikataze kuwa na feza, inaonyesha kwamba mafanikio ya kweli hayatokani na mali. Gazeti hili linafasiria jambo hilo.”
Amkeni! Mwezi wa 1
“Je, unafikiri kwamba jambo hili litatimia wakati wowote? [Soma Isaya 33:24. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linafasiria mambo yanayotimizwa na sayansi ya kiganga na jinsi ahadi hiyo ya Biblia itakavyotimizwa.”